Mkulima adaiwa kuuawa mbele ya Mkuu wa Wilaya , migogoro ya Wakulima na Wafugaji Kata ya Magindu, Wilaya ya Kibaha

kidaru

Member
Mar 30, 2017
22
51
Tukio la kusikitisha la mauaji ya Mkulima limetokea Kijiji cha Lukenge Kata ya Magindu tarehe 27/03/2019 , mbele ya Mkuu wa wilaya ya Kibaha ndugu Asumpta Mshana , wakati alipoenda kujaribu kusuluhisha mgogoro wa Wakulima na Wafugaji kwenye kijiji hicho .

Chanzo cha tukio hilo ni Jamii ya wafugaji wa kimasai kupeleka na kunywesha mifugo yao kwenye Lambo la Maji linalotumika na Wanakijiji kwa mahitaji ya kawaida , hivyo Mtendaji na Mwenyekiti wa Kijiji , walienda hapo lamboni kwa lengo la kuwaambia wafugaji waondoke eneo hilo na badala yake waliambulia kipigo kilichopelekea Majeruhi ya viongozi hao na kukimbizwa hospitali ya Wilaya kwa matibabu zaidi.

Mkuu wa wilaya pamoja na Askari walifika kwa lengo la usuluhishi na kuhakikisha wahusika wanakamatwa. Wakati wa kikao ukaibuka mzozo kwa wakulima kudai kwamba askari waliotangulia kabla ya mkuu wa wilaya waliwakamata wahalifu lakini inaonekana walijenga mazingira rafiki na hatimaye wahalifu hao kukimbia mbele yao.

Mzozo huo na kurushiana maneno ukapelekea Vurugu kubwa iliyosababisha askari kurusha mabomu ya machozi na wakati wananchi wanatawanyika.

Jamii ya wafugaji ya wamang’ati wakaanza kurusha mikuki na hatimaye kupelekea mwananchi mmoja ajulikanaye kwa jina la Mzee jisu kufariki kwa kuchomwa Mkuki.

Mpaka sasa hakuna mshukiwa yeyote aliyekamatwa, japo jitihada za kuwatafuta zinandelea.
 
Tamaaa ya Polisi imeleta maaafa. TAKUKURU Wilaya mko wapi happo? Mkuu wa Mkoa naye aingie kati kuwashughulikia hao Polisi wanaocheka na Wahalifu na kusababisha kifo. Mwisho Serikali ya Kijiji iangalie uwezekano wa kuchepusha maji toka kwenye hilo bwawa ili kuweka kituo cha kunyweshea mifugo.
 
Tamaaa ya Polisi imeleta maaafa. TAKUKURU Wilaya mko wapi happo? Mkuu wa Mkoa naye aingie kati kuwashughulikia hao Polisi wanaocheka na Wahalifu na kusababisha kifo. Mwisho Serikali ya Kijiji iangalie uwezekano wa kuchepusha maji toka kwenye hilo bwawa ili kuweka kituo cha kunyweshea mifugo.
Una hakika na hiyo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tamaaa ya Polisi imeleta maaafa. TAKUKURU Wilaya mko wapi happo? Mkuu wa Mkoa naye aingie kati kuwashughulikia hao Polisi wanaocheka na Wahalifu na kusababisha kifo. Mwisho Serikali ya Kijiji iangalie uwezekano wa kuchepusha maji toka kwenye hilo bwawa ili kuweka kituo cha kunyweshea mifugo.
TAKUKURU na mauaji wapi na wapi mkuu?
 
Ifike mahali wenye mamlaka wawaachie watu majukumu yao
Kwa mfano hapo ilibidi afisa maendeleo ya jamii ahusike na siyo kwa kuitisha kikao baada ya kuwatishia na polisi
Ametaka kuharakisha mambo na mwisho wake ndo huo.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ifike mahali wenye mamlaka wawaachie watu majukumu yao
Kwa mfano hapo ilibidi afisa maendeleo ya jamii ahusike na siyo kwa kuitisha kikao baada ya kuwatishia na polisi
Ametaka kuharakisha mambo na mwisho wake ndo huo.


Sent using Jamii Forums mobile app
Sio simple kama Unavyofikirii nduguu...!! afisa maendeleo haongei kituu hapooo Atageuzwaa nyamaa... maana kila mtu anajiona ana haki ya kumiliki eneo hiloo sasa wewe onyesha unapendelea Wakulima uonee balaaa... Yani motoo unawakaa kwelii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ifike wakati tuache unafiki, wafugaji ni tatizo nchi hii, wanafuga kienyeji na hivyo kupelekea wao kutangatanga kila sehemu ya nchi, hatuwezi kwenda hivyo. Hawa watu wawe na maeneo maalumu ya kufugia na sio kurandaranda nchi nzima. Alafu kama nchi nzima tungekua tunatembea na mapanga na mikuki viunoni hali ingekua mbaya, huu utamaduni wa watu kubeba mapanga na mikuki upigwe marufuku, unahatarisha usalama wa wengine!
 
Dash poleni Sana , hila nchi hii wafugaji wanauwa Sana wakulima halafu wahusika wako kimya tu , juzi nilishangaa mfugaji inasemekana kauwawa na Askari magereza Moro , polisi kwa haraka wakawakamata Askari magereza lakini mfugaji kama angeua sidhani kama polisi wangewakamata wafugaji , pesa kweli inaongea
 
Wafugaji Wana pesa kwahiyo pesa inaongea, ndio maana hao jamaa wafugaji ni jeuri sana
 
Tukio la kusikitisha la mauaji ya Mkulima limetokea Kijiji cha Lukenge Kata ya Magindu tarehe 27/03/2019 , mbele ya Mkuu wa wilaya ya Kibaha ndugu Asumpta Mshana , wakati alipoenda kujaribu kusuluhisha mgogoro wa Wakulima na Wafugaji kwenye kijiji hicho . Chanzo cha tukio hilo ni Jamii ya wafugaji wa kimasai kupeleka na kunywesha mifugo yao kwenye Lambo la Maji linalotumika na Wanakijiji kwa mahitaji ya kawaida , hivyo Mtendaji na Mwenyekiti wa Kijiji , walienda hapo lamboni kwa lengo la kuwaambia wafugaji waondoke eneo hilo na badala yake waliambulia kipigo kilichopelekea Majeruhi ya viongozi hao na kukimbizwa hospitali ya Wilaya kwa matibabu zaidi. Mkuu wa wilaya pamoja na Askari walifika kwa lengo la usuluhishi na kuhakikisha wahusika wanakamatwa. Wakati wa kikao ukaibuka mzozo kwa wakulima kudai kwamba askari waliotangulia kabla ya mkuu wa wilaya waliwakamata wahalifu lakini inaonekana walijenga mazingira rafiki na hatimaye wahalifu hao kukimbia mbele yao. Mzozo huo na kurushiana maneo ukapelekea Vurugu kubwa iliyosababisha askari kurusha mabomu ya machozi na wakati wananchi wanatawanyika, Jamii ya wafugaji ya kimasai wakaanza kurusha mikuki na hatimaye kupelekea mwananchi mmoja ajulikanaye kwa jina la Mzee jisu kufariki kwa kuchomwa Mkuki.

Mpaka sasa hakuna mshukiwa yeyote aliyekamatwa, japo jitihada za kuwatafuta zinandelea.
Ukifuatilia hii migogoro utagundua wafugaji wanachekewachekewa sana. Maana mara zote ndio chanzo cha ugomvi


Pili inakuwaje watu wanakuja mkutanoni na mikuki? Hao majitu busara hayana kabisa so ilitakiwa nguvu itumike dhidi yao hata kuwatia vilema vya maisha ikibidi ili waheshimu wenzao.

Tatu nanyie wakulima mmezidi uzezeta maana kilasiku nyie ni kulialia tu wakati nyie ndio wenyeji wa hayo maeneo. Kila mgogoro mnakufa nyie tu wao wanadunda.
Na mpigwe tu hakuna jinsi maana tumechoka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tamaaa ya Polisi imeleta maaafa. TAKUKURU Wilaya mko wapi happo? Mkuu wa Mkoa naye aingie kati kuwashughulikia hao Polisi wanaocheka na Wahalifu na kusababisha kifo. Mwisho Serikali ya Kijiji iangalie uwezekano wa kuchepusha maji toka kwenye hilo bwawa ili kuweka kituo cha kunyweshea mifugo.
Simple and clear vitu vingine haviitaji mpaka vurugu za nn.. Wafuate hiu ushauri wako
 
Ifike mahali wenye mamlaka wawaachie watu majukumu yao
Kwa mfano hapo ilibidi afisa maendeleo ya jamii ahusike na siyo kwa kuitisha kikao baada ya kuwatishia na polisi
Ametaka kuharakisha mambo na mwisho wake ndo huo.


Sent using Jamii Forums mobile app
Chini ya utawala huu ukiwa mkuu wa wilaya au mkoa basi wewe unajua kila kitu
 
Sio simple kama Unavyofikirii nduguu...!! afisa maendeleo haongei kituu hapooo Atageuzwaa nyamaa... maana kila mtu anajiona ana haki ya kumiliki eneo hiloo sasa wewe onyesha unapendelea Wakulima uonee balaaa... Yani motoo unawakaa kwelii

Sent using Jamii Forums mobile app

Haongei anafata procedure
Hivi watu mmetoka kuwapiga mabomu
Wana muhemko mnawaitisha kikao,??


Sent using Jamii Forums mobile app
 
"Walijenga urafiki na polisi" itaki
uwa polisi walishikishwa kitu kidogo ili wakandamize upande mwingine... hiki ndicho chanzo cha hasira.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom