Mkulima gani bado ana mahindi kwake leo?

comte

JF-Expert Member
Dec 11, 2011
8,171
5,905
Mheshima Rais wa Tanzania amesema jambo jema kuwa hataingilia bei ya mazao ya wakulima wanyonge na kuwachombeza kuwa sasa ndio wakati wa kuwalangua wale wasiolima.

Hofu yangu ni kuwa waliona mahindi sasa ni walanguzi ambao waliyanunua zamani kwa shs 270/- kwa kilo toka kwa wakulima miezi 4 iliyopita na sasa wanawauzia wakulima walioyalima kwa 900/= kwa kilo.
 
Mheshima Rais wa JMT amesema jambo jema kuwa hataingilia bei ya mazao ya wakulima wanyonge na kuwachombeza kuwa sasa ndio wakati wa kuwalangua wale wasiolima. Hofu yangu ni kuwa waliona mahindi sasa ni walanguguzi ambao waliyanunua zamani kwa shs 270/- kwa kilo toka kwa wakulima miezi 4 iliyopita na sasa wanawauzia wakulima walioyalima kwa 900/= kwa kilo.
Viongozi wetu mmmh hakuna mkulima hata mmoja mwenye stock!! Hapa wafanyabiashara watatajirika sana,hata mahindi yaliyo kwa godown za serikali wafanyabiashara ndio watanunua na kuwauzia wakulima...
 
Viongozi wetu mmmh hakuna mkulima hata mmoja mwenye stock!! Hapa wafanyabiashara watatajirika sana,hata mahindi yaliyo kwa godown za serikali wafanyabiashara ndio watanunua na kuwauzia wakulima...
Na usije shangaa mawaziri ndio wakawahi hiyo akiba ya serikali na kuuanza kutuuzia( rejea ya Dr. Kebwe!)
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom