Mkurugenzi mkuu bodi ya kahawa azidi kupagawa

matengo

Member
Jun 1, 2011
30
4
Taarifa zilizojitokeza ni kuwa Mkurugenzi Mkuu Bodi ya kahawa anaendelea kufukuza wafanyakazi bila ya kufuata sheria. Kuna mfanyakazi mwingine jana amemfukuza kazi kwa kutokuwa kazini huku anaumwa. Amefukuzwa kazi wakati uongozi mzima unajua kuwa ni mgonjwa na juzi juzi tu amefanyiwa upasuaji.

Katika kumfukuza huko kazi tunaambiwa hata taratibu za sheria ya kazi hazikufuatwa kwa vile hakupewa nafasi ya kujitetea, aliyekuwa Mwenyekiti wa kamati ya nidhamu wa kikao kilichomjadili ni mkuu wa Idara iliyomfungulia mashitaka na hakupewa hukumu( hearing Form) kutoa maoni yake.

Njama hizi ni za Mkurugenzi Mkuu Bw. Adolph Kumburu ambaye ameamua kuweka sheria kando kutimiza malengo yake ya kuendesha shirika la umma kidikiteta.

Watu wanajiuliza kiburi hiki anapewa na nani hadi haogopi serikali.
 
Kama kweli watanzania tunataka maendeleo ni lazima tubadilike hasa wafanyakazi wa serikali na mashirika ya umma. inawezekana ni mgonjwa kweli lakini hajafuata taratibu anazozifahamu fika lakini kamua kuziweka kando kwanini asifukuzwe? sheria zingine zinafuga wazembe. kwanini apewe nafasi ya kujitetea kama hakufuata taratibu? nenda kwenye makampuni binafsi uone wasivyo na mchezo.huko ni kazi tu.serikalini utasikia mtu anaomba ruhusa kwenda kumzika babu wa babu yake mzaa bibi!! are we serious?
 
jamani hili nalo ni tatizo kweli siku hizi, ajabu sasa unakuta hapo 'kichwa' cha ukweli ndio kinatimuliwa
 
Wewe ni Kumburu nini? Au kibaraka yake bite? Itawashinda na kuna siku mtajutia ubabe wenu.
Kama kweli watanzania tunataka maendeleo ni lazima tubadilike hasa wafanyakazi wa serikali na mashirika ya umma. inawezekana ni mgonjwa kweli lakini hajafuata taratibu anazozifahamu fika lakini kamua kuziweka kando kwanini asifukuzwe? sheria zingine zinafuga wazembe. kwanini apewe nafasi ya kujitetea kama hakufuata taratibu? nenda kwenye makampuni binafsi uone wasivyo na mchezo.huko ni kazi tu.serikalini utasikia mtu anaomba ruhusa kwenda kumzika babu wa babu yake mzaa bibi!! are we serious?
 
Back
Top Bottom