Mkuchika apiga marufuku viongozi wa Serikali kuwatengua watu ambao hawakuwateua

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,495
9,275
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika, amepiga marufuku viongozi wa Serikali kuzuia barua za watumishi kufika eneo linalohusika na kwamba hata kama inakwenda kwake ni lazima iachwe na imfikie.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika

Waziri Mkuchika ameyasema hayo leo Desemba 6, 2019, Jijini Dodoma, ikiwa ni kuelekea kwa Siku ya Maadili na Haki za Binadamu, ambapo amesema baadhi ya wakuu wa idara wamekuwa ni chanzo cha uvunjifu wa haki za binadamu hivyo lazima wabadilike vichwani mwao.

Aidha Mkuchika amewaonya viongozi wanaowafukuza kazi watu ambao hawajawateuwa na hawana mamlaka nao kwani kwakufanya hivyo ni ukiukaji wa Haki za Binadamu.
 
Mkuchika anaongea tu hana meno! Unakumbuka alikataza Ma-DC na RC kuwaweka watu ndani? Lakini to date huu upuuzi unaendelea
Ma-DC na Ma-RC wanaweka watu ndani kwa mujibu wa sheria na sheria hiyo waziri Mkuchika anaijua , iweje atoe agizo la kuzuia wasitende kazi kwa mujibu wa sheria? Acha upotoshaji na sema ukweli uliosemwa na Mkuchika
 
Ma-DC na Ma-RC wanaweka watu ndani kwa mujibu wa sheria na sheria hiyo waziri Mkuchika anaijua , iweje atoe agizo la kuzuia wasitende kazi kwa mujibu wa sheria? Acha upotoshaji na sema ukweli uliosemwa na Mkuchika
Mbona kama vile umepaniki? Si utafute uweke humu? Malumbano ya nini? Mkuchika alisema na alinukuu sharia, kuwa MTU anawekwa ndani tu pale inapothibitika kuwa akiachwa uraiani ataleta madhara au tuseme atahatarisha usalama, sasa wewe nambie, yule Dogo wa Arusha ambaye alikiri kuwaweka ndani maofisa wake hasa Walimu na watendaji pasi kuwasikiliza walisababisha uvunjifu gani wa amani? Usijibu kwa kukurupuka na usitetee ujinga
 
Mbona kama vile umepaniki? Si utafute uweke humu? Malumbano ya nini? Mkuchika alisema na alinukuu sharia, kuwa MTU anawekwa ndani tu pale inapothibitika kuwa akiachwa uraiani ataleta madhara au tuseme atahatarisha usalama, sasa wewe nambie, yule Dogo wa Arusha ambaye alikiri kuwaweka ndani maofisa wake hasa Walimu na watendaji pasi kuwasikiliza walisababisha uvunjifu gani wa amani? Usijibu kwa kukurupuka na usitetee ujinga
Kama alisema hiki ulichosema hapa, kwa Nini mwanzo ulipotosha alisema watu wasiwekwe ndani? Ulitakiwa ku-specify na si ku-generalise kama ulivyofanya.
 
Kama alisema hiki ulichosema hapa, kwa Nini mwanzo ulipotosha alisema watu wasiwekwe ndani? Ulitakiwa ku-specify na si ku-generalise kama ulivyofanya.
Duh! Huwa sipendi kubishana! Sio lazima uelewe kila kitu! Vingine waachie wengine wajibu ndugu! Maana kama vile unataka kuleta ligi! Labda wewe uliposema wanawaweka watu ndani kwa mujibu wa sharia, ulipotosha au ulikua sahihi.???
 
Duh! Huwa sipendi kubishana! Sio lazima uelewe kila kitu! Vingine waachie wengine wajibu ndugu! Maana kama vile unataka kuleta ligi! Labda wewe uliposema wanawaweka watu ndani kwa mujibu wa sharia, ulipotosha au ulikua sahihi.???
Usipotoshe ukweli huku ukijua uhalisia ulivyo
 
Ma-DC na Ma-RC wanaweka watu ndani kwa mujibu wa sheria na sheria hiyo waziri Mkuchika anaijua , iweje atoe agizo la kuzuia wasitende kazi kwa mujibu wa sheria? Acha upotoshaji na sema ukweli uliosemwa na Mkuchika
Ndugu yangu naona wewe ni mjinga wa hiyo shetia ya MaRC na maDC kuwaweka watu ndani kwa masaa yasiyozidi masaa 48. Wanaruhusiwa kufanya hivyo kwa condition maalum. Siyo kwa namna ya hovyo hovyp kama wanavyofanya sasa hivi.
 
Ndugu yangu naona wewe ni mjinga wa hiyo shetia ya MaRC na maDC kuwaweka watu ndani kwa masaa yasiyozidi masaa 48. Wanaruhusiwa kufanya hivyo kwa condition maalum. Siyo kwa namna ya hovyo hovyp kama wanavyofanya sasa hivi.
Jifunze kufanya utafiti na uchambuzi kabla ya kuongea au kuandika ,hili litakusaidia kuepuka kupotosha ukweli na uhalisia. Sheria hiyo Mimi naifahamu na ninafahamu mazingira yote sheria hiyo inapotakiwa kutumika na waziri Mkuchika alipotoa agizo kwa wakuu wa mikoa na wilaya nilimsikiliza na kumuelewa, mwanaJF anayeitwa Elli hapo juu alii-generalize kauli ya mhe.waziri na kuonekana kaipotosha kwamba mhe. Waziri aliagiza wakuu wa wilaya na mikoa wasiweke watu ndani.

Naweza kusema umekurupuka na umeandika vitu vilivyokuzidi uwezo
 
Mbona kama vile umepaniki? Si utafute uweke humu? Malumbano ya nini? Mkuchika alisema na alinukuu sharia, kuwa MTU anawekwa ndani tu pale inapothibitika kuwa akiachwa uraiani ataleta madhara au tuseme atahatarisha usalama, sasa wewe nambie, yule Dogo wa Arusha ambaye alikiri kuwaweka ndani maofisa wake hasa Walimu na watendaji pasi kuwasikiliza walisababisha uvunjifu gani wa amani? Usijibu kwa kukurupuka na usitetee ujinga
Kauli njema hujenga na kuelimisha wasioelewa. Hakuna sababu ya kufoka kwa mtu asiyejua bali kumpa elimu.
 
Back
Top Bottom