Mkurugenzi Standard Chatered aleweshwa penzi la mwanafunzi

Keil

JF-Expert Member
Jul 2, 2007
2,214
802
Mkurugenzi Standard Chatered aleweshwa penzi la mwanafunzi

::Aibiwa vitu vya milioni saba hotelini
::Mwanafunzi apandishwa kizimbani


na primtiva pancras

MWANAFUNZI wa Sekondari ya Green Acres, iliyopo Magomeni, Dar es Salaam, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akituhumiwa kumwibia Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered, Mothusi Dingalo, anayesadikika kuwa mpenzi wake.

Dingalo ni Mkurugenzi wa Benki hiyo nchini Botswana. Anadaiwa kuibiwa fedha hizo katika Hoteli ya Palm Beach, Dar es Salaam.Inadaiwa kuwa mwanafunzi huyo alimpa dawa za kulevya Dingalo, ili aweze kufanikisha wizi wake.Awali ilidaiwa kuwa Dingalo, alifikia katika Hoteli ya Kilimanjaro Kempinski Dar es Salaam na baada ya kuishi hapo kwa siku chache alihamishiwa Palm Beach, ili kupisha ugeni wa Rais wa Marekani, George Bush.

Ilidaiwa kuwa Dingalo akiwa katika mapumziko katika hoteli hiyo, alitokea msichana na kujitambulisha kwake kuwa ni mwalimu, hivyo alimwomba wapumzike pamoja.

Dingalo alikubali ombi hilo na inadaiwa kuwa walilala pamoja na msichana huyo kwa siku moja.

Ilidaiwa kuwa Dingalo, alishtuka asubuhi na kukuta akiwa ameibiwa mali zake, na ndani ya chumba hicho kulionekana kichupa kidogo kinachodhaniwa kilikuwa kimetumika kuhifadhi dawa za kulevya.

Hata hivyo, ilidaiwa kuwa baada ya mshitakiwa kushtuka alikuta ameibiwa vitu mbalimbali vyote kwa pamoja vikiwa na thamani ya Sh milioni 7.

Akisoma mashitaka yanayomkabili mwanafunzi huyo, Inspekta wa Polisi, Nossoro Sisiwaya, alidai kuwa Februari 18, mwaka huu, katika maeneo ya hoteli ya Palm Beach, mshitakiwa alitenda kosa.

Sisiwaya alidai, mshitakiwa aliiba simu mbili, tiketi ya ndege ya kusafiria kutoka Dar es Salaam, Tanzania kwenda Gaborone, Botswana, funguo ya ofisi ya Posta, flash disk tatu na manukato chupa moja vyote vikiwa na thamani ya Sh milioni 7.5.

Hata hivyo, mshitakiwa alikana shitaka, Mwendesha Mashitaka alidai kuwa hana pingamizi la dhamana dhidi ya mshitakiwa huyo.

Hakimu John Msafiri wa Mahakama hiyo, alimtaka mshitakiwa kuwa na wadhamini wawili na kila mmoja na kusaini mkataba wa Sh 500,000 na Mahakama.

Mshitakiwa alitimiza masharti hayo na yupo nje hadi Machi 25, mwaka huu, kesi hiyo itakapotajwa tena.

Source: Mtanzania
 
ZINAA HURITHISHA UFAKIRI....Huyu Bwana Kuibiwa sawasawa!!! siku ingine ataacha KULALA NA WANAWAKE WASIO WAKE...Hawa wakurugenzi wanapewa Mafungu ya pesa ya kutembea na wake zao...wanawaacha kwa visingizio vya UONGO....Wengine wajirekebishe

Kingine naona waandishi wetu kanuni za Uandishi hawazijui kutaja majina ya watu
 

Kingine naona waandishi wetu kanuni za Uandishi hawazijui kutaja majina ya watu
Chanzo cha habari hiyo ni kesi Mahakamani, ambapo Mtuhumu na Mtuhumiwa utajwa kwa majina, sasa kanuni zako sijui zinasemaje hapo...!
 
Changudoa anamwibia tena mteja? Safari nyingine si hawezi kupata wateja wengine?

Tatizo la TZ ni wizi kila sehemu, watu wanafikiria leo badala ya kufikiria
biashara kwa muda mrefu.

Atakuwa amewakosesha wenzake wengi biashara.

Huku majuu hao Wakurugenzi ndio wanaongoza kuchukua malaya wanapokuwa safari. Tena siku hizi ni mashindano kwa kila mtu maana hata akina mama nao wanchukua vijana.

Dunia inakoenda ni balaa tupu. Si mmemsoma gavana wa Newyork alivyopatikana? Si ajabu watu wangemchunguza Makamba wakati ule anafukuzana na Changudoa, wangekuta na yeye anapata huduma humo humo.
 
Changudoa anamwibia tena mteja? Safari nyingine si hawezi kupata wateja wengine?

Tatizo la TZ ni wizi kila sehemu, watu wanafikiria leo badala ya kufikiria
biashara kwa muda mrefu.

Atakuwa amewakosesha wenzake wengi biashara.

Huku majuu hao Wakurugenzi ndio wanaongoza kuchukua malaya wanapokuwa safari. Tena siku hizi ni mashindano kwa kila mtu maana hata akina mama nao wanchukua vijana.

Dunia inakoenda ni balaa tupu. Si mmemsoma gavana wa Newyork alivyopatikana? Si ajabu watu wangemchunguza Makamba wakati ule anafukuzana na Changudoa, wangekuta na yeye anapata huduma humo humo.

Mtz,

Kaazi sana yaani! Hao hao wakubwa wenye pesa ndo clients za machangu!

Sasa hao wanaochukua malaya sijui wanakosa nini kwa wake zao? Au tammaa tu?

Hebu niambia huyu gavana wa NY anatoa dola 4000 kwa mwezi na zinaishia ktk kuwalipa machangu..kwani mke wake hamtoshelezi?

Mimi Mkristo ila nawaheshimu sana Waislamu kwani ukipenda unaoa kabisa na sii kuwa na nyumba ndogo kila mahali !

Machangu wako kwa vile kuna wateja! Ni mambo tu ya supply na demand!
 
Ila huyu kibopa naye ---- sana, yaani mwanamke anajileta eti naomba kulala na wewe na unakubali!! Shule haijamkomboa kabisa na afadhali aliibiwa kwani kapata degree ingine katika maisha!!
 
Jamani hv mtu na akili zko timamu wamezaje kuruhusu kulala na mtu usiemjua kwa kukufuata tu na kujitambulisha kuwa ni mtu fulani....sijaelewa hapa kwa kwel
 
Duh nilijua Bush amekuwa rais tena na amekuja Bongo, kumbe ni thread ya enzi hizo bado nikiwa naishi Sangamwalugesha
 
ilitakiwa mkurugenzi akamatwe kwa kulala na mwanafunzi.

Alivaa sare za shule?Inawezekana ni mwanafunzi lakini ni changudoa. Mwanafunzi hoteli kubwa kubwa anafuata nini kama siyo ukahaba nini? Huyo ni mwiz hana sifa ya uanafunzi.
 
Mtz,

Kaazi sana yaani! Hao hao wakubwa wenye pesa ndo clients za machangu!

Sasa hao wanaochukua malaya sijui wanakosa nini kwa wake zao? Au tammaa tu?

Hebu niambia huyu gavana wa NY anatoa dola 4000 kwa mwezi na zinaishia ktk kuwalipa machangu..kwani mke wake hamtoshelezi?

Mimi Mkristo ila nawaheshimu sana Waislamu kwani ukipenda unaoa kabisa na sii kuwa na nyumba ndogo kila mahali !

Machangu wako kwa vile kuna wateja! Ni mambo tu ya supply na demand!

Teh teh teh!

"Mimi Mkristo ila nawaheshimu sana Waislamu kwani ukipenda unaoa kabisa na sii kuwa na nyumba ndogo kila mahali !"

Swali:
1.Umejuaje kuwa mhusika ni mkristo!
2.Nani aliyekwambia wakristo wakipenda " hawaoi kabisa" na wanakuwa na "nyumba ndogo!"

Kwa ufupi tu,ww ni mkristo jina tu!
Kwa kuwa umeshuhudia baba yako "mkristo jina" kama wewe ana nyumba ndogo,bac unafikiri kila mkristo ana tabia kama ya wazazi wako!!!?

Natumaini sasa utakuwa na wake wanne,wa mwisho akiwa na umri wa miaka 9!!!
Laana ya familia inakutafuna!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom