Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Masasi amkaidi Waziri Ndalichako

mpwisa

JF-Expert Member
Mar 7, 2013
216
251
Katika kuonesha kukaidi maagizo ya waziri wa elimu Bi Joyce Ndalichako, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Masasi Bi Getrude Gimbana ameamua kuwahamisha walimu 55 kutoka shuile za sekondari kwenda shule za msingi
Ikumbukwe kuwa waziri Ndalichako amekuwa akipinga wazo hile kwa kile kinachoelezwa halitaleta ufanisi, huku mheshimiwa Rais JPM akisisitizwa kulipwa kwa stahiki zote za mtumishi kabla ya kuhama

Katika kikao alichofanya na walimu hao juzi Ijumaa, mkurugenzi huyo alieleza uamuzi wake huo, huku walimu hao wakipinga maamuzi hayo na kuelezea tatizo la rushwa, upendeleo na urafiki kutumiwa na wakuu wa shule kupendekeza majina yao. pia walimu hao wameonyesha wasiwasi kama haki nzao zitazingatiwa, ikiwemo malipo ya uhamisho hivyo kuiomba TAKUKURU ifanye uchunguzi

wakati huohuo, wanafunzi katika shule mbalimbali wamepinga uamuzi huo uliojaaa utata, huku wale wa Shule ya Masasi Girls wakiendesha mgomo hapo siku ya jumamosi kupinga kuondolewa kwa mwalimu wao tegemeo wa somo la Historia kwa kile kinachoelezwa chuki binafsi za mkuu washule

Haya sasa, hao ndio wakurugenzi wanaomuangusha mheshimiwa rais hivyo kumfanya aonekane mbaya kwa kukaidi maagizo yake na wateule wake

More to follow.....
 
Tusubiri tuone...
Sure, tusubiri tuone, lakini kuna maswali kadhaa ya kujiuliza kabla hili halijatekelezwa

1. Ni utafiti gan umewahi kufanyika na kuthibitisha kuwa walimu wa sekondari wataweza kufundisha shule za msingi kwa ufanisi?

2. Je nini itakua hatma ya walimu hao jama watashindwa kutimiza malengo yaliyokusudiwa kwa kuwalazimisha kufanya kazi ambayo hawana weledi nayo? izingatiwe kuwa walimu hawa ni kutoka sekondari ambako mtaala wake ni tofauti na shule za msingi

3. je kwa kufanya hivyo tatizo la uhaba wa walimu litaisha au kupungua, au anatafuta kiki tu? walimu 55 si wengi

4. Vipi kuhusu kuongezeka kwa mahitaji ya walimu sekondari kunakoletwa na elimu bure?? hatowahitaji tena walimu hao siku za mbele?? jee huku si kuhamisha tatizo??
 
mwalimu tulikaa ofisini tukaelewana, leo unakimbia jf kuandika. nakuhakikishia hutapata nafasi ya kusimamia na kusahihisha mitihani ya baraza wala moko hafldi nitakapofukuzwa kazi
 
Back
Top Bottom