Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) ana mtihani mkubwa sana akifanikisha hili anastahili tuzo

Huyo jamaa unaesema ilitakiwa apewe tuzo,kwa nchi zinazofuata vizuri utaratibu wa sheria ilitakiwa awe jera kwa kuharibu mfumo mzima wa kibiashara nchini. Mfumo huu wa kuwabambikia kodi kubwa,kuwafungia na kuwavuruga kwa ujumla wafanyabiashara ungeendelea ndani ya miaka mi5 tena mbele,serikali ingekosa kabisa sehemu ya kukusanya mapato
 
Shida nyie wafanya biashara mna ujanja mwingi sana,huwa hampendi kulipa kodi,mnapenda mpate faida tu,ndo maana hata zile mashine za EFD zilipokuja mlilalamika sana kwa kisingizio eti zinauzwa bei ya juu,bado hamkuweza kutoa list ya EFD zaid ya kutuandikia kwenye makaratasi, asilimia kubwa ya wafanya biashara wa Tanzania janja janja ni nyingi mno na ujuaji ni mwingi mno,mnapenda mpate faida tu pasipo kutoa kodi,mkibanwa kidogo tu kelele kibao,acheni ujanja lipeni kodi,mbona sisi wafanyakazi serikalini tunalipa kodi kubwa tu tena zaid ya mfanya biashara mkubwa!

Sasa ujanja mpka tufunge biashara zetu au mpaka tufilisike.Usikoment kitu usichokijua unakuwa kama unaugua fistula ya kichwa.
 
Hujui ulisemalo, ksbb hufanyi biashara. Kwa sisi tuliopo kwenye hiyo sekta kipindi hiki imepitia kigumu sana. Elewa T.R.A hakuishia kwa wa Asia tu. Biashara za wazawa wengi tena wadogo zimefungwa. Ona kariakoo ilivyo sasa na miaka 10 nyuma. Hivi sasa unapata chumba cha biashara maeneo tu mazuri bila kutumia dalalali. Unajua maana yake?. Vyumba vingi viko tupu pale,watu wamefunga biashara. Wapo waliofirisiwa. Ndio unayataka hayo?.
Kibaya zaidi ile kariakoo ilitakiwa iwe kitivo cha biashara kwa nchi za DRC,Rwanda,Burundi,Malawi,Zambia,Mozambique. Lakini kinachofanyika sasa?. Nchi zote hizo wanafuata bidhaa zao Kampala Uganda,nchi ambayo haina bandari.
Unajua tatizo liko wapi hapo?. Bidhaa nzuri kariakoo hamna,eidha watu waliokuwa wanafuata hiyo bidhaa wamefunga biashara au wamefirisiwa. Pili bidhaa za kariakoo wenye bandari ni ghari kuliko Kampala wenye bidhaa zinazopitia bandarini kwetu.
Siku hizi ni kawaida kwa kariakoo kukosa baadhi ya bidhaa kabisa,tofauti kabisa na kipindi cha nyuma.
Walikuwa wanaingia kwenye account za watu. Hata kama una biashara yako umeamua kuhifadhi pesa bank labda kwa kidogo kidogo mpaka kufikia milioni 20,siku wakikuibukia unajua nini walikuwa wanafanya? Mosi ilikuwa lazima uingie kwenye makubariano nao,ukijifanya unajua taratibu ndio hapo unafunguliwa kesi za uhujumu uchumi. Na account inafungiwa kwanza.
Nenda pale tunduma mpaka wa Zambia na Tz. Wafanyabiashara wamehamia upande wa zambia. Unajua ipoje? Mamlaka za Zambia baada ya kunusa wafanyabiashara kunyanyasika na mamlaka za mapato Tz wakawakaribisha kufanyia biashara upande wa Zambia. Tumekimbiza wengi pale,tumekosa mapato mengi sana.
Mwisho ujue wapo walipata strock ksbb ya hawa jamaa,wapo walio maisha kabisa. Ndio unayataka hayo?
Mkuuu unaijua kkoo . Mbon majengo mapya hayajakamilika vizur n vyumba vimesha kodishwa vyote???
 
Shida nyie wafanya biashara mna ujanja mwingi sana,huwa hampendi kulipa kodi,mnapenda mpate faida tu,ndo maana hata zile mashine za EFD zilipokuja mlilalamika sana kwa kisingizio eti zinauzwa bei ya juu,bado hamkuweza kutoa list ya EFD zaid ya kutuandikia kwenye makaratasi, asilimia kubwa ya wafanya biashara wa Tanzania janja janja ni nyingi mno na ujuaji ni mwingi mno,mnapenda mpate faida tu pasipo kutoa kodi,mkibanwa kidogo tu kelele kibao,acheni ujanja lipeni kodi,mbona sisi wafanyakazi serikalini tunalipa kodi kubwa tu tena zaid ya mfanya biashara mkubwa!
Mkuu suala la zile mashine za EFD kuuza gharama ni sahihi zilikuwa bei Sana , ziliuzwa hadi 2.8m. halikuwa kisingizio kabisa Mkuu,
 
Apunguze kodi Ili akusanye zaidi.
Gari japan dola 5000 kodi Bandarini dola 6000 utapata vipi kodi nyingi sasa.
 
Shida nyie wafanya biashara mna ujanja mwingi sana,huwa hampendi kulipa kodi,mnapenda mpate faida tu,ndo maana hata zile mashine za EFD zilipokuja mlilalamika sana kwa kisingizio eti zinauzwa bei ya juu,bado hamkuweza kutoa list ya EFD zaid ya kutuandikia kwenye makaratasi, asilimia kubwa ya wafanya biashara wa Tanzania janja janja ni nyingi mno na ujuaji ni mwingi mno,mnapenda mpate faida tu pasipo kutoa kodi,mkibanwa kidogo tu kelele kibao,acheni ujanja lipeni kodi,mbona sisi wafanyakazi serikalini tunalipa kodi kubwa tu tena zaid ya mfanya biashara mkubwa!
Kwa nchi hii kiuhalisia inafundisha yenyewe ujanja watu. Mifumo haikupi uhuru wa kulipa kodi kiuhalisia. Mfano tuanze na hiyo mashine. Wakati zinaingia wakadanganya kwamba nunueni hizo mashine then mtarudishiwa kidogo kidogo kwenye kodi,lakini sina uhakika kama wapo hata mmoja alierudishiwa.
Halafu mashine zenyewe ni gharama. Laki 8. Haijalishi una mtaji wa kiasi gani. Kiuhalisia hizi mashine,ksbb wewe serikali unataka watu waingie kwenye huo mfumo,basi wagawie bure watu. Ili uwavute waingie kwa wingi,wagawie bure,andaa mazingira ya utengenezaji hizo kila mahala ziliko.
Sasa hizo mashine ukishanunua laki 8.,bado matengenezo ni juu yako. Kwa mfano wilayani kote hakuna mafundi wa hizo mashine. Ikiharibika lazima ufunge duka ukaitengeneze mkoani. Unafika kule mkoani inabidi uisubiri mpaka itengemae unakuta siku 2. Fikiria hizo gharama. Na mashine zenyewe mbovu zinaharibika haribika. Ukija upande wa risit,ukitoa risit 100% lazima ufirisike kwa mfumo wetu. “Nimechoka kuandika mkuu,nitarudi nikuambie kwa nini ufirisike”
 
Upande mmoja anatakiwa atumie akili na hekima kukusanya kukusanya kodi kwa maelekezo ya Rais.

Upande wa pili ni lengo la trilioni 2 kwa mwezi kwa maelekezo ya Makamu wa Rais.

My take:
Siku zote mfanyabiashara lengo lake ni kutengeneza faida kubwa hapa naongelea "Big potatoes" au wafanyabiashara wakubwa ambao kila kitu wakichuma Tanzania wanapeleka kwenye account zao Canada/Ulaya.

Wafanyabiashara wa jamii ya Asia ni wajanja sana na wengi wao hawana uchungu na nchi yetu maana sio RAIA hawana hata kiwanja cha 20*20 hapa kwetu. Bado kuna makampuni makubwa yanayodai kila mwaka yanaingiza hasara ila hayafungi biashara au kuacha kuchimba madini.

Bado kuna ujanja wa kubadili majina ya kampuni baada ya grace period ya kodi kuisha. Wafanya biashara ni wajanja mno. Muhindi anaingiza mzigo kutoka China anausambaza kwenye store zaidi ya tano kisha dukani anaweka kamzigo kadogo ukienda kumkadiria kodi anajikuta analipa laki 1 kwa mwezi sawa na mtumishi kwenye salary ya laki 7.

Ukiweza kutimiza malengo haya yote mawili kwa ukamilifu, kwangu mimi wewe utakuwa mkurugenzi bora Tanzania.

"KAZI IENDELEE"
wewe huelewi chochote subiri mshahara wako mwisho wa mwezi ambao unaupata bila kutoa jasho huku wanafunzi unawafundisha wanamaliza la saba bila kujua kusoma na kuandika
 
wewe huelewi chochote subiri mshahara wako mwisho wa mwezi ambao unaupata bila kutoa jasho huku wanafunzi unawafundisha wanamaliza la saba bila kujua kusoma na kuandika
Sawa mkuu
 
Apunguze kodi Ili akusanye zaidi.
Gari japan dola 5000 kodi Bandarini dola 6000 utapata vipi kodi nyingi sasa.
Dawa ni kuongeza vyanzo vipya vya kodi.
Ila habari ya kucheka na wafanyabiashara itaturudisha kule kwenye mishahara tarehe 40.
 
Kwa nchi hii kiuhalisia inafundisha yenyewe ujanja watu. Mifumo haikupi uhuru wa kulipa kodi kiuhalisia. Mfano tuanze na hiyo mashine. Wakati zinaingia wakadanganya kwamba nunueni hizo mashine then mtarudishiwa kidogo kidogo kwenye kodi,lakini sina uhakika kama wapo hata mmoja alierudishiwa.
Halafu mashine zenyewe ni gharama. Laki 8. Haijalishi una mtaji wa kiasi gani. Kiuhalisia hizi mashine,ksbb wewe serikali unataka watu waingie kwenye huo mfumo,basi wagawie bure watu. Ili uwavute waingie kwa wingi,wagawie bure,andaa mazingira ya utengenezaji hizo kila mahala ziliko.
Sasa hizo mashine ukishanunua laki 8.,bado matengenezo ni juu yako. Kwa mfano wilayani kote hakuna mafundi wa hizo mashine. Ikiharibika lazima ufunge duka ukaitengeneze mkoani. Unafika kule mkoani inabidi uisubiri mpaka itengemae unakuta siku 2. Fikiria hizo gharama. Na mashine zenyewe mbovu zinaharibika haribika. Ukija upande wa risit,ukitoa risit 100% lazima ufirisike kwa mfumo wetu. “Nimechoka kuandika mkuu,nitarudi nikuambie kwa nini ufirisike”
Nakubaliana na wewe kwenye kutoa bure mashine za EFD tena zifike hadi kwa wauzaji magenge na ikiwezekana hata frequent maintenance iwe ni jukumu la TRA.
 
Kwa nchi hii kiuhalisia inafundisha yenyewe ujanja watu. Mifumo haikupi uhuru wa kulipa kodi kiuhalisia. Mfano tuanze na hiyo mashine. Wakati zinaingia wakadanganya kwamba nunueni hizo mashine then mtarudishiwa kidogo kidogo kwenye kodi,lakini sina uhakika kama wapo hata mmoja alierudishiwa.
Halafu mashine zenyewe ni gharama. Laki 8. Haijalishi una mtaji wa kiasi gani. Kiuhalisia hizi mashine,ksbb wewe serikali unataka watu waingie kwenye huo mfumo,basi wagawie bure watu. Ili uwavute waingie kwa wingi,wagawie bure,andaa mazingira ya utengenezaji hizo kila mahala ziliko.
Sasa hizo mashine ukishanunua laki 8.,bado matengenezo ni juu yako. Kwa mfano wilayani kote hakuna mafundi wa hizo mashine. Ikiharibika lazima ufunge duka ukaitengeneze mkoani. Unafika kule mkoani inabidi uisubiri mpaka itengemae unakuta siku 2. Fikiria hizo gharama. Na mashine zenyewe mbovu zinaharibika haribika. Ukija upande wa risit,ukitoa risit 100% lazima ufirisike kwa mfumo wetu. “Nimechoka kuandika mkuu,nitarudi nikuambie kwa nini ufirisike”
Nadhani kitu kinachokosekana kwa wafanya biadhara wengi ni elimu ya kodi nina mwaka wa nne nikifanya biashara ya kusupply vitu mbali mbali kwa kuomba tenda kwenye makampuni na taasisi za serikali na binafsi ,kinachonisaidia ni elimu kubwa ya kodi niliyonayo na TRA wananifahamu myukano unakuwa mkubwa sana ujinga wowote unapoletwa kwenye kazi yangu ,sijawai kuongezewa wala kupunguziwa kodi,wala kuumizwa na kodi ,tunakwenda sawasawa .Nachotaka kujua kwanini ukitoa risiti unafirisika? Wakati kiuhalisia sio wewe unaelipa kodi Bali wateja wako?
 
Dawa ni kuongeza vyanzo vipya vya kodi.
Ila habari ya kucheka na wafanyabiashara itaturudisha kule kwenye mishahara tarehe 40.
Kodi iwe reasonable inayolipika na isiwe komozi.Chukua kidogo Ili kesho uchukue tena kuliko kukausha damu yote unapata nyingi mara moja ila kesho upati tena.Pili kodi ikiwa kubwa usababisha ukwepaji Kodi kuwa Mkubwa.
 
Lazima tuangalie wapi tulipo kosea. kuna mambo matatu. la kwanza . zamani bandalini ujanja unjanja ulikuwa Mwingi sasa wamethibiti ilikuwa wanakuletea kontena mpaka nyumbani kutoka bandalini bila lisiti.pia ukwepaji wa kodi ulikuwa mkubwa sana . ukizoea vya kunyonga vya kuchinja huviwezi. jambo la pili kodi kubwa za bandali ni tatizo kubwa wapunguze. tatu ruswa ndio adui mkubwa Bandarin na TRA. serikali impunguzie Mfanyabiashara kodi kuanzi bandarini hadi Tra.
 
Kama mfanyabiashara mjanja ndo umuonee?
Ndo umnyanyase?
Ndo imakdirie kodi inayozidi hata mtaji wake?
Ndo umuundie task force?
Ndo umwendee na bunduki kudai mapato?

We jamaa najua una ham ule ukatili wa baba yenu uendelee ili umuenzi.
Hii ni awamu ya sita. 6
Maagizo yanayofanyiwa kazi ni ya rais. Mapango hana mamlaka ya kumtumbua mteuliwa na rais.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Wawe wakweli juu ya biashara zao,pia walipe kodi kwa hiyali pasipo kusubiri task force!
 
Ni kweli bongo voluntary compliance level iko chini sana kuliko maelezo, sasa wanapotaka kuzuia level of enforcements iwe chini kabisa maana yake itaweza kupelekea hali ikawa worse ktk makusanyo.

Advanced countries level of voluntary compliance iko juu sana kiasi kwamba haihitaji enforcements efforts kubwa katika kukusanya mapato ya serikali.

Mleta mada una hoja ya msingi isipokuwa hujagusa hasa mambo ya msingi.

Hata hivyo umethubutu.
 
CAG amesoma report,, naamini umeisikia. Madudu chini ya uzalendo yaliyokuwa yanafanyika ni funga mwaka.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Kama ameweza kujenga miradi ya trillions of money,kukarabati shule na vyuo kongwe,kujenga vituo vya afya,masomo,vituo vya mabasi,hospital za wilaya,hospitali za mikoa na kanda,ukarabati wa meli,kununua ndege 11,kujenga miundo mbinu nyingi,na kulikuwa na upigaji ule basi niishie tu kusema jamaa alikuwa shujaa
 
Back
Top Bottom