Mkulo awadanganya watanzania na bunge kuhusu bajeti ya 2011/2012.

MAGAMBA MATATU

JF-Expert Member
Jul 2, 2011
646
1,174
Saturday, 02 July 2011 09:49
0diggsdigg


mafuta%20bango.jpg



Waandishi Wetu
WAFANYABIASHARA wa mafuta ya petroli, dizeli na taa, ni kama wamegomea mpango wa serikali wa kushusha bei kupita bajeti ya serikali iliyotangazwa na waziri wa fedha ndugu MKULO, kufuatia kufutwa na kupunguzwa kwa viwango vya baadhi ya kodi zilizokuwa vikitozwa kweye bidhaa hizo.

Lengo la serikali lilikuwa ni kupunguza ukali wa maisha kwa wananchi unaotokana na mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali unaochangiwa na gharama kubwa za uzalishaji na usafirishaji. Serikali pia kupitia bajeti yake iliyopitishwa na bunge hivi karibuni ilipendekeza kuongeza kiwango cha kodi kwenye mafuta ya taa ili kukabiliana na vitendo vya uchakachuaji wa mafuta vinavyofanywa na wafanyabiashara wasio waaminifu.

Kulingana na mkakati wa serikali uliotangazwa na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), Haruna Masebu, Watanzania wangeanza kufaidika na mpango huo wa serikali kuanzia jana LAKINI HALI IMEKUWA TOFAUTI KABISA,.

Jana, Julai 1, ndiyo ilikuwa siku ya kuanza kutekelezwa kwa bajeti mpya ya 2011/12 ya ndgu MKULO .Lakini uchunguzi wa Mwanachi umebaini kwamba bei za petroli na dizeli ziliendelea kuwa juu lakini lita moja ya mafuta ya taa ilipaa kwa ongezeko la Sh 500 zaidi.

Kulingana na mkakati wa serikali bei ya mafuta ya taa ingeongezeka kwa wastani wa sh 400 kwa lita.
Kabla ya jana Jijini Dar es Salaam dizeli na petroli ilikuwa inauzwa kwa wastani wa Sh 2,070 kwa lita wakati mafuta ya taa yalikuwa yanauzwa kwa wastani wa Sh 1,550 kwa lita.

Katika uchunguzi wa Mwananchi kwenye vituo mbalimbali vya mafuta Jijini Dar es Salaam, hali ilikuwa ni ya kusikitisha na ya kukatisha tamaa kiasi kwamba baadhi ya watu walisikika wakisema; "hii ni serikali ya rushwa, hata mambo yake yanaenda kwa rushwa huku ikihubiri maneno matamu kwenye majukwaa ya kisiasa."

Bei za mafuta
Mabango kwenye vituo mbalimbali yalionyesha mauzo kwa kiwango cha lita kama ifuatavyo: Katika kituo cha Oil Com Temeke petroli ilikuwa inauzwa kwa Sh 2,090, dizeli Sh2,080 wakati bei ya mafuta ya taa Ilikuwa ni Sh2,086.
Katika kituo cha FAB kilichopo Temeke Sudani mafuta aina ya petroli yaliuzwa kwa Sh2,050, dizeli Sh2,050 wakati kituo kingine kilichopo Temeke Sudani cha Big Born petroli ilikuwa ikiuzwa Sh2,070 dizeli Sh2,070 na mafuta ya taa 2086.

1. JE MKULO KWA HILI SUALA LA KUTOA BAJETI AMBAYO INAPINGANA NA UKWELI HALISI WA MAFUTA SI AMELIDANGAYA BUNGE NA WANANCHI KWA UJULA.

1. JE SERIKALI IKO KWA AJILI YA KUWASAIDIA RAIA WAKE AU WAWEKEZAJI???

3. KAMA MKULO AMEWADANGANYA WANANCHI NA BUNGE JE JK UKO TAYARI KUMUAJIBISHA HUYU JAMAA????
 
Safi sana! hapo ndo tutajua maana ya serikali ya watu-Mbayuwayu.

Nasikia petrol stations sasa ni biashara kubwa ya viongozi wa serikali yetu kama ilivyokuwa daladala.

Naona wameheshimu bajeti ya mkulo pale alipowaongezea bei ya mafuta ya taa na pale alipopunguza hawakusikia.
 
Safi sana! hapo ndo tutajua maana ya serikali ya watu-Mbayuwayu.

Nasikia petrol stations sasa ni biashara kubwa ya viongozi wa serikali yetu kama ilivyokuwa daladala.

Naona wameheshimu bajeti ya mkulo pale alipowaongezea bei ya mafuta ya taa na pale alipopunguza hawakusikia.

Ni kawaida ya Serikali ya awamu hii kuongea kinyume. Waliongea kushusha wakimaanisha kupandisha.
 
Sometimes people need to be patient or at least use common sense... though we know common sense is not really common but let me say the following at least:-

Assuming you are Petrol Gas BusinessMan, Yeah! You bought 15mil. litres. of Gas on June 10th... and Of course the government of Tanzania taxed it at the prevailing rate...

Now comes July 1st,,, you still have stock you bought on June 10th, The question is will you reduce price b'se it was just mentioned in the parliament? Thats one.

Second.... Do you know how US Dollars is gain value against Euro recently? Do you know global oli market how much a barrel is sold today as opposed how it was sold during ministers speach?

Please let be serious... unless you have taken that into consideration you do not have even right to write here.

Good day
Kasheshe
 
Watu wa kipato kidogo hawapaswi kuishi.
Kupandisha mafuta ya taa sawa na kuvaa chupi la chuma halisi ili kujilinda na vvu.
 
Sometimes people need to be patient or at least use common sense... though we know common sense is not really common but let me say the following at least:-

Assuming you are Petrol Gas BusinessMan, Yeah! You bought 15mil. litres. of Gas on June 10th... and Of course the government of Tanzania taxed it at the prevailing rate...

Now comes July 1st,,, you still have stock you bought on June 10th, The question is will you reduce price b'se it was just mentioned in the parliament? Thats one.

Second.... Do you know how US Dollars is gain value against Euro recently? Do you know global oli market how much a barrel is sold today as opposed how it was sold during ministers speach?

Please let be serious... unless you have taken that into consideration you do not have even right to write here.

Good day
Kasheshe

Bad argument if at all you own any business.

Budget ilipunguza taxes. Tax ninalipa ninapokwenda kununua mafuta na punguzo limeanza tar 1 july. Kama kuna tatizo pia Taxes zote huombwa upya kama business person yeyote alilipa kupita kiasi (overcharged).


The time lag you are legalizing should therefore apply to all petroleum products, including kerosene. Why a litre of kerosene now obeys Mkulo's words and not other hydrocarbons.

 
Back
Top Bottom