Mkutano Baraza Kuu CHADEMA: Hongera JamiiForums, Hongera Watetezi TV, Hongera Dar Mpya TV- Historia zitawakumbuka

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,224
26,039
Amani iwe nanyi wadau!

Naomba niende moja kwa moja kwenye mada. Leo Kuna mkutano muhimu wa Chama Kikuu cha Upinzani CHADEMA, ambapo macho na masikio ya watanzania wapenda demokrasia na wapenda maendeleo yapo kwenye mkutano huu wa CHADEMA. Moja ya ajenda kuu kwenye mkutano huu ni kumpitisha mgombea wa kiti cha uraisi atakaewakilisha Chadema kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu hapo October 2020.

Tofauti na ilivyokuwa kwenye mikutano wa Chama cha Mapinduzi ambapo Vyombo vya Habari vikubwa vya Tanzania yaani Azam Tv, Clouds Tv, ITV, TBC , Star Tv ukiondoa Channel Ten( Ambao hawa ni channel ya Chama cha mapinduzi) walikuwa wanarusha habari za mikutano ya CCM tena moja kwa moja. Vyombo hivi vilienda mbali kurusha hadi uchaguzi wa kura za maoni za wabunge wa CCM KWENYE Mikutano hii ya Chadema vyombo hivi vya habari vimeacha kwa makusudi kurusha habari za Chama hiki kikuu cha upinzani Tanzania. Sio tu kurusha live Ila hata kwenye pages zao havijaonekana kutoa updates za vikao hivi kama ilivyokuwa katika vikao vya CCM.

Ni vyombo vya habari vichache kama JamiiForums, Mwanahalisi Online, Watetezi Tv pamoja na Dar Mpya ambavyo viko live na vinatoa updates za mikutano ya Chadema. Vyombo vingine vibavyorusha matukio haya ni vya nje navyo ni DW na BBC SWAHILI, Hongereni sana maana historia itakayoandikwa mwaka huu hapo October kwenye uchaguzi Mkuu itawakumbuka.

Napenda kuviambia vyombo hivi vilivyojitoa ufahamu kwa kuwasupport CCM inayoelekea kufa kwa kuwanyima airtime Chadema kuwa baada ya October 2020 wasije sema kuwa wamekumbuka shuka asubuhi. Vijifunze kuwa huru, kutoa taarifa kwa usawa na kuvitreat vyama vyote vya siasa kwa usawa kwa sababu ya kesho ni Mungu tu anayajua.

Napenda kuwaambia pia TCRA pia ambao leo baada ya kuona vikao vya chadema vitaangaliwa mtandaoni kwa live streaming wakaamua kuhujumu kwa kupunguza nguvu ya internet kuwa nao Mungu amewaona. Tundu Lissu ni mpango wa Mungu.

Napenda kusema kwa kumalizia kuwa, Chadema ipo sawa, Chadema iko tayari, Chadema ni Nuru. Naiona Nuru kuu hapo October 2020.

Hongera Tundu Antipas Lissu. Huu ni mwanzo tu. Mungu anaenda kudhuhilisha ukuu wake kwako kwa kukupa rasmi uongozi wa nchi ya Tanzania hapo October 2020. Jiandae
 
Hivyo vyombo vinavyo ripoti mikutano ya CCM havifanyi hivyo kwa mapenzi yao, wanatangaza kwa sababu wanamuogopa yule jamaa, na vile vile hawatangazi mikutano ya Chadema sio kwa mapenzi yao, bali sababu ni ile ile wanamuogopa yule jamaa.

Kwa kifupi CCM wanalazimishwa kupendwa kwa sababu wanajua vizuri hawapendwi.
 
Hivyo vyombo vinavyo ripoti mikutano ya CCM havifanyi hivyo kwa mapenzi yao, wanatangaza kwa sababu wanamuogopa yule jamaa, na vile vile hawatangazi mikutano ya Chadema sio kwa mapenzi yao, bali sababu ni ile ile wanamuogopa yule jamaa.

Kwa kifupi CCM wanalazimishwa kupendwa kwa sababu wanajua vizuri hawapendwi.

Kwani chadema wamekatazwa kuvialika vyombo kuonesha live mkutano wao?
 
Hivyo vyombo vinavyo ripoti mikutano ya CCM havifanyi hivyo kwa mapenzi yao, wanatangaza kwa sababu wanamuogopa yule jamaa, na vile vile hawatangazi mikutano ya Chadema sio kwa mapenzi yao, bali sababu ni ile ile wanamuogopa yule jamaa.

Kwa kifupi CCM wanalazimishwa kupendwa kwa sababu wanajua vizuri hawapendwi.
Pamoja na kubana kote ila watu wamejikita kwenye online channels wanapambana ivo ivo kuangalia live. Hadi online channels zinazidiwa viewers. Kweli Lissu ni mpango wa Mungu
 
Ni ukweli mtupu kuhusu Nchi yetu imefikia mahali pabaya sana na hii ni baada ya miaka mitano tu, imagine baada ya miaka 10 hali itakuwaje kama huyo yesu fake ataiba uchaguzi.

Hivi ITV na Azam wameogopa hata kulisogelea eneo la mkutano....kweli nchi hii inahitaji ukombozi...

Tumefika pabaya mno kama taifa... taifa la watu waoga..
 
Hivi ITV na Azam wameogopa hata kulisogelea eneo la mkutano....kweli nchi hii inahitaji ukombozi...

Tumefika pabaya mno kama taifa... taifa la watu waoga..
Hii nchi imefika hatua mbaya sana ndugu. Acha tu Lissu ajitoe kweli kuwakomboa Watanzania. Ni aibu
 
Ni ukweli mtupu kuhusu Nchi yetu imefikia mahali pabaya sana na hii ni baada ya miaka mitano tu, imagine baada ya miaka 10 hali itakuwaje kama huyo yesu fake ataiba uchaguzi.
Huyu jamaa hatakiwi kuongezewa hata wiki moja ikulu. Ni kumuondoa tu baada ya matokeo ya uchaguzi October 2020 yanakayompa ushindi Lissu.
 
Hivyo vyombo vinavyo ripoti mikutano ya CCM havifanyi hivyo kwa mapenzi yao, wanatangaza kwa sababu wanamuogopa yule jamaa, na vile vile hawatangazi mikutano ya Chadema sio kwa mapenzi yao, bali sababu ni ile ile wanamuogopa yule jamaa.

Kwa kifupi CCM wanalazimishwa kupendwa kwa sababu wanajua vizuri hawapendwi.
Ccm wanlipia
 
Hivi ITV na Azam wameogopa hata kulisogelea eneo la mkutano....kweli nchi hii inahitaji ukombozi...

Tumefika pabaya mno kama taifa... taifa la watu waoga..
Yani unataka itv waoneshe mkutano wa chadema bure?
 
Vionyeshe mikutano ya cdm viwekwe kwenye black list ya jiwe?
Hawajui tu. Hata akiviweka kwenye blacklist mwisho wake kuongoza na kutawala Tanzania ni October 2020. Nguvu ya umma inaenda kumuweka Lissu madarakani hapo October 2020. Amini nakwambia ya Malawi yanaenda kutokea Tanzania
 
Back
Top Bottom