Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke aache kutisha na kufedhehesha Waandishi wa Habari

Wacha wavune walichopanda.

Ilibidi toka kitambo wasuse kuzipa airtime taarifa za serikali wakati ule wanafungiwa fungiwa. Wangeheshimiwa.

Walizidi kulamba miguu ya serikali wakati ule wenzao wanafungiwa.
 
Ni aibu sana kwangu kuwa kabila moja na DED Mshamba kama huyu, aliyeletwa Temeke baada ya kuiba kura Kakonko.
 
Naunga mkono hoja!

Kitendo cha mkurugenzi wa manispaa ya Temeke kujimwambafy kwamba hawezi kuongea na waandishi wadogo wadogo na kumtaka Richard Stephen akamwambie mkurugenzi wa ITV ampigie simu kwa sababu ndiye level yake kinatia kinyaa sana.

cc: DC Godwin Gondwe
Huyo Gondwe uliyempelekea kopi hana mamlaka yoyote kwa DED, mwenzake alifanikisha wizi wa kura Kakonko, sasa yeye ukabila tu ndio unambeba, atafanyaje?
 
Sio kweli huyo jamaa pesa anayokitambo tu na sio mtu wa njaa sema Ni amezaliwa hivyo Ni mtu mpenda sifa na utani wa hapa na pale .

Namjua kwa kias chake coz tunatoka sehem moja huko Budokelo -Mbeya .

Kwanza jamaa wanadai Ni kitengo.

Pia huyu jamaa kudhihirisha kuwa hana njaa huko kijijin kwao amejenga bonge moja la bangaloo Ni hatar na nusu .

So elewa jamaa hana njaa kabisa wala hawez kulewa kamshahara ka Uded so uelewe jamaa ndivyo alivyo zaliwa ,utani mwingi ,vituko vya hapa na pale ,sifa za hapa na pale ,pia Ni mtu wa watu sana hana shida.
Nahisi wewe ndiyo Ded mwenyewe
 
Mkuu,

Ni kweli majibu ya Mkurugenzi hayakuwa na hekima ya kiuongozi, sauti ilikuwa ni ya kutishia wakati akijua fika kabisa kuwa mwandishi katika utafutaji wake wa taarifa alikutana na wananchi hao ndipo wakaanza kutoa kero zao kwa manufaa ya umma. Mpaka hapo mwandishi hana kosa lolote, alichotakiwa kama hakupenda kutoa majibu kupitia simu angempangia siku mwandishi amfuate ofisini kwake ili apate ufafanuzi kutokana na sintofamu ya malalamiko ya wananchi kuliko kudai mwandishi huyo hana sifa ya kuongea naye labda amtaarifu Mkurugenzi wa chombo husika cha habari ampigie simu hizo ni dharau pamoja na kwamba wananchi wana hasira lakini pia ametengeneza hasira dhidi ya wamiliki wa vyombo vya habari.

USHAURI

Mamlaka husika (DC TEMEKE & MKUU WA MKOA DSM) imwonye huyo mkurugenzi na aombe radhi kwa kusababisha sintofamu kwenye jambo ambalo lilihitaji ufafanuzi tu ili mwandishi aiweke taarifa yake kwenye mizania sawia.

Mamlaka ya uteuzi (RAIS) Akishupaza shingo aondolewe kwenye nafasi hiyo maana hayupo kwa ajili ya kutatua kero za wananchi
 
Hayo majibu hutolewa na walio lewa madraka au alipigiwa simu akiwa katika hali ya msongo mawazo.

Yote kwa yote ni majibu ya kuudhi yasiyo stahili kutolewa na kiongozi au mtendaji wa shughuli kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania.
 
Nauliza tu
20201117_215306.jpg
 
Aligombea Busokelo, siyo Rungwe. Wilaya ya Rungwe ina majimbo ya uchaguzi mawili: Busokelo (awali Rungwe Mashariki) na Rungwe (awali Rungwe Magharibi)
Mwaka 2015 aligombea ubunge Rungwe akashindwa kura za maoni.

Akateuliwa kuwa mkurugenzi wilaya fulani huko Kigoma.

Baada ya uchaguzi mdogo huko ambao ulotokana na kifo cha Kasuku Bilago wa CHADEMA, na CHADEMA kupoteza Jimbo wakiwa na Eliya Michael wao, ambaye kwa sasa nasikia ni kada kindakindaki na mtendaji kata, Mwaka alihamishiwa TMK
 
Back
Top Bottom