Malipo ya posho ya walimu ya kuanza kazi kwa ajili ya sensa yameingia dosari jijini Mwanza kuhusu njia ya kuwalipa walimu hao kwa sensa inayofanyika kesho nchini.
Walimu wanaohusika na zoezi hilo walijulishwa kwamba wakusanyike kwenye vituo vya Kata ambako watalipwa fedha hizo. Mapema leo asubuhi walimu wakakusanyika vituoni.
Lakini wakiwa vituoni wakapewa taarifa kwamba itakuwa ni vigumu kuzungukia vituo vyote na hivyo waondoke vituoni na wote wakutane Mwanza Secondary School ambayo kwa kifupi huitwa Mwanza Seco na ndiko malipo yatakapofanyika na si tena vituoni hapo.
Walipofika Mwanza Seco walimu wamesubiri wakijua watalipwa lakini dakika kama 20 zilizopita wakaambiwa kwamba hawatalipwa tena hapo Mwanza Seco kwa sababu Mkurugenzi wa Jiji amekosa escort. Hivyo, walimu wakaambiwa wafunge safari tena kutoka Mwanza Seco hadi Halmashauri ya Jiji.
Kutokana na usumbufu huu kumezuka fujo na aina fulani ya mgomo hadi kuleta hisia kwamba kuna njama ziko juu ya hii danadana ukichukulia kwamba kuna mwalimu anayeweza kuwa ametembea umbali kadhaa kutoka kituo cha nyumbani kwenda kituo cha Kata, ksha umbali toka kituo cha kata hadi Mwanza Seco, na sasa atatakiwa kutoka Mwanza Seco hadi Jiji ambako ni umbali wa kilomita tatu.
Kutokana na mtafaruku huu hadi dakika hii hakuna imani ni nini kinaendelea na hivyo wapo waliokata tamaa. Nusu wameamua kufunga safari ya tatu kuondoka hapo Mwanza Seco kwenda Jiji na nusu wameamua kubaki kwa sababu kwamba kama ni tatizo la escort basi hilo si lao wao kama walimu haliwahusu kwa sababu wamevumilia safari ya kutoka vituo vya kata na hakuna sababu ya kusumbuliwa kuondoka Mwanza Seco kwenda pengine tena.
Waandishi mliomo humu JF, habari ndiyo hiyo!
Walimu wanaohusika na zoezi hilo walijulishwa kwamba wakusanyike kwenye vituo vya Kata ambako watalipwa fedha hizo. Mapema leo asubuhi walimu wakakusanyika vituoni.
Lakini wakiwa vituoni wakapewa taarifa kwamba itakuwa ni vigumu kuzungukia vituo vyote na hivyo waondoke vituoni na wote wakutane Mwanza Secondary School ambayo kwa kifupi huitwa Mwanza Seco na ndiko malipo yatakapofanyika na si tena vituoni hapo.
Walipofika Mwanza Seco walimu wamesubiri wakijua watalipwa lakini dakika kama 20 zilizopita wakaambiwa kwamba hawatalipwa tena hapo Mwanza Seco kwa sababu Mkurugenzi wa Jiji amekosa escort. Hivyo, walimu wakaambiwa wafunge safari tena kutoka Mwanza Seco hadi Halmashauri ya Jiji.
Kutokana na usumbufu huu kumezuka fujo na aina fulani ya mgomo hadi kuleta hisia kwamba kuna njama ziko juu ya hii danadana ukichukulia kwamba kuna mwalimu anayeweza kuwa ametembea umbali kadhaa kutoka kituo cha nyumbani kwenda kituo cha Kata, ksha umbali toka kituo cha kata hadi Mwanza Seco, na sasa atatakiwa kutoka Mwanza Seco hadi Jiji ambako ni umbali wa kilomita tatu.
Kutokana na mtafaruku huu hadi dakika hii hakuna imani ni nini kinaendelea na hivyo wapo waliokata tamaa. Nusu wameamua kufunga safari ya tatu kuondoka hapo Mwanza Seco kwenda Jiji na nusu wameamua kubaki kwa sababu kwamba kama ni tatizo la escort basi hilo si lao wao kama walimu haliwahusu kwa sababu wamevumilia safari ya kutoka vituo vya kata na hakuna sababu ya kusumbuliwa kuondoka Mwanza Seco kwenda pengine tena.
Waandishi mliomo humu JF, habari ndiyo hiyo!