Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,864
- 155,820
MWENYEKITI wa Kijiji cha Kemakorere, Zephania Chacha anadaiwa kumshambulia kwa viboko mkuu msaidizi wa Shule ya Sekondari Kemakorere, Juma Selemani Hango akimtuhumu kukata miti miwili ya shule hiyo.
Chacha ameshafikishwa kituo cha polisi kilicho kwenye Kata ya Nyarero wilayani Tarime na anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote kujibu shtaka la kushambulia kwa fimbo na kumsababishia mwalimu huyo maumivu makali.
Tukio hilo ni mwendelezo wa vipigo dhidi ya walimu ambavyo vilianza kusikika baada ya mkuu wa wilaya ya Bukoba, Albert Mnali kuamuru polisi wa kijeshi kuwatandika viboko walimu wa shule tatu kwa madai kuwa ni watoro kazini.
Lakini katika tukio la mkoani Mara, mwenyekiti huyo wa kijiji alichukua hatua hiyo baada ya kupata habari kuwa mkuu huyo msaidizi wa shule alikuwa akikata miti kwenye shamba la shule kwa ajili ya kutengenezea mlango wa choo.
Mkuu wa makosa ya jinai wa Tarime/Rorya, David Hiza alisema kuwa tukio hilo la shambulio hilo dhidi ya Hango lilitokea Julai 5 mwaka huu mchana wakati mwalimu huyo alipokata miti miwili ya shule kwa ajili ya kupasua mbao za kutengenezea mlango wa choo cha shule hiyo.
Hiza alisema kuwa baada ya mwenyekiti huyo kupata taarifa kuwa mwalimu huyo alikuwa akikata miti bila ya ruhusa yake, alienda eneo hilo na kumkuta Mwalimu hango akiendelea na shughuli ya kupasua mbao pamoja na mafundi na ndipo vurugu kubwa ilipozuka.
Alisema katika vurugu hizo, mwenyekiti huyo alichukua fimbo na kuitumia kumshambulia mwalimu huyo na kusababisha apate maumivu sehemu mbalimbali za mwili.
Hiza alisema baadaye mwalimu huyo alifungua jalada namba NY/IR/392/2010 kwenye kituo cha polisi cha Nyamwaga na kwamba mwenyekiti huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote ule.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kemakorere, Phafin Boroye alisema kuwa uongozi na kamati ya shule hiyo umesikitishwa na kitendo hicho cha mwenyekiti huyo wa kijiji kwa kumshambulia mwalimu wao.
Alisema kuwa miti hiyo ilikuwa kwa ajili ya kupasulia mbao ambazo zingetumika kutengenezea milango ya choo cha shule na kwamba mwalimu huyo hakuwa na nia mbaya kuikata.
Alisema angelipeleka suala hilo kwenye kamati ya shule kama lingekuwa na utata wa ukataji miti hiyo
Chacha ameshafikishwa kituo cha polisi kilicho kwenye Kata ya Nyarero wilayani Tarime na anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote kujibu shtaka la kushambulia kwa fimbo na kumsababishia mwalimu huyo maumivu makali.
Tukio hilo ni mwendelezo wa vipigo dhidi ya walimu ambavyo vilianza kusikika baada ya mkuu wa wilaya ya Bukoba, Albert Mnali kuamuru polisi wa kijeshi kuwatandika viboko walimu wa shule tatu kwa madai kuwa ni watoro kazini.
Lakini katika tukio la mkoani Mara, mwenyekiti huyo wa kijiji alichukua hatua hiyo baada ya kupata habari kuwa mkuu huyo msaidizi wa shule alikuwa akikata miti kwenye shamba la shule kwa ajili ya kutengenezea mlango wa choo.
Mkuu wa makosa ya jinai wa Tarime/Rorya, David Hiza alisema kuwa tukio hilo la shambulio hilo dhidi ya Hango lilitokea Julai 5 mwaka huu mchana wakati mwalimu huyo alipokata miti miwili ya shule kwa ajili ya kupasua mbao za kutengenezea mlango wa choo cha shule hiyo.
Hiza alisema kuwa baada ya mwenyekiti huyo kupata taarifa kuwa mwalimu huyo alikuwa akikata miti bila ya ruhusa yake, alienda eneo hilo na kumkuta Mwalimu hango akiendelea na shughuli ya kupasua mbao pamoja na mafundi na ndipo vurugu kubwa ilipozuka.
Alisema katika vurugu hizo, mwenyekiti huyo alichukua fimbo na kuitumia kumshambulia mwalimu huyo na kusababisha apate maumivu sehemu mbalimbali za mwili.
Hiza alisema baadaye mwalimu huyo alifungua jalada namba NY/IR/392/2010 kwenye kituo cha polisi cha Nyamwaga na kwamba mwenyekiti huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote ule.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kemakorere, Phafin Boroye alisema kuwa uongozi na kamati ya shule hiyo umesikitishwa na kitendo hicho cha mwenyekiti huyo wa kijiji kwa kumshambulia mwalimu wao.
Alisema kuwa miti hiyo ilikuwa kwa ajili ya kupasulia mbao ambazo zingetumika kutengenezea milango ya choo cha shule na kwamba mwalimu huyo hakuwa na nia mbaya kuikata.
Alisema angelipeleka suala hilo kwenye kamati ya shule kama lingekuwa na utata wa ukataji miti hiyo