Mkurugenzi wa upelelezi wa makosa ya jinai ataka wanaosambaza video ya mchele washughulikiwe

hawa watu si ndo wanasemaga raia walisaidie jeshi la polisi
kufichua waalifu na uhalifu kwa ujumla sasa hii imekaaje
 
Sawa yawezekana video clip haina ukweli,tunachoomba ikanushwe na kutufafanulia kile tunachokiona kinadunda ni nini?
 
Amefanya uchunguzi gani hadi kufikia hayo maamuzi!?

Navyojua hata nchi zilizoendelea watu wakirusha video clips wapelelezinndio itaka kukutana nao kujua kilichojiri... sasa huyu hata aliyetekodi hajasikia kutoka kwake na ni wapi anadai alinunua huo mchele anakimbilia kuongea hayo yote.

Kwa upande fulani maneno hayo bila yeye kutupa ukweli wa kutuambia kwanini anasema hakuna mchele wa plastic basi kazi ipo.

Afanye hayo kwanza kutueleza zaidi, sio wananchi wote tupo kusikiliza tu mtu kasema tunashangilia **** tunayotaka kusikia pia.

Hivi wafanyakazi wengi wa serikali kwa nini hawajui kuangalia nje ya box na kutuletea habari kamili...huwezi tu kusema hakuna huku huna hata cha kutueleza kwanini unasema hakuna.

Halafu unatisha wananchi, sasa yakitokea makubwa hamuyajui mnafikiri kuna atakayekuja kujitokeza kuyaongea au kuyaonyesha?

Hapo hao Polisi, Wizara, TFDA wote wajiongeze... eti fulani kasema hakuna... hata kama ni hivyo imekuwaje hamjawa na subira kuongea na hao watuhumiwa na kama kweli ndio mtuambie.

Raisi wetu anapiga kazi, tabu wengine kuongea tu basi. Rais wetu unahitaji vichwa vipya kukusaidia kuongoza nchi wavivu na wasio na maarifa wamejaa tele serikalini kwako.
Huu mchele utakuwa ni Mali ya lumu.ba
Mbn jamaa anawaka sana!

Ova
 
Ukimshtaki polisi wanatoa siri zako so hawa polisi sio wa kuwaamini kabisa
Ndio kisingizio upate uhalali wa kusema uongo, sio lazima polisi kuna TFDA, TBS, Mbunge wako, Mwenyekiti wa chama ukipendacho mbona hujulishi?
 
Kanunue mchele wa mpunga mpya, huu ndiyo msimu wake, upike halafu ukandamize uufanye matonge ya duara uone kama hautadunda. Tena mchele mpya ndiyo unadunda sana.

Hivi matumbo yenu yana mashine za kuyeyusha plastic ziwe mavi? Hamfikirii hata kiduchu?

Kamanda kamata hawa wajinga wote weka ndani, labda ndiyo watatia akili.


Unazifahamu dawa aina ya 'capsule'? Mtu anapokunywa hizo dawa, huwa anakunya mavi yenye capsule?

Au mtu akimeza dawa hizi zinaitwa rangimbili, mbona anakunya mavi ya kawaida. Hilo ganda (cover) huwa linayeyukia wapi humo mwilini?

Au mtu anaposhonwa nyuzi ambazo sio za kutoa (mfano baada ya kutahiri au upasuaji), hizo nyuzi huwa zinayeyukia wapi mwilini?

Yaani wewe akili zako zinakutaarifu kuwa mtu anayekula 'mchele wa plastic' ni lazima angekunya plastic pia?!! Punguani wa kichwa.

-Kaveli-
 
Unazifahamu dawa aina ya 'capsule'? Mtu anapokunywa hizo dawa, huwa anakunya mavi yenye capsule?

Au mtu akimeza dawa hizi zinaitwa rangimbili, mbona anakunya mavi ya kawaida. Hilo ganda (cover) huwa linayeyukia wapi humo mwilini?

Au mtu anaposhonwa nyuzi ambazo sio za kutoa (mfano baada ya kutahiri au upasuaji), hizo nyuzi huwa zinayeyukia wapi mwilini?

Yaani wewe akili zako zinakutaarifu kuwa mtu anayekula 'mchele wa plastic' ni lazima angekunya plastic pia?!! Punguani wa kichwa.

-Kaveli-
Nani alikudanganya kuwa capsules za kwenye dawa ni plastics?

Huo sasa ndiyo ujinga wa hali ya juu. Nenda kasome capsules zinatengenezwa na nini, usikute ni mchele au ngano au mahindi au muhogo.

Punguani wahed.
 
Huyu DCI naye vipi, sasa angejuaje kuna hivyo video bila watu kuisambaza? na kwa nini anasema ni kosa kabla ya kumhoji aliyefanya record ya ile VIDEO? je ameiona hiyo VIDEO? je kweli ni mchele wa kawaida au si wa kawaida?
Mboka kama DCI anakuwa aggressive kabla ya kulichunguza ili suala? maana kama lingekuwa limechunguzwa sasa hivi tungeaambiwa aliye record amefanya kosa gani na amekamatwa na kwamba ule mchele ni mchele gani

Kwa Ili DCI angejipima kwa kweli mimi kama mwananchi naona ametumia vitisho na hii italeta shida watu wakianza kuficha mambo yanayotokea kwenye jamii,
Kazi ya polisi ingekuwa kuchunguza na kupambana na wanao poteza jamii na sio kutisha watu kabla ya kufanya uchunguzi, watoe majibu kwanza huo mchele ni mchele gani

Mkurugenzi wa upelelezi wa Makosa ya jinai (DCI), Robert Boaz, ametoa onyo kali kwa watumiaji wa mitandao ya jamii kwa lengo la upotoshaji na kuliagiza Jeshi la polisi kuanza mara moja kuwashughuliakia na kuwachukulia hatua za kisheria watu wenye tabia hiyo.

Hayo yamezungumzwa na mkurugenzi huyo mara baada ya mitandao ya kijamii kusambaza video yenye habari inayonyesha uwepo wa mchele wa plastiki nchini.

Boaz amekanusha uwepo wa mchele huo wa plastiki na kumsaka kwa udi na uvumba mtu aliyerekodi video hiyo ili asaidie kutoa taarifa zaidi.

Na amewaomba wananchi kutumia vizuri mitandao ya kijamii na kujiepusha kusambaza taarifa zisizokuwa na ukweli, kwani ni hatari na husababisha madhara makubwa katika jamii.

”Kabla ya kusambaza taarifa kwanza uwe na uhakika wa vyanzo vyako, wahsuika wanaweza kuingia kwenye matatizo yasiyokuwa ya msingi”. amesema Boaz.

Aidha waziri wa Afya, maendeleo ya jamii, jinsia na wazee na watoto , Ummy Mwalimu ametaarifiwa na Mamlaka ya chakula na Dawa (TFDA), kuwa hakuna mchele wa aina hiyo nchini.

Waziri Ummy amewasisitizia watanzania kuwa makini na matumizi ya mitandao ya kijamii, na kuepuka upotoshaji.

Hii ni Taarifa ya TFDA
 
Eeeeeeh

Unaniandikia mimi na mimi nimeamua kukuuliza... ningekuwa sijaelewa unavyodai ungenijibu au kusema hauniongelei mimi FULL STOP
Ndio nakwambia hujaelewa!Halafu akili yako sijui haifanyi kazi vizuri,mimi nakujua mpaka nikuzungumzie wewe?Nafahamu unafanya shughuli gani mpaka nikuseme wewe?Muwe mnajiongeza!!!!Period
 
Kuna waziri alisema wanaotoa siri za serikali kukiona chamte makuni, sasa najiuliza na hizi pia huenda ndio siri za serikali eeh
 
hawa watu si ndo wanasemaga raia walisaidie jeshi la polisi
kufichua waalifu na uhalifu kwa ujumla sasa hii imekaaje
Acha tu...
kabla huja share video yeyote inabidi uombe kibali sijui...choka kabisa...
mi ile video niliiona nikashangaa...
Na nikiri nilimtumia ndugu yangu anisaidie kushangaa...
 
Sawa yawezekana video clip haina ukweli,tunachoomba ikanushwe na kutufafanulia kile tunachokiona kinadunda ni nini?
wewe unaongelea kudunda...
kuna video nyingine inaonyesha kiwanda kinavyotengeneza huo mchele toka kwenye maplastiki...
na kwa kweli inaogopesha...huwezi ukaiona ukafuta bila kutishwa kwanza kama hivi...utajikuta una share tu.
 
Back
Top Bottom