Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya simu ya Vodacom Hisham Hendi amerejea kazini wiki hii baada ya kesi ya uhujumu uchumi iliyokuwa inamkabili kuisha

Shigganza

Senior Member
May 24, 2018
160
412
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya simu ya Vodacom Hisham Hendi amerejea kazini wiki hii baada ya kesi ya uhujumu uchumi iliyokuwa inamkabili kuisha kwa kukiri kosa na kukubali kulipa. Ikumbukwe kwamba wakati Hisham hakuwepo kazini bodi ya kampuni hiyo ilimteua Jacque Marais kukaimu nafasi hiyo

Hendi na maofisa wengine 8 wa vodacom waliachiwa Aprili 18 mwaka huu na Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu baada ya kampuni hiyo kulipa fidia ya sh. bilioni 6 ilizokuwa imeshitakiwa katika kosa la uhujumu uchumi, Malipo hayo yalikuwa ni matokeo ya majadiliano kati ya Vodacom na ofisi ya Mwendesha mashitaka(DPP)
 
CEO ajitathimini utendaji wake,wanyonge wanaibiwa pesa kwenye account zao za M-pesa kupitia watumishi wa vodacom wasiowaaminifu.
 
Ndugu Kyaruzi huo msemo uliotumia ni MANZI GA NYANZA kama aliyowahikusema Baba wa Taifa kuwa Mtoa rushwa na mpokea rushwa wote ni manzi ga nyanza! Wote watatiwa msukosuko
 
ruge aliyempa jeuri mama wa bk mpaka akaita visent vya kununua mboga yaani bilioni yeye ananunu amboga tu mzee wa heineken
🤣 🤣
Mkuuu msaidie tu jamani umweleze kuwa ni mzee wa Eskroooooo
 
Back
Top Bottom