Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 42weka
‘Lakini yule sio mzee,ukiangalai umri wako na yeye, huwezi kumuita yule mzee, yule ni saizi yako kabisa, au unataka kuolewa na dogodogo, usidanganyike, huko umeshakupita, sio kwako tena, huyo unayemuona ni mzee, ndiye saizi yako...’nikamshauri.
‘Simpendi, na simtaki....’akasema na mimi nikamuelewa, nikaona nimsaidie na nione vipi nitaweza kumfanya aishi maisha bila ya kutegemea wazazi wake, , kwani kwa muda huo alikuwa ameshakosana na wazazi wake kabisa..na wazazi wake, walisema kuwa binti yao huyo kazidi kwani kila mchumba anayemfuata yeye anamkataa,
‘Basi rafiki yangu mimi naona nikusaidie kwa hilo, unaonaje tukiwa washirika, ....?’ nikamuuliza.
‘Washirika kwa vipi, sisi ni marafiki tangia zamani, hilo la ushirika la kitu gani tena,…?’ akauliza.
Mimi namfahamu sana rafiki yangu huyo , hawezi kupata kazi ya kuajiriwa akatulia, sizani kama anaweza kuhimili sheria na taratibu za kazi, mara ngapi anaajiriwa na baada ya hata mwezi kuisha keshakosana na muajiri wake,...nikataka nimbadili kabisa aondokane na hulika hiyo, japokuwa hiyo ya kuchagua wanaume nilishindwa.
Nakumbuka wakati tunasoma rafiki yangu huyu alikuwa akipenda sana kazi za upelelezi, kutokana na kusoma vitabu mbali mbali vya hadithi za kipelelezi, na kuangalia sinema za namna hiyo,na hiyo ilikuwa ni ndoto yake kuwa akimaliza shule atajiunga na kazi za upelelezi.
Kwa bahati mbaya, ndoto yake hiyo haikuweza kufanikiwa, tulipomaliza shule, akajikuta akifanya kazi nyingine kutokana na matakwa ya wazazi wake, ambazo hakuweza kuzifanya itakiwavyo, akaanza kutafuta sehemu nyingine, na hata huko hakuweza kukaa muda mrefu,ikawa mtu wa kubadili kazi, mara leo yupo hapa , kesho yupo kule.
Basi siku hiyo alipokuja kwangu na malalamiko hayo juu ya wazazi wake, kutaka aolewe, mimi nikakumbuka ile ndoto yake hiyo, nikaona kwa vile tumekuwa watu wakusaidiana, kupendana, toka utotoni, ngoja na mimi nijaribu kumsaidia nionavyo mimi, na ndipo nikamapa wazo langu hilo nikamwambia;
‘Rafiki yangu mimi nataka kuifufua ile ndoyo yako ya shuleni, upo tayari....?’nikamwambia na yeye akawa kama hakunisikia,kwani wakati huo alikuwa anacheza na simu yake, nafikiri alikuwa akiandika ujumbe kwa watu wake, na baadaye akasema;
‘Ndoto ipi...?’ akaniuliza kwa dharau, na huku akiendelea kuangalia simu yake.
‘Kwanza rafiki yangu nakutaka unielewe, nikiongea na wewe uhakikishe kweli unaongea na mimi, ....kama bado una tabia za utoto, hutafika mbali, weka hiyo simu pembeni, nataka tuongee kikubwa....’nikasema kwa sauti ya ukali, na yeye aliponiangalia usoni akakutana na uso wa kazi, uso unaoashiria amri, akashangaa, kwanza, halafu akabetua mdomo, na kusema.
‘Ok. Bosi, maana kwa vile wewe ni bosi kwenye kampuni zako unafikiria kila mtu utamsimamia hivyo hivyo..lakini kwa vile nimekwama, nitakusikiliza bosi....’akasema huku akiiweka simu yake pembeni.
‘Nakumbuka wewe ulikuwa na ndoto ya kuwa askari mpelelezi...lakini haikuwezekana, sasa nataka hilo liwezekane, hujachelewa, utakwenda kusomea hilo, lakini sio askari mpelelezi wa kipolisi, nataka uwe mpelelezi wa watu binafsi,...mpelelezi muhutasi, hiyo si inawezekana...?’ nikamuuliza. Na yeye kwanza akawa kama haamini hilo kwani muda umeshapita, na huenda hakuwa na wazo hilo tena.
‘Mhh, hilo nilishalitoa akilini, hayo yalikuwa ya kishule, ...sijui kama inawezekana, sina uhakika na hilo.na hiyo kazi inapatika kweli, maana nahisi nitahitajika kwenda jeshini, na huu mwili sizani kama utakubali shuruba, na amri.....’akasema.
‘Inawekana,....kwanini isiwezekane, kila kitu ni nia, kila kitu ni utashi, na dhamira ya kweli, sasa hivi vipo vyuo vingi tu vya kutoa hayo mafunzo, na hata kwenye mitandao kuna elimu kama hiyo, tuifanyie kazi, ...na na kwa vile mimi nakuhitajia kwenye mambo yangu,...tushirikiane, tutaweza...upo tayari....?’nikamuuliza.
‘Sijui...tuone ,..’akasema na mimi nikafahamu kuwa yupo tayari, nikamwambia ili aonyeshe dhamira ya kweli, basi ahangaike mwenyewe kuvitafuta hivyo vyuo, na mimi nitamsaidia kwa hali na mali. Na kweli baada ya siku kadhaa akasema keshapata chuo cha namna hiyo, na yupo tayari kwa masomo, na mimi nikamwambia nitawasiliana na wahusika wa hicho chuo.
‘Kwani ni mpaka wewe uwasiliane nao, cha muhimu ni maombi, na maombi nimeshatuma na wao wameshanikubali, kilichobakia na malipo..hakuna zaidi....’akasema.
‘Usijali..malipo nitalipa, lakini kama nilivyokuambia, mafunzo hayo ni kwa ajili ya kazi zangu, kwahiyo nataka niongee nao, nione jinsi gani wanaweza kukupika nitakavyo mimi....’nikasema na kweli nikaenda kuonana na wahusika wa hicho chuo, na tutakakubaliana, kwani nilitaka kwanza wamjenge huyo binti kikakamavu, na kuondoa ulegelege wa kutegemea wazazi,..na wao wakasema hiyo kwao ni kazi ndogo tu.
Sikuamini, huenda ni kwa vile, alikuwa na ndoto hiyo, au ni dhamira tu, ilimtuma ajitume hivyo, kwani, aliweza, na akafuzu vizuri sana, na kuna muda aliombwa ajiunge na askari polisi, lakini yeye mwenyewe alikataa, na akaja kwangu na kusema yupo tayari kwa kazi zangu, na tukaingia naye mkataba, akawa ni mtu wangu nikimuhitajia, lakini hapo hapo akawa kaajiriwa kwenye kazi fulani.
Nikawa kila nikipata kazi inayohitajia mambo hayo, nimampa ananifanyia, namlipa vizuri tu, au wakati mwingine anapata kazi zake nyingine binafsi akikutana na mawakili binafsi kuchunguza kesi fulani, basi ikawa ndio kazi yake nje ya ajira yake.
Kwa hali kama hiyo tukawa ni kitu kimoja, na kikazi mimi ni bosi wake, na haikutokea siku nikampa kazi, akaikataa,...
Kwahiyo ni mtu nilishibana naye, na ananiheshimu mimi na familia yangu, na alishaapa kuwa hataweza kunifanyia jambo baya,…je kwa hali kama hiyo ninaweza kuamini mambo ya kusikia tu…hapana, ilihitajia mud asana kuyaamini maneno ya watu
****************
‘Kwahiyo umenielewa, nikamuuliza , wakato docta naye anaongea na simu
‘Nitafanyaje sasa..inabidi…’akasema
‘Unajua ni kwanini nataka hili, ni ili jamii isije kuniona mimi mjinga, kuwa nafuga nyoka,…hilo linawezekana kweli, kuwa nilifanya yote hayo kwa mtu ambaye atakuja kunizunguka, …’nikasema
‘Lakini…..’akataka kujitetea
‘Sikiliza…mimi sitakubaliana na mawazo yao hata mara moja kuwa wewe rafiki yangu unaweza kunisaliti mimi, nitauweka wapi uso wangu…sasa ni wewe kuilinda hiyo hali, sizani kama unaweza kufanya jambo kama hilo…sizani, …au ..niambie ukweli hapa hapa, je ni kweli…?’ nikamuuliza
‘Mim naondoka….’akasema sasa akitikisa kichwa cha kuchanganyikiwa.
‘Sawa, mimi nakuamini, na..unasikia, …mimi nimeosha mikono yangu, nimechukua dhamana yako mikononi mwangu.., na wewe usije kuniangusha kwa hilo,…umenielewa lakini, na nataka hata wazazi wangu ikiwezekana wasijue kuwa mume wangu kapatwa na ajali, nataka tufanye namna ambayo, sawa ni ajali, lakini kwa mazingira yasiyo kuwa na kashfa, sawa..umenielewa hapo..?’ nikamuuliza
Nilimuona kama anataka kutoa machozi, lakini mimi sikujali,..najua sio mtu wa kutoa machozi, labda kitu kimemuingia machoni,…na muda huo nilikuwa kikazi zaidi, sikutaka kupoteza muda, nilitaka yeye aifanye hiyo kazi, na nione ukweli wake kupitia kwake yeye mwenyewe…., nilikuwa na maana yangu kubwa tu.
‘Ninataka wewe….uifanye hiyo kazi, sitaki utani, nataka tumfahamu huyo mtu, ni nani anaweza kuingilia ndoa yangu, au kama kuna jingine, tulijue mapema…, kwanini mume wangu awe hivyo…hapo kuna mawili, kashfa ya ndoa, au…kuna tatizo kazini, mimi sijui, wewe ni mtaalamu wa mambo hayo, sasa mimi nahitaji msaada wako, hii ni kazi nimekupa…’nikasema kwa hasira
‘Mimi naondoka….’akasema sasa akitaka kuondoka
‘Ondoka bwana,… mimi naondoka, mimi naondoka…ila kumbuka mimi…sitaki utani, …unanielewa, sitaki utani kwenye ndoa yangu kwenye kazi yangu, kwenye maisha yangu…ole wake huyo mtu, sitajali ni nani…hili nakuambia wewe kama rafiki yangu, ukisikia mimi nimefanya jambo, hutaamini….’nikasema kwa jaziba.
‘Sawa bosi....naondoka…’akageuka na nikahisi kuna mtu nyuma yangu nikageuka kwa haraka, nikiwa sasa naangalina uso kwa uso na baba yangu mzazi.
‘Baba…….’nikasema kwa mshangao mkubwa, wenye wasiwasi,
‘Kuna nini kimetokea…?’ ilikuwa sauti ya baba ya kiaskari
WAO LA LEO: Mara nyingi tunapokuwa na shida, tunasahau kuwa wenzetu pia na wao wana shida kama hizo za kwetu au huenda shida zao ni zaidi ya shida zetu, wakati huo wa shida, hatujali shida za wenzetuo,cha muhimu kwa wakati huo ni shida zetu, tunachotamani ni jinsi gani ya kusaidiwa, ni jinsi gani, shida zetu zitachukuliwa kipaumbele, na hapo utaanza kuwachuja marafiki zako, na rafiki utakayemuona ni wa kweli kwako ni yule atakayesimama kwenye shida zako, na kutetea hoja zako.
Tukumbuke kuwa,sisi sote ni wanadamu, na shida zimeumbiwa kwetu, na kwahiyo sote ni wahitajia,kama ni hivyo basi, ili tuwe sawa, tujaribu kuona shida za wenzetu zina umhimu sawa sawa na shida zetu.