Mkojo wa mjamzito: Biashara nyingine ya siri isiyojulikana na wengi

Nitengenezee kwakweli nahitaji, nimechoka kuishi uswazi. Masharti ni kulamba tu?
Yasije kua na ya kwenda makaburini usiku wa manane
Wala hatuendi makaburini, tunaenda tu bandani kwa Kaka sungura, Kisha tunahamia chumbani, tukitoka huko tayari una tumbo kubwa Kama mkurugenzi wa bandari

NB:-
Mshana Jr naomba umpe Lenie ramani ya ofisini kwangu
 
Mji mzito sana huu
Kuna mambo yanaendelea kimyakimya na chini kwa chini huku baadhi wakibaki na vucheko baada ya kupiga pesa ya mabwege na huku wengine wakibaki na majuto na kujiapiza kutorudia tena...

Baadhi ya wanaume wenye macho juu Wamepigwa sana kwenye hili jambo.. Naamini hata kati ya wasomaji watakaosoma hii mada ni wahanga wa hili jambo...
Ujumbe wa BABY NINA MIMBA YAKO.. huwachanganya sana mabazazi na wale wanaojiita mabaharia bila kuwasahau wazee wa mjini... Wazee wa bandari... Unapopata ujumbe kama huu toka kwa mchepuko wako ambaye anaweza kuwa mke wa mtu bandia au halisi, mwanafunzi (halisi au bandia) danga nk unachanganyikiwa kabisa.. Cha kwanza kuwaza ni mkewako nyumbani... Mpenzi wako... Kazi yako ama maisha yako....

Kuna wanawake siku hizi hii ndio biashara yao kubwa na inawalipa vizuri tuu.. Unakutana na binti au mdada mzuri kweli unatupa nyavu zinanasa kimaskhara kabisa lakini unapewa onyo mapema... Mimi ni mwanafunzi au mimi nina mtu wangu au mimi ni mke wa mtu.... Bila kutafakari hilo onyo unasema utafanya siri.. Unakubaliwa unakula mzigo kiboya kabisa

Bila kujijua kuwa uko kwenye foleni ndefu ya kubambikiwa ujauzito feki mwanaume kidume wewe unajiachia kwa raha zako.. Ukimhitaji mtoto unampata unakula anasepa. Na anaweza kabisa awe hakusumbui kwa shida ndogo ndogo.... Usijione mjanja ukadhani umepata... Tambua tu umepatikana

Siku yako ya kupigwa ikifika unapata ujumbe mbaya wa ujauzito na unaambiwa wazi kabisa kuwa hayuko tayari kuzaa kwa wakati huo... Kwahiyo mzee inabidi udhamini mchezo... Na ili kukuaminisha mnaenda wote hospital kupima.. Kumbe tayari mwenzako ana kichupa chake cha mkojo wa mtu mwingine kabisa mwenye ujauzito amekificha kwenye chupi yake

Ni wazi hutamsindikiza mpaka chooni hata akikuomba.. Sana sana utaishia mlangoni.. Yeye huko ndani atabadili tu mkojo toka kichupa alichokuja nacho kwenda alichopewa hospital... Majibu yakitoka... Imooo.. ...
Kifuatacho ni gharama za kutoa mimba tena anachagua Marie Stopes.. Ukikomaa kwenda naye mpaka daktari atapangwa...
Baada ya hapo unahudumia 'mgonjwa' na akipona unapigwa chini.. Mchezo unaendelea kwa maboya wengine....

Wanaonunua mikojo ya waja wazito wengi wao sio kwa ajili ya ushirikina bali kwa ajili ya kuwapiga mabazazi... Najua umesoma huku ukikumbuka pesa ulizotoa kwa ajili ya abortion huku ukijisifu kwa wanaume mwenzako kuwa una mbegu Kali sana.. Ukigusa tu kitu na box... unaibiwaaa...Boya WEWE

Kuna mmoja alikutana na bandidu kiboko.

Ilikuwa hivi alisema anamimba na ikaonekana amedhamilia yule jamaa akasema niletee majibu akaleta yakisoma jina lake. Hakujua kuwa jamaa alishalizwa . Akachukua lodge akaenda kununua vidonge na kumwambia ameze mbele yake na vingine aweke kwenye ikulu dada akabadilika mara oh nitameza nyumbani mara oh nina aleji ya vidonge mara oh . Jamaa akasema usirudie akamtimua ikawa ndio mwisho.

Na vile vidonge alivyonunua ilikuwa panadol tu ili ajiridhishe
 
Kuna mmoja alikutana na bandidu kiboko.

Ilikuwa hivi alisema anamimba na ikaonekana amedhamilia yule jamaa akasema niletee majibu akaleta yakisoma jina lake. Hakujua kuwa jamaa alishalizwa . Akachukua lodge akaenda kununua vidonge na kumwambia ameze mbele yake na vingine aweke kwenye ikulu dada akabadilika mara oh nitameza nyumbani mara oh nina aleji ya vidonge mara oh . Jamaa akasema usirudie akamtimua ikawa ndio mwisho.

Na vile vidonge alivyonunua ilikuwa panadol tu ili ajiridhishe
kupotea njia ni wakati wa kwenda tuu
 
Kuna mmoja alikutana na bandidu kiboko.

Ilikuwa hivi alisema anamimba na ikaonekana amedhamilia yule jamaa akasema niletee majibu akaleta yakisoma jina lake. Hakujua kuwa jamaa alishalizwa . Akachukua lodge akaenda kununua vidonge na kumwambia ameze mbele yake na vingine aweke kwenye ikulu dada akabadilika mara oh nitameza nyumbani mara oh nina aleji ya vidonge mara oh . Jamaa akasema usirudie akamtimua ikawa ndio mwisho.

Na vile vidonge alivyonunua ilikuwa panadol tu ili ajiridhishe
😂😂😂😂😂 Itakua jamaa alishawahi kufanyiwa utapeli ndo maana akawa mjanja. Hapo mdada unaondoka na aibu ya hatari
 
Kweli nikupe ongera kwa kufikiria na kupata hili na kupost pia.
Ulichopost kina ukweli ndani yake wako wengi wakina mama wa aina hiyo ya kihuni.
Wako na wengine mimba moja baba wa mimba hiyo wako (10) na wote wanaitumikia hiyo mimba na wajuani na kadi za clinic ya mimba zina kuwepo idadi hiyo kila anaetaka aone kadi hupewa ilioandikwa jina lake.
Na vituo vya huduma viko sawa na idadi ya baba wa hiyo mimba hapo upo?
 
Back
Top Bottom