lara 1
JF-Expert Member
- Jun 10, 2012
- 15,700
- 29,111
Wakubwa zangu pokeeni yangu shikamoo
Nanyi wenzangu vipi yenu mamboo
Wadau wenzangu hili nalo jamboo
Mkunwa na Mkunaji nani anasikia raha zaidii?
Nimelileta kwenu hili suala nipate zenu shahidiii
Mkunaji kujitumua, kufanya kazi yenu kwa bidii
Ufundi wake wote kuutumia japo apate ushindii
Mkunwa na Mkunaji nani anasikia raha zaidiii?
Mkunwaji yeye ndo haswaa anayewashwaaa
Lakini haishi mwenzie mkunaji kumnyanyasaa
Hata awashwe vipi atakomaa kuvuta masaaa
Mkunwa na Mkunaji nani ansikia raha zaidiiii?
Mkunaji hachoki kujitumaa, Kila saa kuulizia
Kama mkunwaji yupo tayari huduma kuimalizia
Wala hahitaji kujiandaa, akiitwa tu jambo kamalizia
Mkunwa na Mkunaji nani anasikia raha zaidiii?
Mkunajwi binti kiburi, kingi tena kimemjaaa
Katu hakunwi bila kulipwa pesa kadha wa Kadhaa
Au kupewa zawadi, vitu na mali kadha wa kadhaa
Mkunwa na Mkunaji nani anasikia raha zaidiii?
Mkunaji yeye mwanzo huwa hodari mvumilivu
Atakubali yote ili mradi tu apewe hizo mbivu
Akishakula hizo mbivu shurti lake aache maumivu
Mkunwa na Mkunaji nani anasikia raha zaidiii?
Mimi nahitimisha hili jalada na kesi naifunga
Wote wawili kwa pamoja hatiani nawafunga
Kama wote mwasikia raha yanini kwingi kuzuga
Mkunwa na Mkunaji nani anasikia raha zaidiii?
NAOMBA MAJIBU YENU WAKUU JUU YA HILI SWALA?
Nanyi wenzangu vipi yenu mamboo
Wadau wenzangu hili nalo jamboo
Mkunwa na Mkunaji nani anasikia raha zaidii?
Nimelileta kwenu hili suala nipate zenu shahidiii
Mkunaji kujitumua, kufanya kazi yenu kwa bidii
Ufundi wake wote kuutumia japo apate ushindii
Mkunwa na Mkunaji nani anasikia raha zaidiii?
Mkunwaji yeye ndo haswaa anayewashwaaa
Lakini haishi mwenzie mkunaji kumnyanyasaa
Hata awashwe vipi atakomaa kuvuta masaaa
Mkunwa na Mkunaji nani ansikia raha zaidiiii?
Mkunaji hachoki kujitumaa, Kila saa kuulizia
Kama mkunwaji yupo tayari huduma kuimalizia
Wala hahitaji kujiandaa, akiitwa tu jambo kamalizia
Mkunwa na Mkunaji nani anasikia raha zaidiii?
Mkunajwi binti kiburi, kingi tena kimemjaaa
Katu hakunwi bila kulipwa pesa kadha wa Kadhaa
Au kupewa zawadi, vitu na mali kadha wa kadhaa
Mkunwa na Mkunaji nani anasikia raha zaidiii?
Mkunaji yeye mwanzo huwa hodari mvumilivu
Atakubali yote ili mradi tu apewe hizo mbivu
Akishakula hizo mbivu shurti lake aache maumivu
Mkunwa na Mkunaji nani anasikia raha zaidiii?
Mimi nahitimisha hili jalada na kesi naifunga
Wote wawili kwa pamoja hatiani nawafunga
Kama wote mwasikia raha yanini kwingi kuzuga
Mkunwa na Mkunaji nani anasikia raha zaidiii?
NAOMBA MAJIBU YENU WAKUU JUU YA HILI SWALA?