Trust None
JF-Expert Member
- Feb 12, 2018
- 1,260
- 4,415
Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brigedia Jenerali John Mbungo amethibitisha taasisi hiyo kumshikilia kwa mahojiano Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Deusdedit Kakoko aliyesimamishwa kazi na Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan.
Hivi Karibuni Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan alimsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini TPA Mhandisi Deusdedit Kakoko, kupisha uchunguzi wa ubadhirifu wa fedha bandarini.
Rais Samia alifanya uamuzi huo Jumapili, Machi 28, 2021 baada ya kupokea ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Takukuru Ikulu ya Chamwino, Dodoma.
“Ripoti nimeona, nimeipitia na nimebaini ubadhirifu mkubwa uliofanywa pale bandari, hili suala mnatakiwa kushirikiana, nakuomba Takukuru jishughulishe pale, alipita Waziri Mkuu alilishughulikia.
“Waziri Mkuu aliunda kamati na wakafanya uchunguzi kidogo ambao yaliyotoka, hatua chache zilichukuliwa lakini imani yangu ni kwamba kama kuna ubadhirifu pale waliosimamishwa ni hawa wa chini huku, ninaomba mara moja nitoe agizo la kumsimamisha Mkurugenzi Mkuu wa Bandari halafu hatua zaidi ziendelee,” alisema Rais Samia.