Uchaguzi 2020 Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC: Watanzania hawataki mtu atakayeuza madini yao kwa wageni nje

Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC, amesema watanzania wanataka Afya iliyoimarika, barabara nzuri, miradi ya umeme, elimu bora hawataki blah! Blah!

Amesema watanzania hawataki viongozi watakaochukua madini yao na kwenda kuyauza kwa wageni nje, watanzania wanataka viongozi watakaotetea madini yao

Ameyasema hayo alipokuwa anazungumza kumuandikia barua Tundu Lissu ili kutoa maelezo dhidi ya tuhuma za uongo anazotuhumiwa kuzitoa

Amesema Tundu Lissu amekuwa akitangaza matusi, tuhuma na kudanganya wafanyakazi badala ya kutangaza sera


==
YALIYOZUNGUMZWA KWENYE VIDEO YA MKURUGENZI WA UCHAGUZI NEC

Kwa mamlaka ya kisheria Tume iliyonayo, tayari imemuandikia Barua Mh. Tundu Lissu ya kumuita katika Kamati ya Maadili ya Kitaifa ili aje kutoa maelezo na ushahidi wa kile alichokisema katika mkutano wake huko Musoma.

Kwa mara nyengine tena Tume inawasihi Wagombea wa Vyama vyote kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi ili kulinda amani ya nchi yetu, katika kipindi cha kampeni kilichobaki kwa kujali muda wa kampeni, ratiba za kampeni na kuepuka matusi, sababu unatumia muda mwingi kutangaza matusi badala ya kutangaza sera, unatumia muda mwingi kutangaza tuhuma badala ya kutangaza sera, unatumia muda mwingi kuwadanganya Watanzania na wafanyakazi badala ya kutangaza sera.

Watanzania sasa hivi wanataka Afya iliyoimarika, Watanzania sasa hivi wanataka barabara nzuri, Watanzania sasa hivi wanataka miradi ya umeme, Watanzania sasa hivi wanataka elimu bora, Watanzania hawataki bra bra. Watanzania sasa hivi wanataka viongozi ambao watalinda madini yao, sio viongozi watakaokuja kuchukua madini yao na kupeleka kwa wageni nje.
Mbona haya ni maneno ya kampeni ya mgombea mmoja? Is this idiot impartial for real? Kumbe kumuondoa chizi lazima tupigane!!
 
Hivi hii Tume ni kwa ajili ya kusimamia uchaguzi au kufanya kampeni! Sio kazi ya Tume kuzungumzia mambo ya mgombea ambayo hayaingiliani na sheria zinazoongoza uchaguzi! Pia kitengo cha kutoa shutuma ambazo hazina ukweli ni uwongo na upotoshaji! Je wanaweza kutuambia ni lini wamemsikia mgombea akipanga kuuza hayo madini na kwani? Kwa bei gani? Kwa matamshi haya sioni kabisa uhalali wa tume kumuhoji Lissu wakati hata nao wanakiuka misingi na sheria zinazosimamia tume hiyo!
 
watawala wameshapanic sana, Magu keshalegea kulegea sana, Bashiru anawatisha tu wanaCCM, PolePole anavurumisha matusi, Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi ameingia kupiga kampeni

MWENYEZIMUNGU alimuacha hai TAL kwa makusudi yake na kwa kazi,ni mwendo wa MAPIGO 7
 
Mkurugenzi wa NEC hayo maneno ilibidi amuambie Kikwete,Mkapa na Magufuri maaana nae alikiwepo kwenye baraza LA mawaziri wakati wanasaini mikataba ya madini,hao ndio waliouza na wameuza madini yetu nje.Lissu amewahi kuuza madni tangu lini?:Naomba wanasheria wamfungulie kesi huyu Mahera
 
Yani mnatetea mtu anaetaka kuweka rehani ardhi yetu? Unajidai upo deep kumbe umejaza manyoya tu kichwani. Mkiona hamuwezi kuisapoti CCM bora mkae kimya kuliko kutetea uovu.
Mkuu hivi GGM na Barick inamilikiwa na mtanzania yupi?
Kweli nimegundua ndiyo maana wazungu na wachagga walipokuja Shinyanga,Geita,Simiyu nk enzi hizo walitukuta tunachezea dhahabu na almasi bao...VERY SAD
 
Mwambieni huyo mkurugenzi awapangie wanawe nani wa kumchagua sisi wengine tunamuona kiazi tu.
Nakumbuka alivyofokewa na Jerry Muro kule Arumeru huyo jamaa anaongea ukhanithi kwa kulinda tumbo lake.
 
Kilichotokea katika historia ya medani za siasa Tanzania ni kitendo cha aibu sana. Ni kama vile cross ya kona inapigwa na refarii yupo busy kusaka kuunganisha mpira wa kona ili kuifungia timu pendwa.

Ni kama vile refarii anatoa penati harafu anang'ang'ania kupiga mwenyewe.

Ni kama vile faulo ya wazi imefanyika golini kwa timu pendwa, na refarii kujipanga kwenye safu ya difensi kuzuia goli lisiingie.


Hii ni aibu kubwa kwa refarii na aliyemteua.
 
Mungu wangu sio kwa kujisahau huku ...hii evidence mambo yakienda vibaya itamuweka pabaya mno...
Bila kutaraji kajionesha rangi zake halisi
Mkuu bila kutarajia!!! No, huyu ni ignorant hata by facial expression tu ukimwangalia! Ndiyo maana aliwahifokewa hata na mkuu wa wilaya Muro! Huyu kwa nchi za wenzetu hata kazi ya kutunza mafali hawezipata!
 
Kilichotokea katika historia ya medani za siasa Tanzania ni kitendo cha aibu sana. Ni kama vile cross ya kona inapigwa na refarii yupo busy kusaka kuunganisha mpira wa kona ili kuifungia timu pendwa...
Kwa lugha rahisi tunaita kujitoa ufahamu ' unscrupulous '
 
Hyo NeC Isipoangalia safari hii italipuliwa ibakie magofu
Hakika.wanaudhi sana,ila tumuombee mh Tal aendelee kutupa ujasiri.watanzania tuamke kwa ajili ya maendeleo yetu.Jiwe AME fail hana exposure.ni mjamaa very primitive.
 
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC, amesema watanzania wanataka Afya iliyoimarika, barabara nzuri, miradi ya umeme, elimu bora hawataki blah! Blah!..
Nchi hii inachekesha sana......eti huyu ndio mwenyekiti wa tume ya uchaguzi...very strange....
Huyu ni doctor wa nini .....elimu zetu hizi
 
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC, amesema watanzania wanataka Afya iliyoimarika, barabara nzuri, miradi ya umeme, elimu bora hawataki blah! Blah!

Amesema watanzania hawataki viongozi watakaochukua madini yao na kwenda kuyauza kwa wageni nje, watanzania wanataka viongozi watakaotetea madini yao...
Waache watanzania waamue wanataka nini wewe baki kama refa usiingie uwanjani kumsaidia moja wa washindani. Ujiulize mkataba wa madini ulioanzisha kampuni ya Twiga inalinda madini yetu?
 
Nchi hii inachekesha sana......eti huyu ndio mwenyekiti wa tume ya uchaguzi...very strange....
Huyu ni doctor wa nini .....elimu zetu hizi
Hana lolote huyu,ni jamaa mwalimu Wa equation balance, logarithm, etc.Hana ufahamu na mambo ya political science, sheria etc.
 
Back
Top Bottom