Mkurugenzi Wilaya ya Chamwino acha tabia ya kuwapiga Watumishi wa chini yako!

Huwa sipendi kusoma nyuzi kama hizi aiseeee....
Maana hua najiuliza maswali mengi na mwisho wa siki najikuta nang'ata meno kwa hasira tu...

Hata mimi huwa napandwa na hasira sana nikikuta nyuzi kama hizi aiseee maana kama tukio hili litanikuta mimi basi na kazi nitafukuzwa siku hiyo hiyo kamwe siwezi kukubali kuwa ng’ombe namna hii yani unapigwa tuu na wewe upo upo tuu
 
Nafikiri wanamuhurumia sababu ni mwanamama.
Ni kumchana live; apeleke ushenzi wake huko, kuna taratibu za kufuata kama kuna mambo hayako sawa kiutumishi.

waalimu amkeni acheni unyonge wa kishenzi.
 
Huyo boss itatokea siku kwenye piga piga yake
Atakutana na chizi !

Ova
Pia hajihurumii ni mwanamama anaweza kudharirika pia kuwasababishia matatizo familia za watu wengine,nafkiri wapigwaji walitumia hekima tu walikuwa na uwezo wa kumlalua tu
 
Siku ikitokea kwangu hata kama kuna ziara ya Rais, lazima nizindukie kama sio hospital basi mochwari. Yaani mtiti wake utatulizwa kwa kudhibitiwa na vyombo vya ulinzi na usalama. Makameraman lazima wasave video kiwizi. Sitakubali.
Halafu huu mtindo ulitakazoeleka enzi za mwenda zake.
 
Watu nchii hii damu ya upigaji imeota mizizi mi swali langu la msingi ni kwanini vifaa vyote vya ujenzi vinunuliwe na halmashauri kwani huko vijijini hakuna kamati za ujenzi nafkiri ilikuwa ni mwanya wakupiga pamoja na onyo la mama samia watu wameweka pamba masikioni.
Na michezo hii inafanywa geti la ikulu lipo mita chache wanataka kuijua rangi ya mama!!
 
Hata mimi huwa napandwa na hasira sana nikikuta nyuzi kama hizi aiseee maana kama tukio hili litanikuta mimi basi na kazi nitafukuzwa siku hiyo hiyo kamwe siwezi kukubali kuwa ng’ombe namna hii yani unapigwa tuu na wewe upo upo tuu
😀😀😀
 
Hapa ndio utaelewa kwa nini watoto wa Kikurya hufundishwa kupigana na kujihami tangu wangali wadogo siyo kama hiyo boya inapigwa halafu inakimbilia kwenye kibodi. Ulitakiwa uwe umeshatoa meno ya mtu hapa kabla ya kuandika uzi
Watani zangu na bangi nayo inachangia 🤣 🤣 🤣
 
Back
Top Bottom