MAGAMBA MATATU
JF-Expert Member
- Jul 2, 2011
- 646
- 1,174
Saturday, 02 July 2011 09:49 |
0diggsdigg Waandishi Wetu WAFANYABIASHARA wa mafuta ya petroli, dizeli na taa, ni kama wamegomea mpango wa serikali wa kushusha bei kupita bajeti ya serikali iliyotangazwa na waziri wa fedha ndugu MKULO, kufuatia kufutwa na kupunguzwa kwa viwango vya baadhi ya kodi zilizokuwa vikitozwa kweye bidhaa hizo. Lengo la serikali lilikuwa ni kupunguza ukali wa maisha kwa wananchi unaotokana na mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali unaochangiwa na gharama kubwa za uzalishaji na usafirishaji. Serikali pia kupitia bajeti yake iliyopitishwa na bunge hivi karibuni ilipendekeza kuongeza kiwango cha kodi kwenye mafuta ya taa ili kukabiliana na vitendo vya uchakachuaji wa mafuta vinavyofanywa na wafanyabiashara wasio waaminifu. Kulingana na mkakati wa serikali uliotangazwa na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), Haruna Masebu, Watanzania wangeanza kufaidika na mpango huo wa serikali kuanzia jana LAKINI HALI IMEKUWA TOFAUTI KABISA,. Jana, Julai 1, ndiyo ilikuwa siku ya kuanza kutekelezwa kwa bajeti mpya ya 2011/12 ya ndgu MKULO .Lakini uchunguzi wa Mwanachi umebaini kwamba bei za petroli na dizeli ziliendelea kuwa juu lakini lita moja ya mafuta ya taa ilipaa kwa ongezeko la Sh 500 zaidi. Kulingana na mkakati wa serikali bei ya mafuta ya taa ingeongezeka kwa wastani wa sh 400 kwa lita. Kabla ya jana Jijini Dar es Salaam dizeli na petroli ilikuwa inauzwa kwa wastani wa Sh 2,070 kwa lita wakati mafuta ya taa yalikuwa yanauzwa kwa wastani wa Sh 1,550 kwa lita. Katika uchunguzi wa Mwananchi kwenye vituo mbalimbali vya mafuta Jijini Dar es Salaam, hali ilikuwa ni ya kusikitisha na ya kukatisha tamaa kiasi kwamba baadhi ya watu walisikika wakisema; "hii ni serikali ya rushwa, hata mambo yake yanaenda kwa rushwa huku ikihubiri maneno matamu kwenye majukwaa ya kisiasa." Bei za mafuta Mabango kwenye vituo mbalimbali yalionyesha mauzo kwa kiwango cha lita kama ifuatavyo: Katika kituo cha Oil Com Temeke petroli ilikuwa inauzwa kwa Sh 2,090, dizeli Sh2,080 wakati bei ya mafuta ya taa Ilikuwa ni Sh2,086. Katika kituo cha FAB kilichopo Temeke Sudani mafuta aina ya petroli yaliuzwa kwa Sh2,050, dizeli Sh2,050 wakati kituo kingine kilichopo Temeke Sudani cha Big Born petroli ilikuwa ikiuzwa Sh2,070 dizeli Sh2,070 na mafuta ya taa 2086. 1. JE MKULO KWA HILI SUALA LA KUTOA BAJETI AMBAYO INAPINGANA NA UKWELI HALISI WA MAFUTA SI AMELIDANGAYA BUNGE NA WANANCHI KWA UJULA. 1. JE SERIKALI IKO KWA AJILI YA KUWASAIDIA RAIA WAKE AU WAWEKEZAJI??? 3. KAMA MKULO AMEWADANGANYA WANANCHI NA BUNGE JE JK UKO TAYARI KUMUAJIBISHA HUYU JAMAA???? |