Muungano wetu: Mgao wa Fedha za IMF na Zanzibar kupewa asilimia 18, ni sahihi?

Hamatan

JF-Expert Member
Nov 10, 2020
3,183
7,645
Hivi karibuni, kuna taarifa zilizowekwa wazi kwenye baadi ya vyombo vya habari, juu ya mgawanyo wa mikopo ya nje, kati ya Tanzania bara na Zanzibar.

Mkopo wa pesa ya Uviko 19, tunaambiwa Zanzibar ilipata 18%. Mkopo wa kutoka Japan, tunaambiwa Zanzibar imepata 30%.

Mkataba wa Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar, umeweka wazi kanuni ya mgawanyo wa mikopo na misaada kutoka nje, ambapo Zanzibar inastahili kupewa 4.5%.

Kama ni kweli Zanzibar ilipata 18% badala ya 4.5%, na pia ilipata 30% badala ya 4.5%, waliohusika wote, wakiongozwa na Waziri wa Fedha na Katibu Mkuu Wizara ya fedha, walistahili wasimamishwe mara moja, na kama tungekuwa na Bunge, lilistahili kuunda kamati kuchunguza ukweli wa jambo hili, na kuchunguza uhusika wa Rais katika ukiukaji huu wa kanuni za Muungano.

Jambo la kujiuliza:

1) kwa hali hii ya sasa, ambapo nchi haina bunge linalowakilisha wananchi, nani ataihoji serikali?

2) kama trend itaendelea hivi, mpaka kufikia 2025, hali itakuwaje?

3) kama hiki ndicho kinachoendelea, hatuoni kuna njama za kuitumia Tanganyika kuijenga Zanzibar, na kuifanya Tanganyika kuwa 'kubwa jinga?'

4) Hali ikiendelea hivi, na bunge hatuna, nani ataweza kuhoji juu ya jambo hili?

5) Je, hatuoni kuwa kama hali hii ni kweli, mikopo hii inailenga Zanzibar, na Tanzania bara inatumika tu kama daraja, huku kisheria deni likiwa la kwake?

6) Japo hatuombei, kama kukiwa na njama ambazo zikafanya siku moja Muungano ufe, hatuoni hasara itakayokuwepo kwa Tanzania bara kwa sababu madeni haya yote mkopaji ni yeye, na hivyo ndiye atakayewajibika kulipa?
 
Vitambulisho vya wamachinga kwa Zanzibar vimeboreshwa ili waweze kukopesheka ila kwa hapa bara wamachinga wanawindwa kama magaidi vile eti kisa tu wazungu wanataka wakija wapate pa kupita.
 
Vitambulisho vya wamachinga kwa Zanzibar vimeboreshwa ili waweze kukopesheka ila kwa hapa bara wamachinga wanawindwa kama magaidi vile eti kisa tu wazungu wanataka wakija wapate pa kupita.
Comrade tunaomba ushauri wako, tufanyeje sasa?
 
kuna tatizo kubwa la ufahamu wa kiakili kwa watanganyika. Aliewaambia kuwa deni linalipwa na Tanganyika ni nani? Deni linalipwa JMT na sio tanganyika, sasa kwanini watanganyika wamekua wakijimilikisha Tanzania?
 
Kunashida mahali,,kwanini serikali inaogopa kusema wazi,,hata wapinzani akina act wazarendo wakohivyohivyo,,kiwa kimya
Kwa upande wa ACT wazalendo unatakiwa kutambua kuwa, chama hiki ni CUF iliyochukua jina la ACT. Ma CUF, kimsingi nguvu na ngome yake ni Zanzibar, ambayo ndiyo inayonufaika na hali hii ya uvunjaji wa kanuni.

Kitu kinachokunufaisha, kutamka kuwa hiki ninachonufaika nacho siyo halali yangu, kunahitajika uadilifu wa hali ya juu ambao wengi hawana. Kwa hulka ya kiongozi mkuu wa ACT bwana Zito, ambaye zaidi huangalia fursa, hawezi kutoa kauli juu ya hili kwa hofu kuwa wenzake wa Zanzibar, na ndiyo wenye nguvu kwenye chama, hawatamwunga mkono.

Kwa hiyo usitarajie kauli yoyote toka ACT dhidi ya ukiukaji huu.
 
Weka hapa huo mkataba wa Muungano.Pili unaelewa maana ya kero za Muungano? Na je mkataba ni biblia au msahafu?

Mwisho Zanzibar sio Mkoa ni Nchi na pia ni sehemu ya JMT kwa hiyo ina haki zote na tena haki zaidi ya Mkoa.
 
Kwa upande wa ACT wazalendo unatakiwa kutambua kuwa, chama hiki ni CUF iliyochukua jina la ACT. Ma CUF, kimsingi nguvu na ngome yake ni Zanzibar, ambayo ndiyo inayonufaika na hali hii ya uvunjaji wa kanuni.

Kitu kinachokunufaisha, kutamka kuwa hiki ninachonufaika nacho siyo halali yangu, kunahitajika uadilifu wa hali ya juu ambao wengi hawana. Kwa hulka ya kiongozi mkuu wa ACT bwana Zito, ambaye zaidi huangalia fursa, hawezi kutoa kauli juu ya hili kwa hofu kuwa wenzake wa Zanzibar, na ndiyo wenye nguvu kwenye chama, hawatamwunga mkono.

Kwa hiyo usitarajie kauli yoyote toka ACT dhidi ya ukiukaji huu.
Wewe Ni mpumbavu.

Unachojaribu kukipambania hukijui.

Unataka watanganyika waungane kupambania haki yao na wakati huo huo uko busy kuhubiri utengano na kujiona wewe ndio Bora na mpambanaji kuliko yeyote.

Sasa pambana na mpaka utakufa na hakuna kitu chochote utafanikiwa.

Zanzibar itaendelea kuchukua mpaka asilimia 100 na hakuna kitu utafanyaje.

Endelea kununua vibando uweke, yingie mitandaoni ubweeeeke, halafu ukalale uendelee na kupiga miayo mboweeee mboweeee mboweeee.
 
Wewe Ni mpumbavu.

Unachojaribu kukipambania hukijui.

Unataka watanganyika waungane kupambania haki yao na wakati huo huo uko busy kuhubiri utengano na kujiona wewe ndio Bora na mpambanaji kuliko yeyote.

Sasa pambana na mpaka utakufa na hakuna kitu chochote utafanikiwa.

Zanzibar itaendelea kuchukua mpaka asilimia 100 na hakuna kitu utafanyaje.

Endelea kununua vibando uweke, yingie mitandaoni ubweeeeke, halafu ukalale uendelee na kupiga miayo mboweeee mboweeee mboweeee.
Nimeuliza swali dogo kama Tzn hainufaiki na Muungano mbona hawaiiubalii Zanzibar kuwa na Serikali huru? Kwa nini serikali 3 hazikubaliwi?
 
Weka hapa huo mkataba wa Muungano.Pili unaelewa maana ya kero za Muungano? Na je mkataba ni biblia au msahafu?

Mwisho Zanzibar sio Mkoa ni Nchi na pia ni sehemu ya JMT kwa hiyo ina haki zote na tena haki zaidi ya Mkoa.
Kama Zanzibar ni nchi, ilistahili kukopa yenyewe na siyo kutumia mgongo wa nchi nyingine.

Siyo ikope Tanganyika, hela iende Zanzibar, idaiwe Tanganyika.
 
Wewe Ni mpumbavu.

Unachojaribu kukipambania hukijui.

Unataka watanganyika waungane kupambania haki yao na wakati huo huo uko busy kuhubiri utengano na kujiona wewe ndio Bora na mpambanaji kuliko yeyote.

Sasa pambana na mpaka utakufa na hakuna kitu chochote utafanikiwa.

Zanzibar itaendelea kuchukua mpaka asilimia 100 na hakuna kitu utafanyaje.

Endelea kununua vibando uweke, yingie mitandaoni ubweeeeke, halafu ukalale uendelee na kupiga miayo mboweeee mboweeee mboweeee.
I am very sorry, this article is not for the brainless.
 
Back
Top Bottom