BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,820
- 287,889
Pia atufahamishe kampuni hizo zilikuwa zinafanya biashara gani ya kuweza kuwa na mapesa mengi kiasi hicho. Hivi ni kweli kampuni binafsi zinaweza kuacha mapesa yao mengi kiasi hicho yapotee kirahisi namna hiyo? 


Mkulo asisitiza fedha za EPA si za serikali
Mwandishi Wetu, Dodoma
Daily News; Wednesday,June 25, 2008 @08:41
WAZIRI wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo amesema aliyoyasema bungeni kuhusu wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu Tanzania (BoT), ndiyo ukweli na kwamba waliohusika watachukuliwa hatua.
Mkulo alisema jana kuwa fedha hizo zilikuwa ni za kampuni binafsi na zilihamishiwa (BoT) kutoka Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ya zamani.
Kwa maneno haya, mimi sikutamka kwamba waliohusika na fedha za EPA hawatachukuliwa hatua, bali hatua zitachukuliwa baada ya Mheshimiwa Rais kupokea taarifa ya Kamati Maalumu na kuagiza utekelezaji wake, alisema Mkulo, akitoa ufafanuzi wa masuala kadhaa yaliyojitokeza wakati wabunge wakijadili Bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2008/2009, likiwamo suala la EPA na takwimu.
Kwa mujibu wa Mkulo, BoT ilikuwa wakala tu wa kulipa fedha hizo hivyo hakuna mantiki ya kuhoji kwa nini fedha za EPA hazikujumuishwa kwenye Bajeti ya Serikali.
Alisema waliopata fedha hizo kwa njia zisizo halali hawana uhusiano na waliokuwa wanaidai NBC.
Nilisema kwamba akaunti ya EPA ilitokana na akaunti za wafanyabiashara wa Tanzania zilizokuwa katika iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambao katika miaka ya 1980, walikopa kutoka nje ya nchi, malighafi za viwanda, vipuri, na zana nyingine za uzalishaji kwa njia ya suppliers credits, alisema Mkulo.
Mwishoni mwa wiki baada ya Mkulo kuhitimisha mjadala wa Bajeti na kupitishwa na wabunge, baadhi ya wabunge wa upinzani walidai kuwa Waziri huyo amelidanganya Bunge kwa kueleza kuwa fedha za EPA zilizochotwa BoT, hazikuwa za serikali wala BoT; hivyo wakapania kuibana serikali wiki hii hasa katika hotuba ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Kuhusu takwimu, Mkulo alisema takwimu zote za Bajeti ya Serikali zilikuwa sahihi na ni jambo la kawaida kuzibadili wakati wabunge wakiendelea kuijadili.
Serikali inarudia tena kusema kwamba hakuna takwimu za bajeti ambazo hazikuwa sahihi, na bajeti iliyoidhinishwa ndiyo iliyowasilishwa kwa kusomwa bungeni na Waziri wa Fedha, alisema.
Kwa mujibu wa Mkulo, tofauti ya takwimu zilisababishwa na mabadiliko ya taarifa za fedha na kwamba mabadiliko hayo yalifanywa baada ya vitabu kupelekwa kwa Mpigachapa.
Kwa kuwa taarifa ya mwisho imekuja baada ya vitabu vya bajeti kupelekwa kwa Mpigachapa, na baada ya Hotuba Bajeti kuandikwa na kuchapishwa, kiasi hiki cha shilingi bilioni 60.0 hakikuonyeshwa, bali kimeingizwa katika masahihisho, alisema Mkulo.
Mkulo asisitiza fedha za EPA si za serikali
Mwandishi Wetu, Dodoma
Daily News; Wednesday,June 25, 2008 @08:41
WAZIRI wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo amesema aliyoyasema bungeni kuhusu wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu Tanzania (BoT), ndiyo ukweli na kwamba waliohusika watachukuliwa hatua.
Mkulo alisema jana kuwa fedha hizo zilikuwa ni za kampuni binafsi na zilihamishiwa (BoT) kutoka Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ya zamani.
Kwa maneno haya, mimi sikutamka kwamba waliohusika na fedha za EPA hawatachukuliwa hatua, bali hatua zitachukuliwa baada ya Mheshimiwa Rais kupokea taarifa ya Kamati Maalumu na kuagiza utekelezaji wake, alisema Mkulo, akitoa ufafanuzi wa masuala kadhaa yaliyojitokeza wakati wabunge wakijadili Bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2008/2009, likiwamo suala la EPA na takwimu.
Kwa mujibu wa Mkulo, BoT ilikuwa wakala tu wa kulipa fedha hizo hivyo hakuna mantiki ya kuhoji kwa nini fedha za EPA hazikujumuishwa kwenye Bajeti ya Serikali.
Alisema waliopata fedha hizo kwa njia zisizo halali hawana uhusiano na waliokuwa wanaidai NBC.
Nilisema kwamba akaunti ya EPA ilitokana na akaunti za wafanyabiashara wa Tanzania zilizokuwa katika iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambao katika miaka ya 1980, walikopa kutoka nje ya nchi, malighafi za viwanda, vipuri, na zana nyingine za uzalishaji kwa njia ya suppliers credits, alisema Mkulo.
Mwishoni mwa wiki baada ya Mkulo kuhitimisha mjadala wa Bajeti na kupitishwa na wabunge, baadhi ya wabunge wa upinzani walidai kuwa Waziri huyo amelidanganya Bunge kwa kueleza kuwa fedha za EPA zilizochotwa BoT, hazikuwa za serikali wala BoT; hivyo wakapania kuibana serikali wiki hii hasa katika hotuba ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Kuhusu takwimu, Mkulo alisema takwimu zote za Bajeti ya Serikali zilikuwa sahihi na ni jambo la kawaida kuzibadili wakati wabunge wakiendelea kuijadili.
Serikali inarudia tena kusema kwamba hakuna takwimu za bajeti ambazo hazikuwa sahihi, na bajeti iliyoidhinishwa ndiyo iliyowasilishwa kwa kusomwa bungeni na Waziri wa Fedha, alisema.
Kwa mujibu wa Mkulo, tofauti ya takwimu zilisababishwa na mabadiliko ya taarifa za fedha na kwamba mabadiliko hayo yalifanywa baada ya vitabu kupelekwa kwa Mpigachapa.
Kwa kuwa taarifa ya mwisho imekuja baada ya vitabu vya bajeti kupelekwa kwa Mpigachapa, na baada ya Hotuba Bajeti kuandikwa na kuchapishwa, kiasi hiki cha shilingi bilioni 60.0 hakikuonyeshwa, bali kimeingizwa katika masahihisho, alisema Mkulo.