DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,138
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Kigoma imewahukumu kifungo miaka 22 jela watumishi wanne wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji akiwemo aliyekuwa Mkurugenzi wa manispaa hiyo, Athuman Msabila baada ya kupatikana na hatia ya makosa ya kughushi nyaraka na utakatishaji wa fedha.
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi wa Mkoa, Misana Majula katika kesi ya jinai namba 5546 ya mwaka 2024 iliyowakabili watumishi 11 wa serikali, wakiwemo maofisa kutoka idara ya fedha ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.
Kwa mujibu wa hukumu hiyo, Msabila pamoja na Ofisa Uchumi wa manispaa hiyo Ferdinand Filimbi, Kaimu Mweka Hazina Salum Juma na Frank Nguvumali wamehukumiwa kifungo cha miaka miwili jela kwa kosa la kughushi nyaraka.
Aidha, Msabila na Juma wamehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kwa kosa la utakatishaji fedha baada ya kutiwa hatiani kwa kuhusika kutaka kujipatia fedha isivyo halali kiasi cha Sh milioni 463.5.
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi wa Mkoa, Misana Majula katika kesi ya jinai namba 5546 ya mwaka 2024 iliyowakabili watumishi 11 wa serikali, wakiwemo maofisa kutoka idara ya fedha ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.
Kwa mujibu wa hukumu hiyo, Msabila pamoja na Ofisa Uchumi wa manispaa hiyo Ferdinand Filimbi, Kaimu Mweka Hazina Salum Juma na Frank Nguvumali wamehukumiwa kifungo cha miaka miwili jela kwa kosa la kughushi nyaraka.
Aidha, Msabila na Juma wamehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kwa kosa la utakatishaji fedha baada ya kutiwa hatiani kwa kuhusika kutaka kujipatia fedha isivyo halali kiasi cha Sh milioni 463.5.