Mkulo: Kilichoenda kwa wahisani si bajeti ni "makadirio"

AmaniKatoshi

Senior Member
Mar 31, 2009
158
14
Mkulo: Kilichoenda kwa wahisani si bajeti

Mwananchi, Wednesday, 08 December 2010
Raymond Kaminyoge

SIKU tatu
baada ya Kundi la nchi wahisani wa maendeleo ambalo zinachangia kwenye bajeti ya Tanzania (GBS) kuibua kashfa kuwa Serikali iliwapelekea bajeti tofauti na iliyopitishwa na Bunge, Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustapha Mkulo, ameibuka na kusema kilichokua kimepekwa kwao ni makadirio.

Alisema bajeti iliyowasilishwa kwa Shirika la Fedha Duniani (IMF) yalikuwa makadirio ambayo yalibadilishwa katika mchakato wa kuiandaa na kwamba bajeti iliyopitishwa na Bunge ndiyo inayotambulika.


Mkulo alisema hayo jana jijini Dar es Salaam mara baada ya kumalizika mkutano wa kitaifa wa mwaka wa majadiliano ya kisera na bajeti.


"Kuna mchakato mrefu wakati wa kuandaa bajeti, tuliwapa makadirio ya bajeti yetu mwezi Aprili mwaka huu, baada ya hapo bajeti ilipitia kwenye Baraza la Mawaziri ambalo lilifanya marekebisho. Katika kipindi hicho kuna marekebisho yalifanywa hivyo kutofautiana na makadirio tuliyowapelekea wahisani," alisema Mkulo na kuongeza:


"
Ndiyo maana nasema sijawahi kupeleka kwa wahisani bajeti tofauti na iliyopelekwa bungeni. Nasisitiza kuwa bajeti ni moja tu ambayo ndiyo hiyo niliyowasilisha bungeni baada ya kuidhinishwa na Baraza la Mawaziri," alisema.

Alisema ni utaratibu wa kawaida wahisani kupelekewa makadirio mapema, lakini mambo hubadilika kutokana na gharama eza kuendesha Serikali kubadilika".


"
Msidhani Mkulo ndiye anayeandaa bajeti pekee yake, Baraza la Mawaziri ndilo lenye kauli ya mwisho kuhusu bajeti ya nchi, wanaweza kubadilisha chochote wakati wahisani mlishawapelekea bajeti yenu mapema," alisema Mkulo.

Jumatatu wiki hii, Mwenyekiti wa kundi la wahisani wa maendeleo ambalo linachangia kwenye bajeti kuu ya Tanzania (GBS), Svein Baera, katika hotuba yake ambayo Mwananchi ina nakala, alisema serikali ilipeleka IMF, bajeti tofauti na iliyopitishwa na Bunge.


Taarifa hiyo ilitolewa huku wahisani hao wakiwa wamezuia theluthi moja ya zaidi ya dola za Marekani 800 milioni ambazo zinatakiwa zichangiwe na wahisani kwenye Bajeti Kuu ya 2010/11, wakiishinikiza Serikali iharakishe utekelezaji wa programu ya mageuzi, yakiwemo ya mfumo wa usimamizi wa fedha za umma.


Baera alibainisha maeneo sita kuwa ndiyo mhimili wa mjadala wao na serikali.

"Napenda kuainisha maeneo sita ya ujumbe wetu ili kuweka sawa jukwaa la majadiliano yetu haya ya mwaka. Kuna tofauti kati ya bajeti iliyowasilishwa kwa bodi ya (Shirika la Kimataifa la Fedha) IMF na ile iliyopitishwa na Bunge Julai 2010," alisema Baera.

Alisema bajeti ambayo serikali iliwasilisha kwa wahisani hao ilibeba matumaini makubwa ya kuzaa matokeo mazuri na kufanywa kama sababu ya kupitisha matumizi makubwa ya fedha zinazotokana na mapato ya ndani".


Baera alisema kukosekana kwa uwazi katika matumizi, vipaumbele, mapato na mfumo mzima wa fedha kunapunguza kuaminika kwa bajeti hiyo mbele ya wafadhili.



My take:
1. Kwa nini imemchukua Mh Mkulo siku tatu kujibu shutuma wakati jibu alikuwa nalo kwa kuwa alihusika kwenye mchakato wote?


2. Je, kwa nini Mh Mkulo anasema budget inaandaliwa na watu wengi? Ina maana anataka kusema kosa hilo sio la kwake?

3. Kwa kuwa ofisi yake inahusika moja kwa moja kwa nini anatoa majibu ya kujihami badala ya kuchukua uamuzi wa kuijuzulu?

4. Je, Mkulo anataka kutuambia kuwa bajeti sio makadirio?


Hebu tuliangalie hili wana Jf
 
Huyu waziri anafanya mambo kama conmen wa pale nje ya Bills. Hii mambo ya kupeleka bajeti mbili ni utapeli ulioukuka aache masihala.
 
Mkuu umeuliza maswali ya msingi sana. Mimi nadhani ni vyema tukiangalia maneno ya Mkulo kwa maana zaidi ya mbili.
1. Imechukua siku 3 kwa kuwa;
a. Hajui kinachoendelea hivyo wasaidizi wake walilazimika kutafuta sababu
b. Walikuwa wamechakachua na ilibidi watunge sababu.

2.Bajeti inaandaliwa na watu wengi ana maanisha;
a.hakuna coordination nzuri ya ku-reconcile data kutoka pande husika (inefficiency)
b.timu ya wachakachuaji ilihusisha watu nje ya wataalam wa wizara, hivyo mahesabu hayakwenda sawa

3. Kwa nini hajiuzulu? Kwa sababu;
a. haoni kosa ni hitlafu ndogo tu iliyotokea.
b. kosa halikusababishwa na yeye bali ile timu ya wachakachuaji walioharibu mahesabu

4. Je bajeti si makadirio?
a. nothing is set in stone, lkn bajeti ni realistic projection
b. hawezi kukubali kuwa ni makadirio kwani itazua maswli mengi.

Kama jibu ya maswali yako yote ni (a) basi Mkulo ni incompetent arrogant unreliable leader.
Kama jibu ni (b) basi Mkulo ni scapegoat na anajua hilo hivyo anatuma ujumbe kwa wahusika - he is not taking this lying down!
Nawasilisha.
 
Mkuu umeuliza maswali ya msingi sana. Mimi nadhani ni vyema tukiangalia maneno ya Mkulo kwa maana zaidi ya mbili.
1. Imechukua siku 3 kwa kuwa;
a. Hajui kinachoendelea hivyo wasaidizi wake walilazimika kutafuta sababu
b. Walikuwa wamechakachua na ilibidi watunge sababu.

2.Bajeti inaandaliwa na watu wengi ana maanisha;
a.hakuna coordination nzuri ya ku-reconcile data kutoka pande husika (inefficiency)
b.timu ya wachakachuaji ilihusisha watu nje ya wataalam wa wizara, hivyo mahesabu hayakwenda sawa

3. Kwa nini hajiuzulu? Kwa sababu;
a. haoni kosa ni hitlafu ndogo tu iliyotokea.
b. kosa halikusababishwa na yeye bali ile timu ya wachakachuaji walioharibu mahesabu

4. Je bajeti si makadirio?
a. nothing is set in stone, lkn bajeti ni realistic projection
b. hawezi kukubali kuwa ni makadirio kwani itazua maswli mengi.

Kama jibu ya maswali yako yote ni (a) basi Mkulo ni incompetent arrogant unreliable leader.
Kama jibu ni (b) basi Mkulo ni scapegoat na anajua hilo hivyo anatuma ujumbe kwa wahusika - he is not taking this lying down!
Nawasilisha.
Mkuu nakupongeza kwa namna ulivyoweza kujengea hoja maswali ya AmaniKatoshi
Zaidi ya hayo maswali na mfano wa majibu. Pia tutafakari kile ambacho Mkulo hakukisema ni kuwa hayo makadirio yalikuwa replaced baada ya bajeti kupitishwa?? I mean lini walipeleka bajeti kamili IMF? Sidhani wahisani walikurupuka na kudai bajeti ina kasoro. Je ina maana kama IMF wangetoa fungu ambalo limetokana na makadirio hayo hiyo ziada ingerejeshwa au ndo ingekuwa kwenye menu list ya mafisadi??
 
Mkuu Susuviri na wengine, nimefurahishwa sana na majibu yako. Nilipata majibu yanayoendana na ya kwako baada ya kuuliza maswali yangu, lakini nimependelea zaidi yametoka kwako na kuonyesha jinsi "tatizo la usiri wa madudu, uchakachuaji na iniefficiency and lack of accountability" yanavyoitafuna nchi yetu na kodi zetu wavuja jasho.

Kuongezea na swali la mchangiaji wa mwisho najiuliza "kwa nini Mkulo alitata mtoa shutuma aende kwa ofisi yake ili wakazungumze?" na je si ukweli majibu yake ametimiza wajibu kutumia media baada ya kugundua ilikuwa kosa kutaka kujibu shutuma tena ya mtu anayeshikilia hela za bajeti kwa kumnongoneza...na akijua kuwa hanong`onezeki?

Sasa ninaendelea kupata picha kamili kwa nini wale wazee kule Kilosa walisema hafai....
 
Huyu msanii Mkulo aache kutudanganya.kwani alishindwa nini kuwapa hao wahisan bajeti iliyopitishwa ili wajue hali halisi?ni nini anaficha hapa?kweli hafai japo ni swahiba wa JK na wizara ni nzito/delicate kuliko uwezo wake but kwasababu ya kubebana ,ushikaji na upambe kapewa.
iam so bored with minister and his president.
 
Mkulo: Kilichoenda kwa wahisani si bajeti

Mwananchi, Wednesday, 08 December 2010
Raymond Kaminyoge

SIKU tatu
baada ya Kundi la nchi wahisani wa maendeleo ambalo zinachangia kwenye bajeti ya Tanzania (GBS) kuibua kashfa kuwa Serikali iliwapelekea bajeti tofauti na iliyopitishwa na Bunge, Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustapha Mkulo, ameibuka na kusema kilichokua kimepekwa kwao ni makadirio.

Alisema bajeti iliyowasilishwa kwa Shirika la Fedha Duniani (IMF) yalikuwa makadirio ambayo yalibadilishwa katika mchakato wa kuiandaa na kwamba bajeti iliyopitishwa na Bunge ndiyo inayotambulika.


Mkulo alisema hayo jana jijini Dar es Salaam mara baada ya kumalizika mkutano wa kitaifa wa mwaka wa majadiliano ya kisera na bajeti.


"Kuna mchakato mrefu wakati wa kuandaa bajeti, tuliwapa makadirio ya bajeti yetu mwezi Aprili mwaka huu, baada ya hapo bajeti ilipitia kwenye Baraza la Mawaziri ambalo lilifanya marekebisho. Katika kipindi hicho kuna marekebisho yalifanywa hivyo kutofautiana na makadirio tuliyowapelekea wahisani," alisema Mkulo na kuongeza:


"
Ndiyo maana nasema sijawahi kupeleka kwa wahisani bajeti tofauti na iliyopelekwa bungeni. Nasisitiza kuwa bajeti ni moja tu ambayo ndiyo hiyo niliyowasilisha bungeni baada ya kuidhinishwa na Baraza la Mawaziri," alisema.

Alisema ni utaratibu wa kawaida wahisani kupelekewa makadirio mapema, lakini mambo hubadilika kutokana na gharama eza kuendesha Serikali kubadilika".


"
Msidhani Mkulo ndiye anayeandaa bajeti pekee yake, Baraza la Mawaziri ndilo lenye kauli ya mwisho kuhusu bajeti ya nchi, wanaweza kubadilisha chochote wakati wahisani mlishawapelekea bajeti yenu mapema," alisema Mkulo.

Jumatatu wiki hii, Mwenyekiti wa kundi la wahisani wa maendeleo ambalo linachangia kwenye bajeti kuu ya Tanzania (GBS), Svein Baera, katika hotuba yake ambayo Mwananchi ina nakala, alisema serikali ilipeleka IMF, bajeti tofauti na iliyopitishwa na Bunge.


Taarifa hiyo ilitolewa huku wahisani hao wakiwa wamezuia theluthi moja ya zaidi ya dola za Marekani 800 milioni ambazo zinatakiwa zichangiwe na wahisani kwenye Bajeti Kuu ya 2010/11, wakiishinikiza Serikali iharakishe utekelezaji wa programu ya mageuzi, yakiwemo ya mfumo wa usimamizi wa fedha za umma.


Baera alibainisha maeneo sita kuwa ndiyo mhimili wa mjadala wao na serikali.

"Napenda kuainisha maeneo sita ya ujumbe wetu ili kuweka sawa jukwaa la majadiliano yetu haya ya mwaka. Kuna tofauti kati ya bajeti iliyowasilishwa kwa bodi ya (Shirika la Kimataifa la Fedha) IMF na ile iliyopitishwa na Bunge Julai 2010," alisema Baera.

Alisema bajeti ambayo serikali iliwasilisha kwa wahisani hao ilibeba matumaini makubwa ya kuzaa matokeo mazuri na kufanywa kama sababu ya kupitisha matumizi makubwa ya fedha zinazotokana na mapato ya ndani".


Baera alisema kukosekana kwa uwazi katika matumizi, vipaumbele, mapato na mfumo mzima wa fedha kunapunguza kuaminika kwa bajeti hiyo mbele ya wafadhili.



My take:
1. Kwa nini imemchukua Mh Mkulo siku tatu kujibu shutuma wakati jibu alikuwa nalo kwa kuwa alihusika kwenye mchakato wote?


2. Je, kwa nini Mh Mkulo anasema budget inaandaliwa na watu wengi? Ina maana anataka kusema kosa hilo sio la kwake?

3. Kwa kuwa ofisi yake inahusika moja kwa moja kwa nini anatoa majibu ya kujihami badala ya kuchukua uamuzi wa kuijuzulu?

4. Je, Mkulo anataka kutuambia kuwa bajeti sio makadirio?


Hebu tuliangalie hili wana Jf

Ama kwa hakika hii inaonesha wazi kwamba sasa wahisani wameanza kushtukia mipango ya kisanii inayoendeshwa na serikali ya CCM na JK wao hivyo wameanza kufuatilia kila kitu kinachofanywa na serikali hasa katika mipango iliyo katika maandishi. Hata wao pia wanakumbuka jinsi sheria ya gharama za uchaguzi ilivyochakachuliwa mara baada ya kupitishwa bungeni na rais kupewa nyingine iliyoongezwa vipengele ambavyo havikujadiliwa na bunge. Kwa kuzingatia hilo la umaarufu wa kuchakachua kila kitu ilibidi wahisani wachukue muda kuangalia uwezekano wa bajeti kuchakachuliwa na hilo wameliona, sasa hapa Mkullo anakuja na maneno mepesi ya kupoza eti alipeleka makadirio kwa wahisani. Sasa ina maana hayo makadirio yametofautiana sana na hiyo bajeti halisi iliyojadiliwa na kupitishwa na bunge? Na kama ni makadirio ni lazima hiyo copy isomeke kuwa ni makadirio ya bajeti ya serikali ya JMT kwa mwaka wa fedha 2010/2011 hapa hata hao wahisani wasingesema kwamba wamepewa bajeti tofauti na iliyopitishwa na Bunge.
Nashawishika kuamini kwamba hawa wasanii huwa wanaandaa bajeti mbili, moja inazidi ili kupata ulaji wao na ya pili ni ya kutudanganya sisi wadanganyika kuona kwamba ndio bajeti halisi iliyojadiliwa na kupitishwa na bunge letu.
Kwa mtazamo huu namshauri Mkullo aachie ngazi kwa sababu ameliaibisha taifa.
 
1. Imechukua siku 3 kwa kuwa;
a. Hajui kinachoendelea hivyo wasaidizi wake walilazimika kutafuta sababu

Kwa nnavyoifahamu Tanzania hii hasa ndiyo sababu kuu. Yaani hawa mawaziri walio wengi ni kupiga siasa tu, hawajui hata kinachoendelea. And guess wht in just this one month napata picha awamu hii ya Kikwete na serikali yake itakuwa kwenye defensive mode mpaka 2015. Hawajajiandaa kufanya lolote. I just can't believe eti JK yule yule tunayemjua will do, act or plan anaything different. Wao kazi yao kubwa ni kushinda uchaguzi tu!!!
 
Kwa nnavyoifahamu Tanzania hii hasa ndiyo sababu kuu. Yaani hawa mawaziri walio wengi ni kupiga siasa tu, hawajui hata kinachoendelea. And guess wht in just this one month napata picha awamu hii ya Kikwete na serikali yake itakuwa kwenye defensive mode mpaka 2015. Hawajajiandaa kufanya lolote. I just can't believe eti JK yule yule tunayemjua will do, act or plan anaything different. Wao kazi yao kubwa ni kushinda uchaguzi tu!!!

Kweli kabisa, kila mara JK anazungumzia juu ya kwa nini CCM imeshindwa katika majimbo kadhaa na eti ufanyike utafiti kujua hilo! Wanachofikiria hawa jamaa ni kubaki madarakani tuu na kufanya ufisadi!
 
Wakuu, naomba tuendelee kuangalia maswali mengine maana naamini tunaweza tukaendelea kupata picha kamili cha kilichojiri mpaka tumepata aibu hii kama taifa
Naomba kwanza tumalize kuangalia maneno ya Mkulo, alitaka mtoa shutuma aende ofsini kwake kwa sababu;
a) aligundua wasaidizi wake walichemka na alitaka ‘kusave face' yaani kuepusha kuaibika zaidi
b) alifikiri anaweza kuwalisha maneno wahisani watulie na uchakachuaji uendelee

Kuhusu makadirio yaliyotolewa IMF kama yalikuwa ‘replaced' hatuwezi kujua kama ni kweli au la, ila wamepata aibu ya kutosha.

Mi binafsi nadhani ukweli ni c) yaani - both above a) and b) is true. Ni uzembe ukichanganya na uchakachuaji. :eek:
 
Kweli kabisa, kila mara JK anazungumzia juu ya kwa nini CCM imeshindwa katika majimbo kadhaa na eti ufanyike utafiti kujua hilo! Wanachofikiria hawa jamaa ni kubaki madarakani tuu na kufanya ufisadi!

Ni kweli kabisa kuwa hawa jamaa akili yao yote ni jinsi ya kubaki madarakani na sio jinsi ya kuboresha maisha ya wananchi; na ndiyo maana awamu hii ya lala salama ya Kiwete hatafanya kitu cha maana kwa nchi hii isipokuwa kutuibia maliasili zetu yeye akishirikiana na wakina Subash wake!! Mungu mkubwa anawaona na hukumu yao wataipata hapa hapa duniani; kwani wameishaanza kuadhibiwa kwa kulazimika kunywa maji na dawa hadharani hata kwenye gwaride!!
 
bdo shida ya kuwa na mawaziri wenye kuwa na upeo mdogo na wasio na vision..sasa haya ndo matunda yake
 
Kwahiyo kilichoenda ni makadirio wengepewa...... hiyo difference ingekwenda wapi? na nani angekuwa amepitisha matumizi yake? (I thought hii ni kazi ya Bunge?)
 
Wahisani nawashukuru kwa kuwa makini na serikali ya ccm kwani hawa ni ccm ni mabingwa wa kuchakachuwa.
 
Mkulo: Kilichoenda kwa wahisani si bajeti

Mwananchi, Wednesday, 08 December 2010
Raymond Kaminyoge

SIKU tatu
baada ya Kundi la nchi wahisani wa maendeleo ambalo zinachangia kwenye bajeti ya Tanzania (GBS) kuibua kashfa kuwa Serikali iliwapelekea bajeti tofauti na iliyopitishwa na Bunge, Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustapha Mkulo, ameibuka na kusema kilichokua kimepekwa kwao ni makadirio.

Alisema bajeti iliyowasilishwa kwa Shirika la Fedha Duniani (IMF) yalikuwa makadirio ambayo yalibadilishwa katika mchakato wa kuiandaa na kwamba bajeti iliyopitishwa na Bunge ndiyo inayotambulika.


Mkulo alisema hayo jana jijini Dar es Salaam mara baada ya kumalizika mkutano wa kitaifa wa mwaka wa majadiliano ya kisera na bajeti.


"Kuna mchakato mrefu wakati wa kuandaa bajeti, tuliwapa makadirio ya bajeti yetu mwezi Aprili mwaka huu, baada ya hapo bajeti ilipitia kwenye Baraza la Mawaziri ambalo lilifanya marekebisho. Katika kipindi hicho kuna marekebisho yalifanywa hivyo kutofautiana na makadirio tuliyowapelekea wahisani," alisema Mkulo na kuongeza:


"
Ndiyo maana nasema sijawahi kupeleka kwa wahisani bajeti tofauti na iliyopelekwa bungeni. Nasisitiza kuwa bajeti ni moja tu ambayo ndiyo hiyo niliyowasilisha bungeni baada ya kuidhinishwa na Baraza la Mawaziri," alisema.

Alisema ni utaratibu wa kawaida wahisani kupelekewa makadirio mapema, lakini mambo hubadilika kutokana na gharama eza kuendesha Serikali kubadilika".


"
Msidhani Mkulo ndiye anayeandaa bajeti pekee yake, Baraza la Mawaziri ndilo lenye kauli ya mwisho kuhusu bajeti ya nchi, wanaweza kubadilisha chochote wakati wahisani mlishawapelekea bajeti yenu mapema," alisema Mkulo.

Jumatatu wiki hii, Mwenyekiti wa kundi la wahisani wa maendeleo ambalo linachangia kwenye bajeti kuu ya Tanzania (GBS), Svein Baera, katika hotuba yake ambayo Mwananchi ina nakala, alisema serikali ilipeleka IMF, bajeti tofauti na iliyopitishwa na Bunge.


Taarifa hiyo ilitolewa huku wahisani hao wakiwa wamezuia theluthi moja ya zaidi ya dola za Marekani 800 milioni ambazo zinatakiwa zichangiwe na wahisani kwenye Bajeti Kuu ya 2010/11, wakiishinikiza Serikali iharakishe utekelezaji wa programu ya mageuzi, yakiwemo ya mfumo wa usimamizi wa fedha za umma.


Baera alibainisha maeneo sita kuwa ndiyo mhimili wa mjadala wao na serikali.

"Napenda kuainisha maeneo sita ya ujumbe wetu ili kuweka sawa jukwaa la majadiliano yetu haya ya mwaka. Kuna tofauti kati ya bajeti iliyowasilishwa kwa bodi ya (Shirika la Kimataifa la Fedha) IMF na ile iliyopitishwa na Bunge Julai 2010," alisema Baera.

Alisema bajeti ambayo serikali iliwasilisha kwa wahisani hao ilibeba matumaini makubwa ya kuzaa matokeo mazuri na kufanywa kama sababu ya kupitisha matumizi makubwa ya fedha zinazotokana na mapato ya ndani".


Baera alisema kukosekana kwa uwazi katika matumizi, vipaumbele, mapato na mfumo mzima wa fedha kunapunguza kuaminika kwa bajeti hiyo mbele ya wafadhili.



My take:
1. Kwa nini imemchukua Mh Mkulo siku tatu kujibu shutuma wakati jibu alikuwa nalo kwa kuwa alihusika kwenye mchakato wote?


2. Je, kwa nini Mh Mkulo anasema budget inaandaliwa na watu wengi? Ina maana anataka kusema kosa hilo sio la kwake?

3. Kwa kuwa ofisi yake inahusika moja kwa moja kwa nini anatoa majibu ya kujihami badala ya kuchukua uamuzi wa kuijuzulu?

4. Je, Mkulo anataka kutuambia kuwa bajeti sio makadirio?


Hebu tuliangalie hili wana Jf

Mwe sa zengine nataka kucheka vituko vya mawaziri wetu hebu bwana mkulo mzee wa masters ya international business tupe tofauti kati ya Budget na makadirio?
 
Bajeti inayotakiwa kwenda kwa nchi wahisani ni ile iliyopitishwa na bunge au rasimu(draft)yake?Kama ni rasimu basi lazima wanapelekewa tena inayopitishwa bungeni kwakuwa hata wao hujua kuwa hiyo ni rasimu ya bajeti.Kwa nini sasa hawakupelekewa?Jibu ni moja.Draft waliyokuwa nayo ilikuwa inawanufaisha viongozi kwa namna moja au nyingine.Kama iliyopitishwa na bunge ingeongeza maslahi zaidi kwa viongozi zaidi ya draft waliyonayo wahisani,je wahisani wasingepelekewa bajeti hiyo haraka mara baada ya kupitishwa na bunge?Na je hili limetokea bajeti hii tu au na zilizopita?Watanzania tunaliwa na kuibiwa na hawa wezi wa kalamu.
 
Nadhni mimi kma mtanzania,siko proud 2 be tanzanian..wait just wait sababu kubwa yakufeel ths way,nipale vngozi wetu include our prezd wanapokua wanatalk na public wanajua sis nimaignorante..its make me sick.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom