Elections 2010 Mkono wa birika umeigharimu chadema chaguzi hii?

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,422
911,172
Kwa vituo takribani 52, 000 Chadema ilipaswa kutumia bilioni tatu kuwalipa mawakala kwa vituo vyote nchi nzima na kwa shilingi elfu hamsini kwa kila wakala.................kwa kutofanya hivyo na kuwategemea wagombea udiwani na ubunge kuwagharimia mawakala ulikuwa ni mkono wa birika ambao sasa machungu yake wote tunayaona..........

Pale ambapo NEC iliyoteuliwa na CCM ilipoamua kutowalipa mawakala Chadema ilipaswa kushtuka kuwa ni mkakati mzito wa CCM wa kuwarubuni mawakala kusaini matokeo ambayo yawezekana siyo sahihi....................Taarifa nilizonazo Chadema wanadai wanazo takwimu ambazo zaonyesha Dr. Slaa kashinda Uraisi.....kama hizo taarifa ni kweli basi mkakati wao ulikuwa ni sahihi.............lakini kama siyo ni kweli basi kurudia kuhesabu kura katika chaguzi zote zenye utata ni jambo la muhimu kwa minajili ya kuwatoa hofu wapigakura kama kweli sauti yao haikudhulumiwa na ufisadi wa CCM...........................

Hili ni la muhimu hata kwa CCM yenyewe katika kuweza kupata uhalali wa kuongoza nchi bila ya zengwe na mashaka kuwa ni dhuluma tu ndiyo inawaweka madarakani..........na aliyeingia madarakani kwa dhuluma ataendeleza dhuluma kubaki madarakani na katika kuwatumikia raia....

Huko tuendako Chadema iwe na mkakati wa kuweka fungu mapema la kuwalipa mawakala nchi nzima kuondokana na wasi wasi kuwa mawakala wana ukata mkubwa kiasi kuwa waweza kununuliwa........uwakala ni kazi yenye kustahili kuheshimiwa kwa malipo pamoja na kuwepo punje punje za kujitolea................
 
Hivi Ruta umesha-ongea na wakala yeyote wa CHADEMA na aka-sema hakulipwa????
 
Mimi sitahitaji shilingi hata moja kusimamia mahala popote chadema watanihitaji. Fedha isiwe kigezo cha ukombozi wa nchi yetu. Tunahitaji kujitoa zaidi kuliko kutegemea tulipwe. Kutegema chama kuwalipa ni kukubali kuwa mawakala wetu wetu walikuwa kwa maslahi binafsi zaidi kuliko wananchi wa Tanzania.
 
Rutashuba---nanihii

regardless of what you think, opposition will have a smooth ride on 2015. because chadenma have paved the way for their progress

we roll tings'/...........
 
Mimi sitahitaji shilingi hata moja kusimamia mahala popote chadema watanihitaji. Fedha isiwe kigezo cha ukombozi wa nchi yetu. Tunahitaji kujitoa zaidi kuliko kutegemea tulipwe. Kutegema chama kuwalipa ni kukubali kuwa mawakala wetu wetu walikuwa kwa maslahi binafsi zaidi kuliko wananchi wa Tanzania.

Kudos Aeka Mangi.

The issue of money for service to your party is the CCM way. I dont think we should go the same way to build CHADEMA, CUF, or any other political party in that matter. This will set a bad precedent that money is the issue. I believe that the ideology and the urge to serve is the building block for a strong and cohesive party. Members will have to understand that party politics is not about individuals gains but community service whose dividends have public interests. Tusianze mambo ya wajumbe wa kikao kujilipa madonge manono kuliko manufaa ya kikao chenyewe.

It will be hard to a society and leadership used to benefit from these clandestine payments, however, we need to be principled otherwise five to 10 years to come, we will find ourselves in the CCM mess today!!!
 
Mimi sitahitaji shilingi hata moja kusimamia mahala popote chadema watanihitaji. Fedha isiwe kigezo cha ukombozi wa nchi yetu. Tunahitaji kujitoa zaidi kuliko kutegemea tulipwe. Kutegema chama kuwalipa ni kukubali kuwa mawakala wetu wetu walikuwa kwa maslahi binafsi zaidi kuliko wananchi wa Tanzania.

Nakubaliana na wewe mia kwa mia ndugu yangu. Ukombombozi wa kweli ni lazima uanzie kwenye nafsi ya mtu mwenyewe kwani unaweza kuwalipa mawakala hata laki moja na kama bado ni mtu asiyena maono na dhamira ya kweli basi wakala huyo akihongwa millioni moja atahujumu ushindi wa chama tu.
Maana tafsini kwake amekosa maono na utashi. Hivyo fedha isiwe kigezo bali pengine staili ya kupata mawala pengine ingeweza kufanywa kwa umakini wa ziada badala ya hii kamata kamata ya last minutes ili kukamilisha number ya mawakala. Wawe ni watu wenye quality na dhamira dhabiti.
 
You should not have said this buddy, but i do not only respect you but also i respect your analysis. As for me dude money should never ever be the hurdle against our political and economic struggles against the fisadis!
 
Ruta.. CHADEMA (Tanzania ya kweli ) haihitaji malipo ya kifisadi kama haya!!! Hivi kura kama ni kwa ajili ya Maendeleo Yetu inahitajikulindwa na mwanadamu!!!! Wacha wajitwike laana ya kuiba haki za watu watakaa utumwani miaka 430 (Naona prof yako ina Bible) nafikiri unaelewa maanayake - WANA WA YAKOBO NA FARAO
 
Rutashuba---nanihii

regardless of what you think, opposition will have a smooth ride on 2015. because chadenma have paved the way for their progress

we roll tings'/...........
Kulikuwa na post hapa isemayo 'Ushindi wa JK ni shubiri kwa CCM'. Ambaye anaweza kuipata ai repost tena tafadhali.
 
Pamoja na ukweli kwamba watu kadhoo si wanachama wa CCM, taratibu na mazoea yaliyojengwa na Mfumo wa serikaliya CCM katika maisha yetu ya kila siku umetuathiri kwa kiwango kikubwa sana.
Bado tunatamani kutajirika kwa wizi uuaji uongo na unafiki.
Wako walioingia ndani ya mageuzi kwa sababu wamepanga foleni ya ulaji ndani ya CCM kwa muda mrefu walihisi zamu yao isingeweza kufika hivi karibuni kwa hiyo wameamua kujiunga na upinzani ili kufupisha urefu wa foleni ya ulaji.
Wasicho jua ni hiki. Safari hii ndani ya upinzani kutakuwa kuna kula na kupiga Tindo ili kujenga kesho na keshokutwa. Kujilimbikizia mali kutategemeana na nguvu ya kubuni mikakati ya kuzarisha zaidi na si ufisadi

Kuendelea kuongelea utendaji kwa mtindo wa kiCCM
Ni sawa kabisa na mtu ajiitaye mlokole,aliyekata shauri kumfuta Yesu na kukataa kila aina ya dhambi, kisha kila apitapo demu Bomba na Sketi fupi hukata jicho kali la tamaa kisha kwa unafiki hugeuza shingo yake upande mwingine kujifanya hakuyatamania mapaja yale na baadaye kugeuka na kukodolea mimacho kwa nyuma huku amelegea kwa mtindo wa mbweha aliye likosa windo wazi wazi. Mlokole Mwngine aonapo bango lenye Glass ya Serengeti ikiwa na Jasho la ubaridi hujificha uso wake kwa kiganja kwani moyoni na kooni bado yu atamani radha ya Bia.

Uadilifu siku zote ni aghali sana. Watu waadilifu ni watu wanaojitolea kwa sababu tu wanaamini uadilifu una thamani kuliko maburungutu yote ya fedha, pia wanaamini kwamba uadilifu hujenga jamii yenye utajiri katika kila sekta.

Kwanza jiulize,CHADEMA wakifuata nyayo za CCM kutanguliza fedha mbele tofauti yao na CCM itakuwa nini??
Pili Jiulize, Fedha ya kulipa mawakala wote wa CCM, CCM wameitoa wapi?? Bunge likitaka kujua source za fedha yao wako tayari kuiweka wazi??

Hisia Machale na Pekuapekua yetu inadhihirisha hivi;

CCM wakiingiza mikono yao mirefu, ya KIJITUJITU, katika mifuko ya kaptula zao kutoa fedha, mifuko yao ina mahandaki marefu yanayopitiliza mpaka kwenye Hazina Kuu ya Taifa. Kifupi wanaiba sehemu kubwa ya makusanyo ya kodi ya wananchi wote Tanzania kufinance shughuli binafsi za Chama chao bila ridhaa ya Watanzania na pia kwenda kinyume na sheria ya vyama juu ya fedha.
 
Kudos Aeka Mangi.

The issue of money for service to your party is the CCM way. I dont think we should go the same way to build CHADEMA, CUF, or any other political party in that matter. This will set a bad precedent that money is the issue. I believe that the ideology and the urge to serve is the building block for a strong and cohesive party. Members will have to understand that party politics is not about individuals gains but community service whose dividends have public interests. Tusianze mambo ya wajumbe wa kikao kujilipa madonge manono kuliko manufaa ya kikao chenyewe.

It will be hard to a society and leadership used to benefit from these clandestine payments, however, we need to be principled otherwise five to 10 years to come, we will find ourselves in the CCM mess today!!!

Ni kweli tunahitaji watu wanaojitolea zaidi ya kulipwa pesa. Hapa Marekani wanaolipwa ni wafanyakazi wa ndani ya kampeni na ndio gharama za uchaguzi huhesabika. Lakini kiukweli kazi kubwa inafanywa na wanaojitolea ambao hata mgombea hataweza kuwafahamu. Hivyo ni jukumu la Chadema kujenga vikundi vya wajitoleao ili kuweza kujenga chama madhubuti cha kila mtaa, kitongoji, kijiji, mkoa na Taifa. Historia ya nchi yetu katu kamwe haitakuwa kama ya miaka 25 iliyopita.
 
Kudos Aeka Mangi.

The issue of money for service to your party is the CCM way. I dont think we should go the same way to build CHADEMA, CUF, or any other political party in that matter. This will set a bad precedent that money is the issue. I believe that the ideology and the urge to serve is the building block for a strong and cohesive party. Members will have to understand that party politics is not about individuals gains but community service whose dividends have public interests. Tusianze mambo ya wajumbe wa kikao kujilipa madonge manono kuliko manufaa ya kikao chenyewe.

It will be hard to a society and leadership used to benefit from these clandestine payments, however, we need to be principled otherwise five to 10 years to come, we will find ourselves in the CCM mess today!!!

Can not agree more ..............
 
Kwa vituo takribani 52, 000 Chadema ilipaswa kutumia bilioni tatu kuwalipa mawakala kwa vituo vyote nchi nzima na kwa shilingi elfu hamsini kwa kila wakala.................kwa kutofanya hivyo na kuwategemea wagombea udiwani na ubunge kuwagharimia mawakala ulikuwa ni mkono wa birika ambao sasa machungu yake wote tunayaona..........

Pale ambapo NEC iliyoteuliwa na CCM ilipoamua kutowalipa mawakala Chadema ilipaswa kushtuka kuwa ni mkakati mzito wa CCM wa kuwarubuni mawakala kusaini matokeo ambayo yawezekana siyo sahihi....................Taarifa nilizonazo Chadema wanadai wanazo takwimu ambazo zaonyesha Dr. Slaa kashinda Uraisi.....kama hizo taarifa ni kweli basi mkakati wao ulikuwa ni sahihi.............lakini kama siyo ni kweli basi kurudia kuhesabu kura katika chaguzi zote zenye utata ni jambo la muhimu kwa minajili ya kuwatoa hofu wapigakura kama kweli sauti yao haikudhulumiwa na ufisadi wa CCM...........................

Hili ni la muhimu hata kwa CCM yenyewe katika kuweza kupata uhalali wa kuongoza nchi bila ya zengwe na mashaka kuwa ni dhuluma tu ndiyo inawaweka madarakani..........na aliyeingia madarakani kwa dhuluma ataendeleza dhuluma kubaki madarakani na katika kuwatumikia raia....

Huko tuendako Chadema iwe na mkakati wa kuweka fungu mapema la kuwalipa mawakala nchi nzima kuondokana na wasi wasi kuwa mawakala wana ukata mkubwa kiasi kuwa waweza kununuliwa........uwakala ni kazi yenye kustahili kuheshimiwa kwa malipo pamoja na kuwepo punje punje za kujitolea................


hizo bilioni TATU CHADEMA kingezizaa wapi ......mkuu kama sio ndoto !!! ni pesa nyingi hizo....CHADEMA Walitegemea mawakala wengi wakiwa ni wanafunzi wa vyuo vikuu waliojitolea ....baadhi kwa mapenzi tu tena bila senti....CCM iliwalipa kila wakala wao laki moja!!

kama sio mawakala wa chadema hata hivyo viti 30 walivyopata wasingepata..watu jifunzeni kuwa na shukrani kwa walio jitolea...chukulia mtu kama sugu ....alikuwa na pesa gani ya kumlipa mawakala kumshinda mpesya.....vijana wamejitolea tu!
 
Kwa vituo takribani 52, 000 Chadema ilipaswa kutumia bilioni tatu kuwalipa mawakala kwa vituo vyote nchi nzima na kwa shilingi elfu hamsini kwa kila wakala.................kwa kutofanya hivyo na kuwategemea wagombea udiwani na ubunge kuwagharimia mawakala ulikuwa ni mkono wa birika ambao sasa machungu yake wote tunayaona..........

Pale ambapo NEC iliyoteuliwa na CCM ilipoamua kutowalipa mawakala Chadema ilipaswa kushtuka kuwa ni mkakati mzito wa CCM wa kuwarubuni mawakala kusaini matokeo ambayo yawezekana siyo sahihi....................Taarifa nilizonazo Chadema wanadai wanazo takwimu ambazo zaonyesha Dr. Slaa kashinda Uraisi.....kama hizo taarifa ni kweli basi mkakati wao ulikuwa ni sahihi.............lakini kama siyo ni kweli basi kurudia kuhesabu kura katika chaguzi zote zenye utata ni jambo la muhimu kwa minajili ya kuwatoa hofu wapigakura kama kweli sauti yao haikudhulumiwa na ufisadi wa CCM...........................

Hili ni la muhimu hata kwa CCM yenyewe katika kuweza kupata uhalali wa kuongoza nchi bila ya zengwe na mashaka kuwa ni dhuluma tu ndiyo inawaweka madarakani..........na aliyeingia madarakani kwa dhuluma ataendeleza dhuluma kubaki madarakani na katika kuwatumikia raia....

Huko tuendako Chadema iwe na mkakati wa kuweka fungu mapema la kuwalipa mawakala nchi nzima kuondokana na wasi wasi kuwa mawakala wana ukata mkubwa kiasi kuwa waweza kununuliwa........uwakala ni kazi yenye kustahili kuheshimiwa kwa malipo pamoja na kuwepo punje punje za kujitolea................

Smell like CCM shit ............ kama ni kujitafutia kipato basi CHADEMA ingeshindwa kote, kwa kuanzia ingekuwa Arusha ambako EL alitaka
kupenyeza rupia lakini ikakataliwa ............
 
i am with u pal. Pesa si zaidi ya uhuru wa nchi hii....!!!! Mimi ni kijana, nimeshakata tamaa na nchi hii, but am not giving up yet....CCM ni wizi wizi mtupu//!!!!
 
Suala la ukombozi especially kwetu sisi watanzania hatuhitaji kulipwa. This is for the sake of our next generation. Sihitaji hata senti moja for CHADEMA or chama kingine chenye mwelekeo wa kumpunguzia mtanzania mizigo na ukali wa maisha. Ndiyo maana hapo awali wakati wa kampeni nilitoa mchango wangu katika kuhakikisha tunamuumbua aliyekuwa anasambaza SMS za kumchafua Dr. Slaa. Sikuomba pesa wala udiwani na ninajivunia kwa kile nilichokifanya. Hata usalama wa Taifa wanaelewa hilo upinzani nao wana wataalamu wazuri wa IT lakini wapenda AMANI kuliko hao akina Miraji na genge lake.
 
hizo bilioni TATU CHADEMA kingezizaa wapi ......mkuu kama sio ndoto !!! ni pesa nyingi hizo....CHADEMA Walitegemea mawakala wengi wakiwa ni wanafunzi wa vyuo vikuu waliojitolea ....baadhi kwa mapenzi tu tena bila senti....CCM iliwalipa kila wakala wao laki moja!!

kama sio mawakala wa chadema hata hivyo viti 30 walivyopata wasingepata..watu jifunzeni kuwa na shukrani kwa walio jitolea...chukulia mtu kama sugu ....alikuwa na pesa gani ya kumlipa mawakala kumshinda mpesya.....vijana wamejitolea tu!
Mkuu umegonga penyewe.

"Mkono wa birika umeigharimu Chadema chaguzi hii" unaamanisha chadema walikuwa na pesa wakakataa kuzitumia,sasa wewe tueleze chadema wanakiasi gani wakabania kuzitumia kwenye uchaguzi, kwa sababu mimi ninavyojua chadema ilikuwa na hali mbaya kifedha ndio maana wakaomba watu wachangie katika ya kampeni.

Inabidi tukubaliane na hali ilivyokuwa,kwenye fedha tusiwalaumu chadema kabisa.Chadema hawawezi kujilinganisha na ccm,hatujui hizo pesa wanachota wapi. Hata kama Chadema ingeweza kuwalipa mawakala wake kila mmoja laki, ccm ingeweza kuongeza kuwalipa mawakala wake laki tano iliwaweze kuwarubuni wa upinzani na bado tungelalamika kwanini Chadema wamewalipa mawakala wake pesa kidogo.Mimi naona uwakala bado ibakie ni kitu cha kujitolea.
 
Kama ingekua kwa sababu ya pesa wala tusingepoteza muda wetu huku. Huu ushenzi wa kudai posho Tena umeanzia serikalini hasa wakati wa mkapa. Idara nyingi za serikalini zilipata mafungu wakawa wanashindwa lkuzitumia ipasavyo ndio watu wakaanza kujilipa mara imtindo ukasambaa, ilhali watu mishahara wanapewa. Ugonjwa na tabia hii ukijumlisha na umaskini wa watu ukashika kasi mpaka vijijini. Maendeleo ni pamoja na siasa safi, Kama mchonga alivyoiweka huko zamani.
 
Kwa vituo takribani 52, 000 Chadema ilipaswa kutumia bilioni tatu kuwalipa mawakala kwa vituo vyote nchi nzima na kwa shilingi elfu hamsini kwa kila wakala.................kwa kutofanya hivyo na kuwategemea wagombea udiwani na ubunge kuwagharimia mawakala ulikuwa ni mkono wa birika ambao sasa machungu yake wote tunayaona..........

Pale ambapo NEC iliyoteuliwa na CCM ilipoamua kutowalipa mawakala Chadema ilipaswa kushtuka kuwa ni mkakati mzito wa CCM wa kuwarubuni mawakala kusaini matokeo ambayo yawezekana siyo sahihi....................Taarifa nilizonazo Chadema wanadai wanazo takwimu ambazo zaonyesha Dr. Slaa kashinda Uraisi.....kama hizo taarifa ni kweli basi mkakati wao ulikuwa ni sahihi.............lakini kama siyo ni kweli basi kurudia kuhesabu kura katika chaguzi zote zenye utata ni jambo la muhimu kwa minajili ya kuwatoa hofu wapigakura kama kweli sauti yao haikudhulumiwa na ufisadi wa CCM...........................

Hili ni la muhimu hata kwa CCM yenyewe katika kuweza kupata uhalali wa kuongoza nchi bila ya zengwe na mashaka kuwa ni dhuluma tu ndiyo inawaweka madarakani..........na aliyeingia madarakani kwa dhuluma ataendeleza dhuluma kubaki madarakani na katika kuwatumikia raia....

Huko tuendako Chadema iwe na mkakati wa kuweka fungu mapema la kuwalipa mawakala nchi nzima kuondokana na wasi wasi kuwa mawakala wana ukata mkubwa kiasi kuwa waweza kununuliwa........uwakala ni kazi yenye kustahili kuheshimiwa kwa malipo pamoja na kuwepo punje punje za kujitolea................

Nasikia harufu ya "michango" mingi halafu watu kula kona! Hivi zile hela zote za ma-Conservatives wa Uingereza mlizopewa zimetumika wapi vile?
 
Du! mlisha anza kuleta habari za vijiweni hapa, sioni kama kuna ukweli wowote kuhusiana na hilo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom