mkusanyiko wapongezaji Ikulu unahamasisha udokozi na kugoma kujiuzulu

KALABASH

JF-Expert Member
Jan 26, 2011
493
206
Miaka ya hivi karibuni kumeibuka utamaduni wa utiriri watu kukusanyika Ikulu siku ya wateule hususan mawaziri manaibu wao na makatibu wakuu wanapoapishwa. Atakuwepo mke/mume watoto wajukuu shangazi majirani marafiki na wengineo. Muda si mrefu hata watumishi wa ndani watajumuishwa kuwepo ikulu kumpongeza baba/mama kwa kuteuliwa kuwa waziri. Huu ni mwendelezo wa ile dhana ya "AMEULA" inayotumiwa mitaani na kwenye magazeti fulani wakati ukweli ni kwamba mteule huyo amebebeswha mzigo wa kuwatumikia wananchi. Matokea yake ni kwamba mara tu mteule huyo anapokalia kiti atafanya kila njia kukidhi mategemeo ya wale waliomzunguka na muda mwingi atatumia kupanga mikakati ya wizi udokozi wa mali ya umma rushwa etc na hata inapofikia kutakiwa kuachia ngazi inakuwa vigumu kila anapofikiria hao waliofika kumpongeza na matarajio yao kwake. Mikusanyiko hii Ikulu ya kupongezana haikuwepo awamu ya kwanza na sijui ilianza lini. Imefika wakati tubadilike.
Nawasilisha.
 
Ni kweli wengi wamekuwa wakifanya sherehe binafsi za mamilioni akijua sasa anakamata Wizara anaenda kuwa milionea.
 
huu nao ni uchuro wa serkali dhaifu hasa udhaifu wa maono wa kuona walioteuliwa ni kama wameula kutoka kwa kikwete mwnyewe
 
proponent wa kupongezana ni kikwete so i think he has cultivated this precedence by himself. what you see are just outcomes
 
huu nao ni uchuro wa serkali dhaifu hasa udhaifu wa maono wa kuona walioteuliwa ni kama wameula kutoka kwa kikwete mwnyewe

Mkuu ulichosema ni kweli. Ingependeza wewe au wa JF wengine mngetoa ushauri nini kifanyike kurekebisha hili jambo. Kumbuka hivi karibuni watateuliwa mawaziri wengine na ngoma vifijo na vigegelegele vya kupongezana vitahamia ikulu tena kuendeleza utamaduni ule ule wa "WAMEULA"
 
Back
Top Bottom