Mkutano Mkuu Wa CCM - Matarajio Ya Kujiokoa?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,988
Mkutano mkuu wa CCM unaanza wiki moja toka sasa na yawezekana katika historia ya CCM huo ndio mkutano mkubwa zaidi na wenye kupima mwelekeo wa CCM kwa miaka mingi ijayo. Mkutano Mkuu wa CCM kwa mujibu wa Katiba ya CCM Ibara 105:2 ndiyo Kikao cha Juu kabisa cha CCM na majukumu yake yanaathari kubwa zaidi katika mwelekeo wa sera na siasa wa nchi yetu.

Majukumu ya Mkutano Mkuu ni haya yafuatayo:

Kazi za Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa zitakuwa zifuatazo:-
(1) Kupanga Siasa ya CCM na kusimamia utekelezaji wa shughuli zote za CCM
(2) Kupokea na kufikiria taarifa ya kazi za CCM iliyotolewa na Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa na kutoa maelekezo ya mipango na utekelezaji wa Siasa ya CCM kwa kipindi kijacho.
(3) Kuthibitisha, kubadili, kukataa au kuvunja uamuzi wowote uliotolewa na kikao chochote cha chini yake au na mkuu yeyote wa CCM.
(4) Kubadili sehemu yoyote ya Katiba ya CCM kwa uamuzi wa theluthi mbili za Wajumbe walio na haki ya kupiga kura kutoka Tanzania Bara na theluthi mbili kutoka Tanzania Zanzibar.
(5) Unapofika wakati wa uchaguzi, Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa utashughulikia mambo yafuatayo:-
(a) Kuwachagua Mwenyekiti wa CCM na Makamu wa Mwenyekiti wa CCM.
(b) Kuchagua jina moja la Mwanachama atakayesimama katika uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
(c) Kuchagua jumla ya Wajumbe themanini na tano kutoka Tanzania Bara na Zanzibar wa kuingia katika Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa kutoka orodha ya Taifa.
(6) Kuunda Kamati za Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa kwa kadri itakavyoonekana inafaa.
(7) Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa waweza kukasimu madaraka yake kwa Halmashauri Kuu ya Taifa kuhusu utekelezaji wa kazi zake kwa kadri itakavyoona inafaa.

Kwa maneno mengine, wakati Kamati Kuu ina uwezo wa kufanya maamuzi fulani (kama kuwasimamisha kazi watendaji, Mkutano Mkuu unaweza kubadili maamuzi hayo) Kuna baadhi ya watu wanaoamini (mimi mmojawapo) kuwa Mkutano Mkuu una nguvu kuliko Bunge na maamuzi yake kwa upande wa CCM yana uwezo wa kubadili kabisa mwelekeo wa kisiasa wa chama na Tanzania.

Ni matarajio yangu kuwa ingawa kikao hiki ni cha Uchaguzi, ninaamini kuwa viongozi wa CCM watatumia nafasi hii pia kufanya maamuzi fulani muhimu kwani alama za nyakati haziko upande wao.

Wakichelewa kuzisoma alama hizo watajikuta kabla ya 2010 wanalazimika kuitisha Mkutano Mkuu usio wa Kawaida. Sijui wenzangu mnamatumaini gani au wasiwasi gani kuhusu wale watakaochaguliwa katika mkutano huu na mada hii itatrack nani anaanguka na nani anaibuka kidedea huko Dodoma!!

Nawatakia wajumbe wote safari njema Dodoma, na kutarajia watafanya zaidi ya kile walichofanya wabunge wao miezi michache iliyopita huko huko Dodoma! Na binafsi naomba kutumia nafasi hii kutoa udhuru kuwa kuanzia kesho sitaonekana sana humu kwa ajili ya maandalizi ya Mkutano huo Mkuu ambao natarajia kutuma ujumbe maalum.

M. M.
 
Wajumbe watakaohudhuria mkutano huu ndio wale wale waliokuwa Dodoma kumchagua mgombea wa CCM katika uchaguzi mkuu wa 2005. Hawa walichukua na kuifumbia macho rushwa iliyokuwa inatolewa bila kificho wala woga wowote. Na inasemekana mabilioni ya fedha yalimwaga katika kikao hicho toka kwa matajiri mbali mbali katika juhudi za kuwapigia debe wagombea wao.

Mimi sina imani na CCM, hiki chama kimeshaoza na kuna watu wachache wanaoweza kukinusuru chama hiki mmoja wao ni Butiku kwa kusema bila woga na kusema mbele ya Watanzania wote. Tatizo Butiku kishaanza kupigwa vita ndani ya CCM ili wamnyamazishe. Na wakiweza kumnyamazisha Butiku basi ndio CCM itakuwa inazidi kujitenga zaidi na Watanzania maana anayoyasema Butiku yanaungwa mkono na Watanzania wengi.
 
bubu ataka kusema

asitukane mamba na wewe hujavuka mto.

tusubiri tuone, ccm ni chama dynamic and flexibility ambacho huenda kutokana na mazingira, na ndio kikawa hakiko rigid sasa lolote jua laweza kutokea
 
bubu ataka kusema

asitukane mamba na wewe hujavuka mto.

tusubiri tuone, ccm ni chama dynamic and flexibility ambacho huenda kutokana na mazingira, na ndio kikawa hakiko rigid sasa lolote jua laweza kutokea

CCM ingekuwa ni chama dynamic na flexible kama unavyodai basi wangemsikiliza kwanza muasisi wa chama hicho Mwalimu Nyerere~Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema peponi, AMIN~ambaye siku nyingi alianza kusema hovyo kuhusiana na mwenendo ndani ya chama hicho, lakini mpaka anafariki hakuna mabadiliko yoyote yaliyofanywa ili kukisafisha chama hicho. Sasa kama hawakumsikiliza Mwalimu sidhani kama watakuwa tayari kumsikiliza yeyote ili kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya chama hicho. Labda hali halisi ndani ya Tanzania kuhusu kutoridhika kwa wananchi na matukio mbali mbali hadi kufikia kuzomewa viongozi yanaweza kuwaamsha toka kwenye usingizi mzito, tusubiri.
 
hivi hujui kuwa nyerere alikuwa rigid? yeye alin;ga;ngania ujamaaa, na laoto tungeendelea kuufata atakavyo tungetopea kwenye umaskini.

ccm inaamini kila zama na kitabu chake, na inasoma alama za nyakati kwa hiyo ww tulia uangalie halafu tuje tena tujadili
 
hivi hujui kuwa nyerere alikuwa rigid? yeye alin;ga;ngania ujamaaa, na laoto tungeendelea kuufata atakavyo tungetopea kwenye umaskini.

ccm inaamini kila zama na kitabu chake, na inasoma alama za nyakati kwa hiyo ww tulia uangalie halafu tuje tena tujadili

Umemsikia juzi Muungwana anasema kelele za wapinzani hazimkoseshi usingizi, anachoshindwa kuelewa kelele za wapinzani hazina tofauti na kelele za wananchi kuhusiana na ufisadi, ula rushwa, viongozi kujilimbikizia mali, mikataba mibovu, hali ngumu ya maisha na kutoona mafanikio yoyote katika usanii wa maisha bora kwa kila Mtanzania.

Sasa kama mwenyekiti wa CCM kishasema hivyo unafikiri wajumbe watakuwa na ubavu wa kumpinga mwenyekiti wao? Si umeona bunge la CCM? hovyo kabisa! na utabiri wangu katika mkutano mkuu wa chama kutakuwa hakuna jipya watajipongeza na kujifanya kila kitu ndani Tanzania kiko shwari kabisa na wataendelea kushika UTAMU.
 
Huo Mkutano sidhani una jipya,wote ni wala rushwa tu,labda Butiku anatoa hoja nzito huko,ni hayo tu.
 
hivi hujui kuwa nyerere alikuwa rigid? yeye alin;ga;ngania ujamaaa, na laoto tungeendelea kuufata atakavyo tungetopea kwenye umaskini.

ccm inaamini kila zama na kitabu chake, na inasoma alama za nyakati kwa hiyo ww tulia uangalie halafu tuje tena tujadili

Hebu fafanua kumfuata Nyerere tungepotea vipi katika umaskini? Na hao walioamua kutomfuata Mwalimu ni utajiri gani waliouleta kwa Watanzania?

Kama ndio ingekuwa hivyo si Watanzania wangewapongeza sana Mkapa na Kikwete na kumsahau kabisa Mwalimu aliyewaingiza kwenye umaskini wa kupindukia? Lakini ukweli ni kwamba Watanzania wanamuona Mwalimu ndiye kiongozi aliyejali na kuyaweka mbele maslahi ya Watanzania kinyume na Mkapa na Kikwete.
 
Homa ya wagombea yapanda

2007-10-30 10:29:25
Na Mary Edward, PST, Dodoma (Nipashe)


Wakati maandalizi ya Mkutano Mkuu wa CCM yakipamba moto, homa ya uchaguzi mkuu wa chama hicho imeendelea kupanda huku baadhi ya wagombea wakiwa wamewasili mjini Dodoma mapema zaidi, wakiwa na wapambe wao kwa ajili ya kufanya kampeni.

Uchunguzi unaonyesha kuwa walioamua kuwahi wamefanya hivyo ili kuongeza nguvu kwenye kampeni.

Kufiatia uchaguzi huo utakaofanyika Jumapili, tayari mji umefurika na karibu nyumba zote za wageni zilizopo katikati ya mji huu.

Mvutano mkali unatazamiwa kujitokeza kutokana na vigogo wa siasa na serikali, wasomi na wafanyabiashara wakubwa kujitosa kugombea nafasi mbali mbali za chama hicho katika ngazi ya taifa.

Mmoja wa wagombea wa NEC kampu la viti 20 aliyefika Dodoma siku tatu zilizopita kwa ajili ya kampeni alisema, kadiri siku zinavyozidi kusogea ndivyo presha ya mkutano huo inavyozidi kupanda.

``Uchaguzi wa safari huu ni mgumu mno, naweza kusema ni zaidi hata ule wa urais uliofanyika 2005 maana hata wale wanasiasa wazoefu wana presha ya kuchaguliwa au kubwagwa sembuse watu kama sisi ambao kwanza ni wachanga katika siasa na majina yetu hayafahamiki sana,`` alisema mgombea huyo akiomba jina lake tulitaje gazetini kwa sasa.

``Nimewahi ili kufanya kampeni kwa sababu sikuwa na uwezo wa kuzunguka mikoa yote kutembelea wajumbe kwa hiyo nitaitumia fursa hii ili angalau nami wanione kama walivyowaona wenzangu.``

Aidha alisema msuguano mkali zaidi upo katika viti hivyo 20 ambavyo vimegombewa na vigogo wakubwa serikalini na ndani ya chama?pamoja na wafanyabiashara wazito ambao kwa vyovyote uwezekano wa kushinda ni mkubwa mno.

Katika majengo yaliyopo kati kati ya mji kumebandikwa baadhi ya majina ya wagombea wakiomba kura, hali ambayo ni tofauti na uchaguzi wa 2005 ambapo vituko kama hivyo havikuwepo.

Wakati hayo yakiendelea maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa CCM unaotarajia kufanyika kwa siku tatu mjini hapa yamefikia asilimia 99, kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Yusuph Makamba.

Alisema katika uchaguzi huo CCM imealika wageni 550, kati yao 60 wanatoka nje na ni vyama marafiki zake, ambapo pia wamewaalika waasisi wa chama kutoka mikoa yote ya Bara na Visiwani wakiwemo wazee maarufu.

Bw. Makamba aliongeza kwamba vyama 13 kutoka nje vimealikwa na kwamba wawakilishi wa vyama vya upinzani pia wamealikwa.

``Wajumbe wote wanatakiwa wawe wamefika Dodoma kuanzia Novemba 2,`` alisema.

Alisema mada zitakazojalidiliwa kwenye mkutano huo ni pamoja na uchaguzi, taarifa ya chama katika kipindi cha miaka mitano pamoja na taarifa ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Bara na Visiwani.

Aidha katika hatua nyingine Bw. Makamba ametahadharisha wageni wanaokuja Dodoma?kuwa hivi sasa hakuna nafasi katika nyumba za kulala wageni kwani mbali na mkutano huo pia kuna kikao cha Bunge kinachoendelea kwa muda wa wiki tatu.

Aliongeza kwamba mkutano huo utakuwa na wajumbe 1,968 baada ya mmoja wa wajumbe wake aliyekuwa Naibu waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Salome Mbatia, kufariki dunia kwa ajali ya gari wiki iliyopita.
 
nyie mtakuwa kama fisi anavyongoje mikono ya mtu idondoke...

Wambie waelewe,CCM ina wenyewe,ila kitu kimoja ambacho nilikigusia kuhusu Muungwana kuwa ni Raisi ambae Tanzania haijawahi kumpata,CCM ina vikosi viwili kikosi kilichoko serikalini na kikosi hiki cha baraza kuu la CCM,huu uchaguzi unaokuja kunatabiriwa mchujo wa hali ya juu kabisa ambao utajaribu kusafisha trace zilizo ndani,ni kujaribu kuwaondoa mahasimu wake ambao wamekuwa wakichimba chini chini kumharibia njia anayotaka kuielekeza Tanzania na wananchi wake,hakuna asie jua kuwa Muungwana si chaguo la CCM chini ya Mkapa..
 
tusubiri tuone, ccm ni chama dynamic and flexibility ambacho huenda kutokana na mazingira, na ndio kikawa hakiko rigid sasa lolote jua laweza kutokea

Mtu wa Pwani, are you serious with this statement?
 
CCM ni kubwa sana kuliko watuhumiwa wa ufisadi, wanaoshitakiwa ni baadhi tu ya viongozi wachache wa CCM na serikali, sio wote ni wananchama wa CCM,

Matokeo ya udiwani majuzi ni majibu tosha toka kwa wananchi kwamba wanaelewa tofauti ya watuhumiwa na chama CCM,

CCM haihitaji kujiokoa, ni upinzani ndio wanaotakiwa kujiokoa, ili wakubalike na wananchi!
 
Kadaaaa!!! welcome back! yeah, that is deep... ni sawa na mtu kudai kuwa sihitaji kulitoa boriti langu kwa vile na wewe la kwako kubwa! Litoe la kwako la kwangu nimelizoea na watu wanalipenda!
 
Tatizo ni kuwa wewe mwenye liboliti kubwa unataka kuongoza watu.. sasa kabla hatujapata mtu mwingine wa kutuongoza ambaye tunaona anacho kibanzi, tunataka wewe unayetuongoza sasa utoe boriti lako. Ndio maana, hata huko Ulaya wanaoboronga wanaondolewa madarakani, kama haumini uliza Poland, Ukraine, Germany, France, na Ureno!! hata huko Uingereza Brown anaweza kutupwa nje baada ya kupewa UPremier mezani..!
 
Tatizo ni kuwa wewe mwenye liboliti kubwa unataka kuongoza watu.. sasa kabla hatujapata mtu mwingine wa kutuongoza ambaye tunaona anacho kibanzi, tunataka wewe unayetuongoza sasa utoe boriti lako.

Mkuu MMJ,

Heshima mbele, hivi kweli tondoe boriti kwa sababu tu Zitto, Slaa, Freeman, Mrema, na Marando, wanataka tuondoe boriti?

Yaaani tuwanyime haki wananchi 80%, waliotuchagua kutawala, na ambao hata juzi tu wamewakataa kwenye hata udiwani? Hivi mkuu anayetakiwa kuondoa boriti hapa ni nani aliyeshindwa au aliyeshinda?

Ushindi ni ushindi, mkuu hata wa udiwani ni ushindi na ni utabiri tosha kuhusiana na uchaguzi unaokuja, kule Europe, chama kikishindwa uchaguzi wowote ule, huwa viongozi wa juu wanatakiwa wajitoe, kama Gingrich alivyojitoa baada ya kushindwa uchaguzi wa wabunge tu! Sasa hapa bongo kwa sababu demokrasia yetu ni ya ki- Afrika, Afrika, upinzani ulioshindwa ndio unadai walioshinda watoke,

Hiv haya sio maajabu na kweli?
 
Back
Top Bottom