CUF Habari
JF-Expert Member
- Dec 12, 2019
- 239
- 234
MKUTANO MKUU WA TAIFA WA CUF CHAMA CHA WANANCHI UMEMPITISHA MUSSA HAJI KOMBO KUWA MGOMBEA WA URAIS ZANZIBAR KWA TIKETI YA CUF
Mkutano Mkuu Maalum wa Chama cha Wananchi (CUF) umempitisha Mussa Haji Kombo kuwa Mgombea wa Urais visiwani Zanzibar kwa asilimia 66 ya kura zote.
Wagombea wengine katika mchakato huo walikuwa Eng. Mohamed Habib Mnyaa aliyepata asilimia 19 za kura na Rajab Mbarouk Mohamed aliyepata asilimia 15.
Kwa upande wa Tanzania, CUF imepitisha Prof. Ibrahim Lipumba ambaye aliungwa mkono na asilimia 97% wa Wajumbe.