Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Leo wakati Mh. Anne Makinda akihairisha bunge alisikika akilalama juu ya zomea zomea iliyowakumba baadhi ya wana- CCM wakati wa mijadala ya kutoa maoni juu ya mswada wa marekebisho ya katiba. Jambo hilo limewashangaza wengi, maana katika siku za hivi karibuni mh. Makinda mwenyewe amekuwa akiendekeza zomea zomea ya wabunge wa CCM kwa wabunge wenzao wa CDM. Sasa kwakuwa kibao kimegeuka spika huyo anaona uchungu. Ama kweli, wale wanao mtuhumu kwa kuwa na upendeleo kumbe wanayo hoja.