mkulima ananufaika vipi na sera ya viwanda na biashara!!

frankfrut_

Member
Apr 24, 2015
20
8
Je serikali imejipangaje kumuinua huyu mkulima wa tangu 1961 analima mpaka leo lakini hana maendeleo!
Nadhani sasa tufike mahali tuweke siasa pembeni tuache sayansi ifanye kazi! serikali inabidi iwekeze Zaidi katika tafiti ili kuweza kufanya mambo yenye uwakika kuliko kujaribu. Serikali itumie taasisi zake za vyuo vikuu kufanya tafiti mbalimbali za kilimo na biashara. Tanzania ya viwanda inabidi iwe Tanzania ya sayansi na technologia sio siasa tena.
Tumekuwa tukiwapa wakulima pembejeo za kilimo zikiwemo mbolea mbalimbali bila kupima udongo una upungufu wa virutubisho gani, madhara yake unanufaika misimu mitatu alafu misimu ilio baki yote unapata hasara kwa kutokujua ardhi yako ilikuwa inahitaji nini na nini haiitaji.
Naweza kuongea mengi lakini serikali katika swala la viwanda inabidi iwekeze katika tafiti Zaidi
 
Back
Top Bottom