Mkurugenzi Mtendaji TANESCO aelezea hali ya maji Mtera na Kidatu

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,293
24,173
February 10, 2020




Bwawa la Mtera lenye uwezo wa kufua umeme megawatts 80 linazidi kujaa maji na hivyo TANESCO huenda wakalazimika kufungulia maji, hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco. Maji yakitoka hapo pia huenda kituo cha Kidatu na kufua umeme mwingine wa Megawatts 204. Hii inatokana na mvua zinazoendelea kunyesha kwa miezi miwili iliyopita nchini.

Kufuatia hatua hiyo wananchi wa mikoa ya Dodoma, Morogoro na Bonde la Ruaha /Rufiji wametakiwa kuchukua tahadhari maana mkondo wa maji ktk mito ya maji kama Mtera itazidi kujaa katika maeneo yao iwapo bwawa la Mtera litazidi kujaa maji kufikia ukomo wake na kulazimika kufungulia maji.

Maeneo yatakayopata ongezoko la mtiririko wa maji ktk mito na vijito ni wilaya za Mpwapwa, Kilolo, Kilombero, Kilosa na Bonde la Mto Rufiji.

Hivyo wananchi wanaoishi maeneo hayo waendelee kufuatilia taarifa juu ya hali ya Bwawa la Mtera zitakazokuwa zinatolewa na Tanesco kila mara. Mara ya mwisho kufungulia bwawa la Mtera ili kutiririsha maji ya ziada kulifanyika mwaka 2008 hivyo TANESCO ina uzoefu wa kufanya zoezi hili kwa usalama bila kuleta madhara kwa watu waoishi katika mkondo wa maji. Taasisi zingine zote zimetaarifiwa kuhusu tahadhari hiyo. Mwisho wa kumnukuu Mkurugezi Mtendaji wa Tanesco Dr. Tito Mwinuka.

Source: TANESCO Yetu
 
February 10, 2020




Bwawa la Mtera lenye uwezo wa kufua umeme megawatts 80 linazidi kujaa maji na hivyo TANESCO huenda wakalazimika kufungulia maji, hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco. Maji yakitoka hapo pia huenda kituo cha Kidatu na kufua umeme mwingine wa Megawatts 204. Hii inatokana na mvua zinazoendelea kunyesha kwa miezi miwili iliyopita nchini.

Kufuatia hatua hiyo wananchi wa mikoa ya Dodoma, Morogoro na Bonde la Ruaha /Rufiji wametakiwa kuchukua tahadhari maana mkondo wa maji ktk mito ya maji kama Mtera itazidi kujaa katika maeneo yao iwapo bwawa la Mtera litazidi kujaa maji kufikia ukomo wake na kulazimika kufungulia maji.

Maeneo yatakayopata ongezoko la mtiririko wa maji ktk mito na vijito ni wilaya za Mpwapwa, Kilolo, Kilombero, Kilosa na Bonde la Mto Rufiji.

Hivyo wananchi wanaoishi maeneo hayo waendelee kufuatilia taarifa juu ya hali ya Bwawa la Mtera zitakazokuwa zinatolewa na Tanesco kila mara. Mara ya mwisho kufungulia bwawa la Mtera ili kutiririsha maji ya ziada kulifanyika mwaka 2008 hivyo TANESCO ina uzoefu wa kufanya zoezi hili kwa usalama bila kuleta madhara kwa watu waoishi katika mkondo wa maji. Taasisi zingine zote zimetaarifiwa kuhusu tahadhari hiyo. Mwisho wa kumnukuu Mkurugezi Mtendaji wa Tanesco Dr. Tito Mwinuka.

Source: TANESCO Yetu

Awamu ya 5 imekomesha mambo ingekuwa zamani yangefunguliwa bila taarifa
 
Wafungue mdogo mdogo maji yaendelee kupungua taratibu,kupunguza adha kwa waliokaribu na mto
Sio kwamba wamefunga. Tatizo ni balance kati ya yanayoingia na yanayotoka. Kwa sasa yanayoingia ni mengi kuliko yanayotoka, na wasiwasi unakuwa kama itatokea kukawa na flux kubwa ya maji kuingia kwa wingi kwa kiindi kifupi ukiwa na kiwango kilichopo cha bwawa kujaa. Hivyo lazima uwe na allowance ya huo uwezekano kutokea na kufungulia maji kwa tahadhari.
 
January 13, 2020

Vyanzo vya maji toka mikoa 11 vinatakiwa kulindwa ili kujaza mito inayoelekea bonde la Rufiji ktk mto Rufiji hususa mradi wa bwawa jipya litakalozalisha 2115 MW linahitaji Mita za ujazo 33 bilioni zinahitajika kujaza bwawa la JNHPP / TANESCO Dam. Bwawa hili jipya la umeme linatarajiwa kukamilika mwezi Julai mwaka 2022 kufuatana na kauli ya serikali ya Tanzania



Source: Mtanzania digital
 
Zile zama za Kufungulia Maji ili mashine zishindwe kufua Umeme zimepitwa na wakati daaaah. Najua hapo Kuna Mainjinia wamepiga sana pesa ya Mzee Rugemalila wa IPTL na Richmond ili kuleta mgao wa Umeme na sasa Wanaisoma namba.

Mungu anawaona nyie mtaishia peponi Mlifanya kila mwenye biashara anunue Jenerretta kwa Tamaaa zenu. Malipo ni hapa hapa
 
Nimepita mtera juzi, maji hayaendi upande mwingine.
Sio kwamba wamefunga. Tatizo ni balance kati ya yanayoingia na yanayotoka. Kwa sasa yanayoingia ni mengi kuliko yanayotoka, na wasiwasi unakuwa kama itatokea kukawa na flux kubwa ya maji kuingia kwa wingi kwa kiindi kifupi ukiwa na kiwango kilichopo cha bwawa kujaa. Hivyo lazima uwe na allowance ya huo uwezekano kutokea na kufungulia maji kwa tahadhari.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu maji yasipoenda upande mwingine basi hakutakuwa na maji yanaingia bwawa la Kidatu na wala hakutakuwa na umeme unazalishwa Mtera. Ili uzalishe umeme lazima maji yapite kwenda upande wa pili maana hili sio bwawa la kufugia samaki.
Mkuu Maji yanayozarisha umeme kwa kuzungusha Turbines Yanapita Chini kwa chini kwenda kwenye power House ambayo ipo mbali sana kwenda chini na hapo unapoona bwawa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Kalemani anasema umeme uunganishwe gridi ya Taifa shemu mbili, Chalinze na Kibiti. Sasa wahandisi wa umeme mkubwa nauliza; hivi kuunganisha kwenye gridi ya Taifa lazima ufanye sehemu mbili? Kwa nini upeleke kuunganisha gridi ya Taifa Chalinze na Kibiti? Kwani gridi inayounganishwa Chalinze na ile ya Kibiti haziko kwenye grid moja ya taifa?

Nahofia isije kuwa ni suala la wanasiasa kuingilia uhandisi. Kuna mwanasiasa mmoja kingunge akiwa airport Dar aliuliza kwa nini abiria kutoka Mbeya wakifikia JK Nyerere kwa ndege hawa-scan mizigo yao lakini wale wa kutoka Dubai wana-scan? Akaamrisha scan zifungwe upande wa abiria wanaowasili na domestic flights ili kuona abiria wana import nini kutoka mikoani ili walipe kodi! Vyuma vimebana hadi serikali!
 
Mkuu Maji yanayozarisha umeme kwa kuzungusha Turbines Yanapita Chini kwa chini kwenda kwenye power House ambayo ipo mbali sana kwenda chini na hapo unapoona bwawa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hili ni jibu ulipaswa kumpa Mkuu aliyesema alipita Mtera hakuona maji yakitokea upande wa pili sio mimi!

Nimepita mtera juzi, maji hayaendi upande mwingine.

Kwani hayo maji yakishazungusha turbines kwenye power house yanaenda wapi? Yanaisha kama vile gensets zinavyokula mafuta?
 
Wakulima wazidishe juhudi kulima mpunga unaohitaji maji mengi sana mashambani.., halafu sipati picha Zitto angekuwepo kipindi wanajenga hayo mabwawa ya Mtera na Kidatu, mababu zetu wangepata tabu sana la hilo Zitto Kabwela.., pia tunawashukuru mababu zetu kwa kutuachia urithi wa mabwawa, maana sisi tunaelekea kurithisha madeni kwa wajukuu..
 
Back
Top Bottom