Mkurugenzi wa Barrick Gold adai Makinikia yaliyozuiwa Bandarini Dar yana thamani ya $280 Milioni

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,172
23,975
Wakati akiongea na shirika la habari ya Uingereza liitwalo Reuters, Mkurugenzi wa Kampuni ya Barrick Gold, Mark Bristow amesema Makontena ya Makinikia yaliyozuiwa na serikali ya Tanzania Bandarini Dar es Salaam yana thamani ya Dola za Kimarekani milioni 280 ambapo ni sawa na takribani shilingi za Kitanzania bilioni 647.

Mkurugenzi huyo amesema kwa sasa wako mbioni kutekeleza makubaliano ya mkataba waliokubaliana na serikali ikiwa ni pamoja na kuilipa serikali ‘’kishika uchumba’’ cha thamani ya dola milioni 300.

‘’Tunavyoongea kwa sasa tumeanza mchakato wa kuyasafirisha Makinikia na baadaye tutailipa serikali ya Tanzania dola milioni 100’’, Mkurugenzi Mark Bristow alisema.

Alimalizia kwa kusema, ‘’Kwa sasa tuko mbioni kuanza tena uzalishaji katika mgodi wa Bulyanhulu baada ya kuufunga kutokana na amri ya serikali kuzuia usafirishaji wa Makinikia’’.

Kwa mnaojua lugha ya Kiingereza mnaweza kusoma hapa:
Barrick Gold will start to ship gold worth up to $280 million from Tanzania, chief executive Mark Bristow said on Monday, after the government lifted an export ban following the resolution of a three-year tax dispute.

“The shipments will start immediately and, as we speak, we are mobilising the concentrates,” Mark Bristow told Reuters in a telephone interview.

“It’s (worth) around $260-$280 million depending on the price of metal prices at the time of sale.”

Spot gold, which rose 18% last year, is hovering at about $1,600 per ounce.

Bristow said $100 million from the proceeds of the sale of concentrates will go towards paying down a $300 million settlement agreed with the government.

As part of the deal, Tanzania will own 16% of Twiga Minerals, a new joint venture set up to manage the Bulyanhulu, North Mara and Buzwagi mines.

In the long-standing dispute, Acacia was accused of tax evasion, leading the government to impose a ban on exporting mineral concentrates and to change mining laws in 2017.

Barrick also plans in the fourth quarter of this year to re-start the Bulyanhulu mine in Tanzania, which ceased operations because of the export ban.
 
Tuliambiwa na baadhi ya ‘’wataalam wa madini’’ nchini kuwa ule ni mchanga hauna thamani kama ambavyo serikali kupitia Rais Magufuli wanadai!

Ukweli umeanza kujitokeza kupitia kwa ''wenye mchanga''!

Ninazidi kuamini kuwa uongo hutumia lift kuwafikia walengwa lakini ukweli hutumia ngazi!

Inawezekana hata haya makadirio (estimate) ya Mkurugenzi wa Barrick niya chini kwa faida yake ya kibiashara!

Ikumbukwe Kamati ya Prof Mruma ilisema kuwa kwenye zile Kontena 277 kuna dhahabu ya USD 521.3mil, Copper ya Usd 10.6mil, Silver ya Usd 1.08mil, Iridium ya Usd 105mil, Iron ya 1.2mil, Ytterbium ya Usd 7.5mil, Beryllium ya 3.8mil, Tantalum ya Usd 1.3mil, Rhodium ya Usd 0.689mil, Lithium ya Usd 0.649mil, na Sulphur ya Usd 0.844mil.

Jumla kuu ya thamani ya madini yote kwenye zile kontena 277 walipata Usd 652.663 million.

Tuendelee kuusubiri ukweli!

''Uncle Magu'' ni king'ang'anizi kweli kweli!
 
Tuliambiwa na baadhi ya ‘’wataalam wa madini’’ nchini kuwa ule ni mchanga hauna thamani kama ambavyo serikali kupitia Rais Magufuli wanadai!

Ukweli umeanza kujitokeza kupitia kwa ''wenye mchanga''!

Ninazidi kuamini kuwa uongo hutumia lift kuwafikia walengwa lakini ukweli hutumia ngazi!

Inawezekana hata haya makadirio (estimate) ya Mkurugenzi wa Barrick niya chini kwa faida yake ya kibiashara!

Tuendelee kuusubiri ukweli!

..nadhani viongozi wanadanganya.

..hakuna mtu aliyesema ule ulikuwa mchanga sawa na unaochimbwa maeneo mengine.

..kwa uelewa na kumbukumbu zangu ule ulikuwa ukiitwa mchanga wenye dhahabu. baadaye ukapata jina jipya la makinikia.

..wakati mwingine VIONGOZI wanadanganya na kupotosha kitu ambacho siyo sahihi.
 
Tuliambiwa na baadhi ya ‘’wataalam wa madini’’ nchini kuwa ule ni mchanga hauna thamani kama ambavyo serikali kupitia Rais Magufuli wanadai!

Ukweli umeanza kujitokeza kupitia kwa ''wenye mchanga''!

Ninazidi kuamini kuwa uongo hutumia lift kuwafikia walengwa lakini ukweli hutumia ngazi!

Inawezekana hata haya makadirio (estimate) ya Mkurugenzi wa Barrick niya chini kwa faida yake ya kibiashara!

Tuendelee kuusubiri ukweli!
Mkuu barrick walikua wanasafirisha dhahab iliyochenjuliwa tayar wakiichanganya na makinikia ili kukimbia kodi,ndomana ishu ilibumburuka,ila kwa maana ya makinikia kama makinikia,ni ngum sana kukuta kiasi king hvyo cha dhahab

Ulikua ni mchezo mchafu walicheza barrick
 
Tuliambiwa na baadhi ya ‘’wataalam wa madini’’ nchini kuwa ule ni mchanga hauna thamani kama ambavyo serikali kupitia Rais Magufuli wanadai!

Ukweli umeanza kujitokeza kupitia kwa ''wenye mchanga''!

Ninazidi kuamini kuwa uongo hutumia lift kuwafikia walengwa lakini ukweli hutumia ngazi!

Inawezekana hata haya makadirio (estimate) ya Mkurugenzi wa Barrick niya chini kwa faida yake ya kibiashara!

Tuendelee kuusubiri ukweli!
Wauze tunuliwe Noah Zetu. Bahati nzuri nina watoto 7, mke house gal hivyo kwangu tutapaki Noah 10.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
..nadhani viongozi wanadanganya.

..hakuna mtu aliyesema ule ulikuwa mchanga sawa na unaochimbwa maeneo mengine.

..kwa uelewa na kumbukumbu zangu ule ulikuwa ukiitwa mchanga wenye dhahabu. baadaye ukapata jina jipya la makinikia.

..wakati mwingine VIONGOZI wanadanganya na kupotosha kitu ambacho siyo sahihi.
Mkuu;
Soma vizuri na uelewe maoni yangu!

Ni wapi nimesema huo ni mchanga kama mchanga wa kawaida?

Nimesem, ''Tuliambiwa na baadhi ya ‘’wataalam wa madini’’ nchini kuwa ule ni mchanga hauna thamani kama ambavyo serikali kupitia Rais Magufuli wanadai!
 
..nadhani viongozi wanadanganya.

..hakuna mtu aliyesema ule ulikuwa mchanga sawa na unaochimbwa maeneo mengine.

..kwa uelewa na kumbukumbu zangu ule ulikuwa ukiitwa mchanga wenye dhahabu. baadaye ukapata jina jipya la makinikia.

..wakati mwingine VIONGOZI wanadanganya na kupotosha kitu ambacho siyo sahihi.

Mkuu usitulishe matango pori - kama viognozi wanadanganya - sasa Barrick walikubali uongo wa viongozi? Sasa tofauti zilitokea wapi kati ya Serikali na Barrick - kama viongozi wanadanganya??
 
..nadhani viongozi wanadanganya.

..hakuna mtu aliyesema ule ulikuwa mchanga sawa na unaochimbwa maeneo mengine.

..kwa uelewa na kumbukumbu zangu ule ulikuwa ukiitwa mchanga wenye dhahabu. baadaye ukapata jina jipya la makinikia.

..wakati mwingine VIONGOZI wanadanganya na kupotosha kitu ambacho siyo sahihi.

Mkuu usitulishe matango pori - kama viognozi wanadanganya - sasa Barrick walikubali uongo wa viongozi? Sasa tofauti zilitokea wapi kati ya Serikali na Barrick - kama viongozi wanadanganya??
 
Back
Top Bottom