Mkulo aitengea wizara yake milion 500 za chai

Kikombe gani cha chai kinagharimu kiasi hiki... wenye datas za gharama halisi hebu tuwekeeni hapa kwa tathmini kikombe cha chai pia kitumbua kimoja au andazi moja vinagharimu kiasi gani hapo Dar...
Mkuu, sidhani kuwa wanazungumzia kitumbua kimoja au andazi moja. Hawa huwa wanatumia sambusa zaidi, tena si moja. Nadhani pia hualika watu kuwatembelea ili wapate chai na sambusa. Kaazi kweli kweli. Ngoja waje kuniomba kura waone.
 
Hiyo ndiyo hali halisi inayoendelea serikalini. Tusijiulize kwa nini tunashindwa sababu ziko wazi na huhitaji kufanya thesis kujua hilo. Hili la chai ni moja tu. Kila wizara ina kitengo cha planning. Waulize hao watu wa planning utajua kuwa tunaishi katika nchi ya kusadikika. Lakini siku zote tunajidanganya kuwa tunaendelea.

Hizi bajeti nyingi ukizifumua kwa mtindo kama huu utakuta humo ndani ni hela ya chai, Sitting allowances (kwenye vikao vinavyofanyika ofisini humo humo), training huwa zinapangiwa hela ndefu sana (na kwenda hizo training unahitajika kuwa na godfather), Safari za nje na ndani (ambazo hulipiwa full board, plus subsistence allowance), gharama za semina na makongamano mahotelini, etc ... etc. Ukiachana na hawa kuna vitengo kama usalama wa Taifa ambao matumizi yao hayahojiwi. Siku hizi huku mitaani ukiona nyumba ya ajabu unaambiwa huyo anafanya kazi usalama wa Taifa.

Spending hizo huwa ziko so uncontrolled na ni eneo ambalo tunapoteza karibu asilimia 40 ya kodi zote zinazokusanywa na TRA.
 
Au hii chai inayoombewa pesa Bungeni si chai ya kwenye kikombe????? Isije kuwa hatujawaelewa viongozi wetu hawa. Si ajabu ni chai ya kwenye kibahasha.

Maana wakikaa kwenye warsha/kongamano/semina na mikutano mingine yenye majina mbalimbali hupewa chai na vitafunwa vyake, chakula (caterer wanaemjua wenyewe), na mwisho kibahasha kirefu.

Wakifunga mkutano wao wa siku kibao, wanafanya sherehe. Yaani nchi hii....sijui tutafika wapi mwishowe.

Kwanini hizo seminar wasizifanye kwa mtandao (Webinar)?
 
1.hapo ni chai tu, siku tukija kuambia matumizi mengineyo kama ya stationaries and other facilities; huchelewi kuja kupewa figure ambayo utakuta kila mfanyakazi wa serikalini anatumia kalamu 3 kwa siku, rim 1 ya karatasi kwa siku, toilet paper piece/roller moja kwa siku etc etc etc

Kwa chai ya 1.5M kwa siku, ni haki yao kutumia Roller Moja ya TP kwa siku kwa kila mfanyakazi. Hiyo RUKSA!
 
Kweli Tanzania inaliwa na wenye meno, huyu Mkulo na Majambazi wenzake wa CCM wanazidi kuimaliza na kuitafuna nchi kwa kasi mpya, Nguvu za Kijambazi na Ari za Kifisadi, Rest in Peace Tanzania.
 
Au hii chai inayoombewa pesa Bungeni si chai ya kwenye kikombe????? Isije kuwa hatujawaelewa viongozi wetu hawa. Si ajabu ni chai ya kwenye kibahasha.

Maana wakikaa kwenye warsha/kongamano/semina na mikutano mingine yenye majina mbalimbali hupewa chai na vitafunwa vyake, chakula (caterer wanaemjua wenyewe), na mwisho kibahasha kirefu.

Wakifunga mkutano wao wa siku kibao, wanafanya sherehe. Yaani nchi hii....sijui tutafika wapi mwishowe.

Kwanini hizo seminar wasizifanye kwa mtandao (Webinar)?

Mkuu, nakubaliana na wewe. Serikali yetu huenda imetumia neno 'chai' ikimaanisha 'special attendance'. Kama maana yao ndo hii basi kiasi kilichtengwa hakitoshi. Mambo ya 'chai' hapa kwetu yanatisha!!! lakin sasa najiuliza, serikali inamuonga nani?? Au ndo mambo ya kujilipa 'baada ya kazi ngumu' za kuliletea taifa letu 'maendeleo'??
 
Watanzania wenzangu inasikitisha sana kuona kuwa nchi yetu haina viongozi waadilifu ambao wanajali maslahi na hali za wananchi. Ubinafsi na unafiki unaoonyeshwa na Mawaziri na Wabunge wetu kweli kabisa unaudhi na unastahili kulaaniwa.

Haiwezekani serikali ije na kauli mbiu ya KILIMO KWANZA itenge shilingi milioni 700 tu za kununulia matrekta kwa ajili ya KILIMO na wakti huo huo ikijitengea shilingi Bilioni 19 za chai na vitafunwa. Huu ni upumbavu na ujinga. Milioni 700 zaweza kununua matrekta 20 ambayo hayatoshi ukiyagawa kwa kila mkoa trekta moja moja.

Shilingi bilioni 19 zaweza kununua matrekta 540 ambayo yanaweza kugawiwa kila jimbo la mbunge yakabaki. Laiti wangelifanya hivyo tungeliwapongeza na kuwaambia kuwa hakika wame-maanisha kuwa KILIMO KWANZA.

Lakini walichofanya ni kugeuza kauli mbiu yao badala ya KILIMO KWANZA imekuwa ni CHAI NA VITAFUNNWA kwanza. Hii ni aiubu kwa Bunge letu,ni matusi na kejeli ambazo haziwezi kuvumiliwa na mtu yeyote. Jana tarehe 18 tumeshuhudia Bunge lote likipitisha upumbavu kama huuuu!!!!

Nihitimishe kwa kusema kwamba hizi Bilioni 19 hakika hazitaenda kwenye chai na vitafunwa. Mimi siyo mtabiri wala nabii lakini nina uhakika kabisa hizi pesa zimetengwa kwa ajili ya uchaguzi Mkuu wa 2010. CCM hapa kwa makusudi kabisa wametengeneza ka-EPA kadogo ili wapate pesa za kufanyia kampeni mwaka kesho. Wewe unafikiri watapata wapi pesa ya kuhonga wapiga kura na kununua shahada za wapiga kura???

Na ndiyo maana hata akina Selelii,Shibuda na wabunge wengine wa CCM wameipitisha bajeti hii kwa kuiunga mkono mia kwa mia. Si wanajua watakatiwa posho ya Kampeni za mwaka kesho.

Hakika CCM ni CHAMA CHA MAJAMBAZI.

Nawasilisha
 
Ndiyo maana hili li nchi letu haliendelei. Hela zinavuja kila upande... mara posho ya hili mara posho ya lile, mara fungu la chai...n.k. na kinachozalishwa wala hakilingani na matumizi! Grrrrr,
sa' mishahara yao minono minono wanatumia kufanyia nini iwapo chai na vitumbua vinanunuliwa kutoka kwenye fungu la walipa kodi - kununulia movie za kinajeria?!!
Umesahau kuwa Mkulo anatafuta pesa za kampeni next year? na kawatengea mawaziri wenzake kama huyo wa miundo mbinu ini ziwanusuru kurudi bungeni tena mwakani. Huoni kuwa ni aibu kama ulikuwa waziri kushindwa ubunge?.
 
Au hii chai inayoombewa pesa Bungeni si chai ya kwenye kikombe????? Isije kuwa hatujawaelewa viongozi wetu hawa. Si ajabu ni chai ya kwenye kibahasha.

Maana wakikaa kwenye warsha/kongamano/semina na mikutano mingine yenye majina mbalimbali hupewa chai na vitafunwa vyake, chakula (caterer wanaemjua wenyewe), na mwisho kibahasha kirefu.

Wakifunga mkutano wao wa siku kibao, wanafanya sherehe. Yaani nchi hii....sijui tutafika wapi mwishowe.

Kwanini hizo seminar wasizifanye kwa mtandao (Webinar)?

Recta, hivi katika hao hakuna waliopitia 'seminari' kwako?

Nina uhakika hapa wanamaanisha cha kwa sababu ukiangalia au ukijua hizo za semina mbona tutapata presha! hadi pinda kupigia kelel ujue ni kufuru mkuu omba usijue tu!
 
Wakati wa enzi za Nyerere kila mfanyakazi aliyetaka kunywa chai alikuwa anaenda na Thermos Flask yake ikiwa na chai iliyotengenezwa nyumbani. Hata Mkulo akiwa NPF alikuwa anafanya hivyo.

Kwa nini tusirudie mtindo wa zama hizo? Tungeokoa Shs 19 bilioni tungeweza kuwapatia watoto wetu madawati shuleni 3,800,000 ambao sasa wanakaa chini au kukalia mawe.

It is very disappointing. Lack of an effective political opposition to this government has led them to forget their role. Kuna kipindi ktk Chanel moja ya Televisheni kinachouliza "Je Tutafika?" by Makwaiya wa Kuhenga. Kwa staili hii ya Mkulo na J.K. hatufikiiiiiii.
 
Kuna aliyesoma budget yote akatuwekea hapa hicho kipengele cha 'Chai' katika tafsiri ya Kiswahili na Kiingereza? Sidhani kwamba kwenye budget imeandikwa 'chai' au 'tea'!

Enzi hizo kulikuwa na kipengele cha 'entertainment' na mambo kama entertainment allowances etc. Hiyo Entertainment sio chai ya wafanyakazi wizarani bali ni kwa ajili ya kuwakirimu (?) wageni mashuhuri wa wizara wageni wa kimataifa na hata wa kitaifa.

Pamoja na hayo, kama kweli 'chai' hiyo ni ya kiwango cha milioni 1.5 kwa siku inatisha.
 
Wala mshishangae...kumbukeni Lukuvi aliwaambia wanaolalamikia marupurupu makubwa kuwa "KILA MTU ANAKULA MEZANI KWAKE". Hivyo na nyie kuleni kwenye meza zenu...full stop!

Idumu Chukua Chako Mapema (CCM)
 
Hii yote ni kwa kuwa kutakuwa na uchaguzi mwakani kwa hiyo wizara mbili hizo zinatumika kuptisha hela watakazo zitumia!
Kama kila uchaguzi unapofika watu wanajichukulia hela bililions kiasi hich kwa ajili ya kununua watu je kuna haja gani ya kuwa na uchaguzi!!

Ni afadhali tuamue moja kusiwe na uchaguzi tuwe na rais wa milele hadi afe ndiyo tuchague mwingine!

Nimekataishwa tamaa mie!!!!!!!!!!!!
 
Wakati mnashangaa hayo, mpasha habari wangu amenieleza kuwa kuna Idara ndani ya Wizara ya Miundombinu imejitengea mabilioni kwa ajili ya maofisa wake kwenda safari za nje na masomo huko ughaibuni, huku idara hizo zikiwa na watumishi wachache sana. Waheshimiwa wabunge mnaombwa muombe maelezo ya kutosha kuhusu matumizi hayo ya kutisha yaliyotengwa kwa ajili ya watu wachache.

Mazee ishu technical tuwaachie wenyewe wataalamu, kuanza kumpangia mtaalamu kuhusu taaluma yake unakuwa huna tofauti na mwanasiasa....kama hiyo wizara imeona umuhimu wa ku-train watumishi wake mimi binafsi nawapongeza..tusitegemee miujiza kama watendaji wetu serikalini hawana maarifa na ujuzi wa kisasa..
 
Binafsi nakubaliana na hilo fungu provided litatumika ipasavyo wafanyakazi wapate staftahi yenye akili ili wasichelewe kazini au kuzurura huku na huko kupata staftahi..Watu wengi mnaopiga kelele hamwajali watumishi wa serikali, hasa wa ngazi ya chini jinsi wanavyopigika na mishahara midogo..bila kusahau hawana cha bonus wala marupurupu yeyote..

Mazee punguzeni jazba zisizo na maana.
 
Mkuu nimesoma hii habari nimebaki kichwa chini, yaani watu wana amua kuiba mchana kweupe! Jamani chai gani ya milioni 1.5 kwa siku?

Halafu hawa watu wanajilipa mishahara minono, bado wanajiwekea bajeti nono za vyai ma ofisini? vipi yule daktari anaye kesha akiokoa maisha ya binadamu wenzake hata maji ya moto hapewi kazini kwake?
Kwakweli nchi ina wenyewe.. ndo maana hadi wanajisahau na kutukana watu hovyo

Hizi lawama nyingine tunazutupa mahali pasipohusika..hivi ni lini mishahara ya serikali inapangwa kienyeji hivyo?
 
Hivi credibility ya viongozi wetu wengi iko wapi? Kwanini wanaendekeza mambo yanayotia shaka kuwa wanataka kufanya wizi au kutengeneza mazingira ya fraud?Kibaya hata wafanye tatizo gani, bado wamo tu.Kwa hali hii ya kunywa chai ya gharama kuliko lunch na diner tusahau kabisa mambo ya maendeleo!!

Mazee matumizi ya wizara yanafanyika kitaalamu na kunafanyika auditing baada ya kila mwaka wa fedha..sasa sioni fraud inayoiongelea ..labda tuhabarishane hapa tuweke kumbukumbu zetu vizuri..
 
Pamoja na hayo, kama kweli 'chai' hiyo ni ya kiwango cha milioni 1.5 kwa siku inatisha.

1.5 mil per huwezi kusema ni kubwa au ndogo iwapo hujapata mchanganuo wake. Tuanze kuzifanyia kazi taarifa tunazoletewa badala ya kujenga dhana na kuendelea kuijadili dhana wakati option ya kupata full story ipo.
 
Hivi kweli unaanzia wapi kuongea na hii Serikali, watu wanaotenga Tshs 19Bilioni kwa ajili ya chai na vitafunwa? Help me guys to understand them coz I dont! It is so dissapointing! Shame on them! I am sorry to say this lakini hapa Tanzania hatuna Viongozi !
 
Back
Top Bottom