Mkurugenzi wa TPA aliyesimamishwa kazi, Kakoko ashikiliwa kwa mahojiano na TAKUKURU

View attachment 1738405
Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brigedia Jenerali John Mbungo amethibitisha taasisi hiyo kumshikilia kwa mahojiano Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Deusdedit Kakoko aliyesimamishwa kazi na Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan.

Hivi Karibuni Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan alimsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini TPA Mhandisi Deusdedit Kakoko, kupisha uchunguzi wa ubadhirifu wa fedha bandarini.

Rais Samia alifanya uamuzi huo Jumapili, Machi 28, 2021 baada ya kupokea ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Takukuru Ikulu ya Chamwino, Dodoma.

“Ripoti nimeona, nimeipitia na nimebaini ubadhirifu mkubwa uliofanywa pale bandari, hili suala mnatakiwa kushirikiana, nakuomba Takukuru jishughulishe pale, alipita Waziri Mkuu alilishughulikia.

“Waziri Mkuu aliunda kamati na wakafanya uchunguzi kidogo ambao yaliyotoka, hatua chache zilichukuliwa lakini imani yangu ni kwamba kama kuna ubadhirifu pale waliosimamishwa ni hawa wa chini huku, ninaomba mara moja nitoe agizo la kumsimamisha Mkurugenzi Mkuu wa Bandari halafu hatua zaidi ziendelee,” alisema Rais Samia.

Hawa ni wa kufungwa tu ,hauwezi kucheka na majizi.
 
Huyo jamaa inaonekana alikuwa mpigaji, kajificha kwenye kichaka cha kuaminiwa na Magufuli. TAKUKURU endeleni kuusaka uhalifu wote na mtandao huo uliokuwa TPA.
Ilikuwa hvy mkuu huy bwana alikuwa anachenga anawauzia masara wachin koo hayati mh alikuwa akifika inaonekana yeye yuko sahihi kutimuliwa kunamkosa sasa mwisho wake umewadia maana kasabisha wengi sana kuondoka
 
... bora wapotezee tu maana Jua laweza kugeuza direction; likaanzia West to East! Miradi ile itakuwa na madudu ya hatari!
Umeona eee! Bunge halijawahi kupitisha bajeti yake. Inaonekana huyu Kakoko alikuwa mshirika wa mwendazake
 
Gazeti la the Citizen online limeandika kwamba Kakoko alikamatiwa Morogoro akiwa njiani kukimbia nchi.
 
Sisi wananchi tunataka hapo TPA Kusafishwe, watendaji wote hapo wananuka, hakuna aliye msafi, Takukuru jiongezeni, mhe Rais amewapa tu clue sasa kazi kwenu, hapo Bandari ni ufisiadi tu, wazee kwa vijana wanapiga dili tu.
 
Umeona eee! Bunge halijawahi kupitisha bajeti yake. Inaonekana huyu Kakoko alikuwa mshirika wa mwendazake
... fikiria mtu akihemuka anagawa fedha mabarabarani hadi unajiuliza ni mshahara wake au zinatoka fungu gani hizi? Hakuna kanuni yoyote ya fedha inayoruhusu kitu kama hicho!
 
Bodi ya TPA Pia itakuwa imechangia ubadhirifu huu, ilikuwa wapi?
ni vyema pia wajumbe wa Bodi ya TPA wakachunguzwe kwa undani maana kuna kila dalili......uchunguzi ufanyike kwa wote.
na hatua kali zichukuliwe dhidi yao maaana hao ndio wachawi wa maendeleo ya nchi yetu.
tusioneane haya wala hakuna kuangaliana sura.
 
Kakoko analaumiwa sana Kwa kudharau kila mtu, kutukana wafanyakazi na kuwatishia, style yake ilikua ni copy and paste na watu wengi katika mawizara na idara mbali mbali za Serikali.

Kakoko unalaumiwa pia kujifanya Mungu mtu kwenye kazi za umma umenyanyasa sana watumishi wenzio lakini ukasahau ya Dunia hii ni mengi.

mko wengi na wote kwa nyakati tofauti Mungu atawalipa hapa hapa Duniani.
Mmeumiza watu sana
 
Back
Top Bottom