Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya Magu, usiwatetee na kuwalinda waalimu wasiokidhi vigezo vya Ualimu Mkuu; unawavunja moyo wanaostahili nafasi hizo

Nzelajape

Member
Nov 7, 2019
12
9
Nawasalimu wanajukwaa.

Bila kupoteza muda, naleta hoja yangu kwa DED MAGU; itokanayo na hotuba yake aliyoitoa majuzi kwenye semina ya mtihani wa darasa la nne kwa waalimu wa shule za msingi.

Kati ya mengi uliyoongea, ulimzungumzia pia Mwl. Mary Maganga wa Magu S/Msingi, ukionyesha kuridhishwa na utendaji wake shuleni hapo na kusisitiza kwamba hutamwondoa licha ya kuandikwa kwenye mitandao ya kijamii.

DED; yaliyoandikwa awali kuhusu huyu mwalimu unayajua na jamii inayajua, ni kweli yalitokea na mengine yanaendelea kutokea.
Alihamishwa kutoka Nyanguge kwenda Nyambitilwa kwa sababu ya migogoro na jamii; akahamishwa kutoka Nyambitilwa kuja Magu kwa sababu ya migogoro na jamii mpaka watu wa Nyambitilwa kufikia hatua ya kumchomea ofisi.

Hapo Magu S/Msingi amelalamikiwa kwa mambo mengi kutokana na uongozi wake usiofaa, ikiwa ni pamoja na kushindwa kufanya kazi na Kamati ya Shule; kamati ambayo ipo kimuundo wa wizara, lakini Mwl. huyu ameipuuza hata kufikia hatua ya wanakamati kumsusia.

DED; wewe uliona ni sawa watoto hadi wadogo wa darasa la II kwenda kuteka maji bwawani kwa kuvuka barabara bila kuwa na mwalimu wa kuwasindikiza?

Unajua matokeo yake, kwamba watoto wawili waligongwa wakati wakivuka barabara kwenda kuchota maji.

Hilo likitokea, shuleni kuna bomba la maji lakini lilikuwa halitoi maji eti kwa sababu mita iliibiwa! Ufumbuzi ulikuwa ni kutuma watoto wakachote maji bwawani badala kuwekwa mita nyingine?

Mbona baada ya watoto kupata ajali wakienda bwawani kuchota maji mita iliwekwa? Mlikuwa mnasubiri watoto wetu waumie ndipo mchukue hatua?

Usiendelee kutunanga wana-Magu kwa sababu ya utendaji mbovu wa Mwl. Maganga kwa kusema eti hutamtoa! Usimtoe, tutamtoa!! Mbona Nyambitilwa walimtoa, unadhani sisi tunashindwa? Sisi hatuchomi mali za shule wala za yeyote, lakini tunafuata taratibu zingine, maana wewe huoni kwamba huyo mwalimu anaumiza jamii ambayo wewe ni mkurugenzi wake, msimamizi wa maendeleo yetu lakini umetupuuza na umeamua kumlinda mtumishi mwenzako at our expense!

Waraka wa elimu ulishatoka siku nyingi kuhusu waalimu wakuu kwamba wanatakiwa kuwa wenye stashahada (Diploma); waalimu walisisitizwa kujiendeleza na waalimu wengi wamefuzu na kupata stashahada, wengine mpaka shahada za elimu wanazo.

Badala ya waalimu hawa wenye sifa stahiki kuwapa madaraka ya ualimu mkuu, halmashauri yako imeendelea kuwakumbatia waalimu wakuu wenye vyeti (certificate), badala ya diploma na degree (kama waraka unavyoagiza)

Halmashauri nyingi zimeshawaondoa waalimu wakuu wasiokuwa na diploma au degree; Magu mnasubiri nini wakati hilo ni agizo na kisera?

Mnawavunja moyo waalimu waliojiendeleza na kufaulu; wapeni haki zao za ualimu mkuu.

Kila mtu anayejiendeleza kielimu anafanya hivyo ili kuboresha maisha yake, siyo abaki palepale. Hata wewe DED na maofisa wako wote hapo wilayani, mlijiendeleza kielimu ili mpande madaraja na mpate maslahi bora kazini. Kwa nini mnawabania wenzenu? It's not fair!

Inawezekana mnaogopa challenge kama mtawapa madaraka waalimu wenye sifa stahiki; maana hiyo idara ya elimu Magu DC vilaza ni wengi. Ndio maana mnawakumbatia waalimu wasiokuwa na sifa maana mnaweza kuwaendesha mtakavyo; mnawapoka posho zao, mnawalazimisha kugharamia mitihani, michezo na matumizi mengine ya shule kwa posho zao! Wananyenyekea, wanatii maagizo yenu batili kwa sababu wanajua wamekalia viti visivyokuwa vyao!

Naamini DED Magu DC utachukua hatua stahiki badala ya kutoa mipasho vikaoni; unawaumiza waliochukua hatua ya kujiendeleza, watendee haki.

Good day.
 
Nawasalimu wanajukwaa.

Bila kupoteza muda, naleta hoja yangu kwa DED MAGU; itokanayo na hotuba yake aliyoitoa majuzi kwenye semina ya mtihani wa darasa la nne kwa waalimu wa shule za msingi.

Kati ya mengi uliyoongea, ulimzungumzia pia Mwl. Mary Maganga wa Magu S/Msingi, ukionyesha kuridhishwa na utendaji wake shuleni hapo na kusisitiza kwamba hutamwondoa licha ya kuandikwa kwenye mitandao ya kijamii.

DED; yaliyoandikwa awali kuhusu huyu mwalimu unayajua na jamii inayajua, ni kweli yalitokea na mengine yanaendelea kutokea.
Alihamishwa kutoka Nyanguge kwenda Nyambitilwa kwa sababu ya migogoro na jamii; akahamishwa kutoka Nyambitilwa kuja Magu kwa sababu ya migogoro na jamii mpaka watu wa Nyambitilwa kufikia hatua ya kumchomea ofisi.

Hapo Magu S/Msingi amelalamikiwa kwa mambo mengi kutokana na uongozi wake usiofaa, ikiwa ni pamoja na kushindwa kufanya kazi na Kamati ya Shule; kamati ambayo ipo kimuundo wa wizara, lakini Mwl. huyu ameipuuza hata kufikia hatua ya wanakamati kumsusia.

DED; wewe uliona ni sawa watoto hadi wadogo wa darasa la II kwenda kuteka maji bwawani kwa kuvuka barabara bila kuwa na mwalimu wa kuwasindikiza?

Unajua matokeo yake, kwamba watoto wawili waligongwa wakati wakivuka barabara kwenda kuchota maji.

Hilo likitokea, shuleni kuna bomba la maji lakini lilikuwa halitoi maji eti kwa sababu mita iliibiwa! Ufumbuzi ulikuwa ni kutuma watoto wakachote maji bwawani badala kuwekwa mita nyingine?

Mbona baada ya watoto kupata ajali wakienda bwawani kuchota maji mita iliwekwa?
Mlikuwa mnasubiri watoto wetu waumie ndipo mchukue hatua?

Usiendelee kutunanga wana-Magu kwa sababu ya utendaji mbovu wa Mwl. Maganga kwa kusema eti hutamtoa! Usimtoe, tutamtoa!! Mbona Nyambitilwa walimtoa, unadhani sisi tunashindwa? Sisi hatuchomi mali za shule wala za yeyote, lakini tunafuata taratibu zingine, maana wewe huoni kwamba huyo mwalimu anaumiza jamii ambayo wewe ni mkurugenzi wake, msimamizi wa maendeleo yetu lakini umetupuuza na umeamua kumlinda mtumishi mwenzako at our expense!

Waraka wa elimu ulishatoka siku nyingi kuhusu waalimu wakuu kwamba wanatakiwa kuwa wenye stashahada (Diploma); waalimu walisisitizwa kujiendeleza na waalimu wengi wamefuzu na kupata stashahada, wengine mpaka shahada za elimu wanazo.

Badala ya waalimu hawa wenye sifa stahiki kuwapa madaraka ya ualimu mkuu, halmashauri yako imeendelea kuwakumbatia waalimu wakuu wenye vyeti (certificate), badala ya diploma na degree (kama waraka unavyoagiza)

Halmashauri nyingi zimeshawaondoa waalimu wakuu wasiokuwa na diploma au degree; Magu mnasubiri nini wakati hilo ni agizo na kisera?

Mnawavunja moyo waalimu waliojiendeleza na kufaulu; wapeni haki zao za ualimu mkuu.

Kila mtu anayejiendeleza kielimu anafanya hivyo ili kuboresha maisha yake, siyo abaki palepale. Hata wewe DED na maofisa wako wote hapo wilayani, mlijiendeleza kielimu ili mpande madaraja na mpate maslahi bora kazini. Kwa nini mnawabania wenzenu? It's not fair!

Inawezekana mnaogopa challenge kama mtawapa madaraka waalimu wenye sifa stahiki; maana hiyo idara ya elimu Magu DC vilaza ni wengi. Ndio maana mnawakumbatia waalimu wasiokuwa na sifa maana mnaweza kuwaendesha mtakavyo; mnawapoka posho zao, mnawalazimisha kugharamia mitihani, michezo na matumizi mengine ya shule kwa posho zao! Wananyenyekea, wanatii maagizo yenu batili kwa sababu wanajua wamekalia viti visivyokuwa vyao!

Naamini DED Magu DC utachukua hatua stahiki badala ya kutoa mipasho vikaoni; unawaumiza waliochukua hatua ya kujiendeleza, watendee haki.

Good day.
Posho za walimu wakuu zitakutoa movu sana
 
Serikali ipo kwa ajili ya wananchi na sio wananchi wapo kwa ajili ya serikali hivyo ni wajibu wake serikali kusikiliza wananchi.

Huu ni utumiaji mbaya wa madaraka na ni ujinga.
Kama ni hivi basi taifa litaendelea kutengeneza watu useless considering tuna mfumo mbovu wa elimu.
 
Tangu uwe member wa JF mwaka 2019 una post 4, zote unaishambulia MAGU upande wa Elimu Msingi. Wamekutenda nini hasa Mkuu, Umenyimwa Cheo, Umefukuzwa kwa Vyeti Feki au ni Majungu kazini.
All in all kama unampenda mtu ni vema kumweleza ukweli wako kuhusu usichopendezwa nacho kwake, lkn kitendo cha kumchora huyo Mama hapa JF, mmmmh, tumeumbwa na Mioyo tofauti lkn.
 
Kumbe Kuna sehemu walimu wakuu bado wapo wa certificate, inasikitisha Sana, maana Kuna kitu tunaita inferiority complexity ambayo Hawa walimu wakuu wanakumbana nayo, pia walimu wenye sifa kuletewa figisufigisu na Giza Giza!
 
Kumbe Kuna sehemu walimu wakuu bado wapo wa certificate, inasikitisha Sana, maana Kuna kitu tunaita inferiority complexity ambayo Hawa walimu wakuu wanakumbana nayo, pia walimu wenye sifa kuletewa figisufigisu na Giza Giza!
Ni kweli mkuu; hapo Magu S/Msingi kuna waalimu kibao waliofuzu Diploma na mmoja ana digrii. Hata kama Mkurugenzi anaogopa kuleta mwalimu mwenye diploma kutoka mbali ili kuepuka kumlipa; kwa mini asiteue miongoni mwa waalimu walioko palepale wenye sifa?
 
Mitano Tena
Nitaomba Kwa Jina Yesu Na Mohammed
Sheikh Alhad
😁😂😅😏😐😀😁😂🤣😅😄😏😏😃😁😂🤣
 
Hapana!! Lakini hiyo hainizuii kupaza sauti ili wahusika waweke mambo sawa; ni haki ya kikatiba yangu kutoa kero na maoni yangu (Right of speech), ilimradi sivunji sheria wala simsingizii mtu.
Pamoja na hayo je,unadhani hapa ndio mahali sahihi pa kutoa malalamiko yako?.
 
Hai
Tangu uwe member wa JF mwaka 2019 una post 4, zote unaishambulia MAGU upande wa Elimu Msingi. Wamekutenda nini hasa Mkuu, Umenyimwa Cheo, Umefukuzwa kwa Vyeti Feki au ni Majungu kazini.
All in all kama unampenda mtu ni vema kumweleza ukweli wako kuhusu usichopendezwa nacho kwake, lkn kitendo cha kumchora huyo Mama hapa JF, mmmmh, tumeumbwa na Mioyo tofauti lkn.
Kwanza mimi siyo mwalimu, japo hutaamini; lakini hata kama ningekuwa mwalimu.
Haijalishi nimejiunga lini JF, haijalishi nimechangia mara ngapi; muhimu ni kwamba ninachoandika ni cha kweli, na ninachangia mijadala kama wewe ulivyochangia ili wahusika wachukue hatua kama mwanajamii.
Mwl. Mary Maganga alihamishwa kutoka Nyanguge kwenda Nyambitilwa kwa mgogoro na jamii.
Alihamishwa tena kutoka Nyambitilwa kuja Magu kwa mgogoro na jamii.
Kwa uongozi wake usiofaa, amesababisha watoto wawili kugongwa wakienda kuteka maji kwenye lambo.
Ana mgogoro na Kamati ya shule, mpaka wanakamati wamemsusia, kiasi kwamba hata ujenzi wa jengo jipya amesimamia peke yake. Kamati za shule zipo kimuundo wa wizara, siyo uamuzi wa DED, DEO, AEK, WEO wala mwalimu mkuu.
Anaongoza waalimu waliomzidi kitaaluma, hiyo inamfanya asijiamini na amekuwa kupeleka mashtaka mara kwa mara ofisi ya DEO na DED.
Ndivyo alivyo mwl. Mary Maganga unayesema ninamchora kila mara kwenye post zangu.
Huwezi kumsafisha kwa kuni-shoot mimi; hiyo ni historia aliyojitengenezea mwenyewe, haiwezi kubadilika.
 
Mkuu pole sana, kwenye kada ya ualimu kuna unafiki makubwa sana ,usipokuwa makini unakuwa mtu wa majungu majungu hadi unastaafu huna hata bati moja.kwa mwalimu anayejitambua kamwe hawezi kulilia ukuu wa shule.

Nimekuwa kwenye hii kada kuwa miaka sasa lakini nilichojifunza, walimu sisi ni watu wanafiki sana,mwalimu yuko radhi kumsema vibaya mwalimu mwenzake kwa mkuu wa shule au maafsa wa elimu ili tu apate ofa ya kusimamia mitihani ya taifa na ikiwezekana ateuliwe awe mkuu wa shule au afsa elimu kata.

Usipojipendekeza kwa mkuu wa shule, kusimamia mitihani utakusikia tu,mfano mzuri ni hapa kituoni kwangu,mkuu wangu ni Mungu mtu,usipomuanza kumsalimia hana taimu na wewe atakupita kama hakuoni,mkiwa kwenye vikao kazi yake ni kutishia walimu eti atawapa barua ya onyo kwa wale wote wenye kwenda kinyume na yeye vile anaamini,huu ni upuuzi makubwa.


Nilichojifunza walimu hatuna kazi mbadala ndio maana kila siku tunajipendekeza kwa matumaini ya kupata ofa,

Pole sana walimu,ila kikubwa tujitahidi tuwe na vipato mbadala hii itasaidia kuondoa majungu na chuki zisizo tija.

Mimi huwa hainiingia akilini mwanamme mzima kuuza sura kwa mwanamme mwenzangu ili tu nipewe ofa, huu ni upuuzi walimu tushituke,tutumie mishahara yetu ili kujipatia vipato mbadala
 
Alitakiwa Amuone Nadhani Dkt Bashiru Ama Pole Pole
Ni mahali sahihi kabisa; DED ndiye kiongozi wake wa juu kabisa kimamlaka; siyo Dr. Bashiru wala Polepole; otherwise you are kidding!!
Acha mzaha bwana, uchaguzi umekwisha; sasa kazi tu. Vipi wewe?
 
Ni mahali sahihi kabisa; DED ndiye kiongozi wake wa juu kabisa kimamlaka; siyo Dr. Bashiru wala Polepole; otherwise you are kidding!!
Acha mzaha bwana, uchaguzi umekwisha; sasa kazi tu. Vipi wewe?
Naona Hata Hapa Hajakosea Lolote
 
Magu ni moja ya wilaya za hovyo Sana Tanzania hii......hovyo mno hata viongozi wake wengi ni mamburura , wilaya ya hovyo Sana hiii , rushwa , usukuma mwingi nothing new ....... Halmashaur mbovu Sana kuwahi kutokea
 
Ni mahali sahihi kabisa; DED ndiye kiongozi wake wa juu kabisa kimamlaka; siyo Dr. Bashiru wala Polepole; otherwise you are kidding!!
Acha mzaha bwana, uchaguzi umekwisha; sasa kazi tu. Vipi wewe?
Kumlalamikia DED,hapa JF unasema ni mahali sahihi??
 
Back
Top Bottom