Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke aache kutisha na kufedhehesha Waandishi wa Habari

Jana wakati nafuatilia taarifa ya habari ITV saa mbili usiku niliona mgogoro ulipo katika kiwanja mojawapo kilichopo Yombo wilaya ya Temeke lakini wakati mwandishi wa habari anatafuta ukweli wa jambo hilo alipojaribu kumpigia simu Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke ajulikanaye kwa jina la Lusubilo Mwakabibi nataka ufafanuzi wa mgogoro huo kwa kuomba nafasi ya kuonana naye ofisi kwake aliishia kujibiwa kuwa huyo mwandishi hana hadhi ya kuonana naye! Swali ni je wenye hadhi ya kuonana na viongozi hawa ni waandishi wa namna gani?
Hiki ni kiburi wanachokipata kutoka kwa bwana yule. Like father like son!

Hakuna wa kumuwajibisha kwasababu maji hufuata mkondo!
 
Huyu Mkurugenzi ni kiongozi wa hovyo kuwahi kutokea. Nilisikia mbwembwe zake. Hana sifa ya kuwa kiongozi bali jambazi. Nafikiri ana backup nzuri ya kufanikisha yakiyofanikishwa hivyo ndiyo maana alipayuka hovyo. Kiongozi hana maadili. Very poor communication skills.
Backup gani bhana, kama hawezi kufanya kazi za wananchi na wananchi arudi nyumbani kwake akakurugenzi familia yake. Wanaotafuta kazi na wenye sifa za kuwa wakurugenzi wako wengi
 
Naomba unielewe Ndugu sipo hapa kumsafisha huyo jamaa .ila nimekwambia ndivyo alivyo hayupogo sirias sana Ni mropokaj sana .

Sasa nimsafishe kwa kipi ,nimeongea ivo coz namjua kwa kiasi maana natoka nae sehem moja japo vijiji tofaut huko Busokelo-Mbeya .

Hata huko home Ni maaluf sana sabab ya vituko vyake vya hapa na pale ,lakin tukirud kwenye ukwel jamaa hana shida kabisa na Ni mtu wa watu sana

Hapa sasa ndio umeongea ukweli uliposema jamaa ni mropokaji, hapaswi kuropoka hovyo
 
Sio kweli huyo jamaa pesa anayokitambo tu na sio mtu wa njaa sema Ni amezaliwa hivyo Ni mtu mpenda sifa na utani wa hapa na pale .

Namjua kwa kias chake coz tunatoka sehem moja huko Budokelo -Mbeya .

Kwanza jamaa wanadai Ni kitengo.

Pia huyu jamaa kudhihirisha kuwa hana njaa huko kijijin kwao amejenga bonge moja la bangaloo Ni hatar na nusu .

So elewa jamaa hana njaa kabisa wala hawez kulewa kamshahara ka Uded so uelewe jamaa ndivyo alivyo zaliwa ,utani mwingi ,vituko vya hapa na pale ,sifa za hapa na pale ,pia Ni mtu wa watu sana hana shida.
Yaani kwamba mtu akijenga jumba zuri mkoani ndio anakuwa hana njaa? Au mimi sijaelewa
 
Boss wao aliwahi kuombwa lami enzi hizo huko jimboni kwake akawaambia wananchi kunyeni mavi yakishakauka yatageuka kua lami.

Kwahio sishangai sana majibu ya hawa manyokaa wake.
 
Jana wakati nafuatilia taarifa ya habari ITV saa mbili usiku niliona mgogoro ulipo katika kiwanja mojawapo kilichopo Yombo wilaya ya Temeke lakini wakati mwandishi wa habari anatafuta ukweli wa jambo hilo alipojaribu kumpigia simu Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke ajulikanaye kwa jina la Lusubilo Mwakabibi nataka ufafanuzi wa mgogoro huo kwa kuomba nafasi ya kuonana naye ofisi kwake aliishia kujibiwa kuwa huyo mwandishi hana hadhi ya kuonana naye! Swali ni je wenye hadhi ya kuonana na viongozi hawa ni waandishi wa namna gani?
Wenye pesa zao labda
 
MKURUGENZI WA MANISPAA YA TEMEKE AACHE KUTISHA NA KUFEDHEHESHA WAANDISHI WA HABARI!

Tarehe 2 Desemba 2020, ITV ilikuwa na taarifa kuhusu kero ya wananchi katika Manispaa ya Temeke. Mkurugenzi wa Manispaa ambaye ni Mteule wa Rais anapigiwa simu na mwandishi wa habari wa ITV kutaka ufafanuzi kuhusu jambo muhimu la kijamii lenye masilahi kwa taifa.

Badala ya kujibu au kutoa ushirikiano kwa mwandishi wa habari, yeye anaamua kumfokea mwandishi wa habari kwa kumwambia kuwa, yeye (Mkurugenzi) siyo saizi yake (mwandishi wa Habari), hivyo aliyetakiwa kumpigia simu Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke ni Mkurugenzi [wa ITV?] na wala siyo mwandishi yule wa habari.


Vyombo vya Habari na Waandishi wa Habari katika nchi hii wasipozinduka watakuwa wanakaripiwa na kila Mtendaji wa Serikali. Uhuru wa Vyombo vya Habari katika nchi hii umewekwa mfukoni mwa Serikali na hili la Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke kumfokea mwandishi wa Habari wa ITV ni kielelezo kimojawapo!

Tunamuonya Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke, ndugu Lusubilo Mwakabibi, kuacha tabia ya kuwafokea, kuwadharau na kuwatisha waandishi wa habari. Anahitaji kuwa mnyenyekevu kwa kuwa anakalia ofisi ya umma inayoendeshwa kwa kodi za Watanzania! Kama tuliwahi kuwakemea na kuwaonya wengine, ni wajibu wetu kumkemea na kumuonya na yeye pia! Tunaomba rehema kwake ili atambue kuwa alilofanya halikuwa jema machoni pa Watanzania.

Tunaishauri Serikali isianze kumfuatilia Mwandishi wa ITV aliyeripoti tukio lile na wala ITV isifuatiliwe kwa kurusha hewani tukio lile. Badala yake Serikali ijikite katika kuwaonya na kuwaelekeza watendaji wake kujirekebisha. Tunamshauri pia Mwakabibi asianze kumfuatilia mwandishi, bali ikiwezekana amuombe msamaha mwandishi yule na ITV yenyewe kwa kumnyanyasa mwandishi wake!

Tunatimiza wajibu wetu wa kikuhani kwa Serikali na jamii kwa ujumla (Ezekieli 33:1-20)!

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula - Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki
 
Mwakabibi kuwa DED na kwa vile alishiriki kuiba kura Kakonko basi anajiona mungu mtu , nimemdharau sana ! Hivyo vijimadaraka alivyonavyo ni dhamana ya muda mfupi sana .
 
Jana wakati nafuatilia taarifa ya habari ITV saa mbili usiku niliona mgogoro ulipo katika kiwanja mojawapo kilichopo Yombo wilaya ya Temeke lakini wakati mwandishi wa habari anatafuta ukweli wa jambo hilo alipojaribu kumpigia simu Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke ajulikanaye kwa jina la Lusubilo Mwakabibi nataka ufafanuzi wa mgogoro huo kwa kuomba nafasi ya kuonana naye ofisi kwake aliishia kujibiwa kuwa huyo mwandishi hana hadhi ya kuonana naye! Swali ni je wenye hadhi ya kuonana na viongozi hawa ni waandishi wa namna gani?
Amefanya kama wakubwa zake, hakuna jipya.
 
Sio kweli huyo jamaa pesa anayokitambo tu na sio mtu wa njaa sema Ni amezaliwa hivyo Ni mtu mpenda sifa na utani wa hapa na pale .

Namjua kwa kias chake coz tunatoka sehem moja huko Budokelo -Mbeya .

Kwanza jamaa wanadai Ni kitengo.

Pia huyu jamaa kudhihirisha kuwa hana njaa huko kijijin kwao amejenga bonge moja la bangaloo Ni hatar na nusu .

So elewa jamaa hana njaa kabisa wala hawez kulewa kamshahara ka Uded so uelewe jamaa ndivyo alivyo zaliwa ,utani mwingi ,vituko vya hapa na pale ,sifa za hapa na pale ,pia Ni mtu wa watu sana hana shida.
wewe DED cha ulimbukeni, leo upo kesho utaacha hiyo ofisi
 
Sio kweli huyo jamaa pesa anayokitambo tu na sio mtu wa njaa sema Ni amezaliwa hivyo Ni mtu mpenda sifa na utani wa hapa na pale .

Namjua kwa kias chake coz tunatoka sehem moja huko Budokelo -Mbeya .

Kwanza jamaa wanadai Ni kitengo.

Pia huyu jamaa kudhihirisha kuwa hana njaa huko kijijin kwao amejenga bonge moja la bangaloo Ni hatar na nusu .

So elewa jamaa hana njaa kabisa wala hawez kulewa kamshahara ka Uded so uelewe jamaa ndivyo alivyo zaliwa ,utani mwingi ,vituko vya hapa na pale ,sifa za hapa na pale ,pia Ni mtu wa watu sana hana shida.
Mzee unamsifia mwanaume mwenzako hata chawa hafikii huko, usizoee sana wanaume tunaweza waza mengine. Labda kama una jinsia ya kike. Mwambie jamaa usilete utani kazini wamedondoshwa hadi mawaziri wakuu. Kitengo ni nani
 
19 Reactions
Reply
Back
Top Bottom