Mkulima mbaroni kwa kumvunjia heshima Rais Samia na Dkt. Kikwete mtandaoni

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,010
9,875
MKAZI wa Kidete mkoani Morogoro anayejishughulisha na kilimo,Piniston Nzali (20) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kujibu mashtaka matatu ya kuchapisha mtandaoni taarifa yenye kuharibu hadhi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan na Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.

Piniston pia antuhumiwa kwa kosa la kushindwa kusajili laini ya simu iliyokuwa ikimilikiwa na mtu mwingine.

Kwa mujibu wa hati ya mashtaka iliyosomwa mahakamani hapo na wakili wa Serikali Sylivia mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Yusto Luboroga imedaiwa, Oktoba 8, 2022 katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mshtakiwa alichapisha taarifa yenye kuharibu heshima au hadhi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Aidha, katika taarifa hiyo inadaiwa, mshtakiwa kupitia mtandao wa Tiktok alichapisha video inayomuonesha Rais Samia akiimba jambo ambalo halikuwa la kweli.

Mshtakiwa pia anadaiwa kuchapisha taarifa inayofanana na hiyo ikimuonesha Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiimba kosa alilolitenda Oktoba 10, 2022 huku akijua kuwa jambo hilo halina ukweli.

Katika shtaka la mwisho, inadaiwa katika tarehe tofauti kati ya Oktoba Mosi, 2022 na Oktoba 20, 2022 mshtakiwa alitumia laini ya simu ambayo awali ilikuwa inamilikiwa na Benjamani Chaji bila kutoa taarifa ya mabadiliko ya umiliki kwa mtoa huduma.

Hata hivyo, mshtakiwa amekana mashtaka hayo na amerudishwa mahabusu mpaka kesho kesi hiyo itakapotajwa kwa ajili ya kueleza hatua za upelelezi ulipofikia.

1668107492926.jpeg


Chanzo: Dira Makini
 
Hizo pesa za kuhangaika na watu hawa minor wangezipeleka VETA au kule wanakopeleka TOZO zetu hence kutupunguzia TOZO huenda badala ya kutumia nguvu kuziba midomo kwa wanaomuona Mtawala kwa jicho la ku-criticise wangemuona vinginevyo..., hence wasingehangaika kuziba watu midomo...

Hivi wale kila siku wanaojaza humu nyuzi kwamba anaupiga mwingi sio wapotoshaji pia hence wafunguliwe mashitaka !!!

Huenda huyo Mkulima alishikwa na msongo wa mawazo hence kuchanganyikiwa kutokana na bei ya mbolea kuwa juu... Na sisi walaji sijui tumekosa mazao kilo ngapi kwa kupoteza hii nguvu kazi...
 
MamaSamia2025 una kwama wapi mama etu?🤣🤣
Mzani haujakaa sawa kabisa kwa Fish babies Kama mwanetu mliemdaka.
Kutumia jina la MamaSamia2025 haimaanishi mimi ni mama. Namaanisha Mama Samia tena 2025. Hili ni jina ambalo liko mbele ya muda. Kuhusu kijana aliyedakwa ingekuwa vema CHADEMA na wale wanaharakati wakamtetea. Vilevile wengine watajifunza kati ya uhuru wa kutoa maoni na uhuru wa kutukana/kudhalilisha.
 
Back
Top Bottom