VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Namshukuru Mungu nimewasili salama hapa Chalinze nikitokea Dodoma. Sasa nipo hapa kata ya Miono utakapofanyika Mkutano wa Ufunguzi wa Watani wetu CHADEMA. Kila mwananchi anamtaja Dr.Slaa,kwani naye atakuja kweli jamani!? Chalinze yazizima.Yawasubiri mje mjionee. Mjionee sera na sura;raha na karaha. Njooni ndugu zangu watanzania.
Kwakuwa si chama changu,sitawawekea kitakachokuwa kikisemwa moja kwa moja.Lakini,nitaleta uchambuzi wangu kama ilivyo ada yangu. Niliulizia kuhusu ufunguzi wetu jana.Kila mtu anailaumu mvua. Siwezi kuwabishia kwakuwa sikuwepo. Nangoja hapa hapa Miono nione yatakayojiri.
Mkimaliza kule Kalenga-Iringa,njooni huku Chalinze-Pwani. Halali mtu hapa kwa siku hizi za kampeni
Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Chalinze)
Kwakuwa si chama changu,sitawawekea kitakachokuwa kikisemwa moja kwa moja.Lakini,nitaleta uchambuzi wangu kama ilivyo ada yangu. Niliulizia kuhusu ufunguzi wetu jana.Kila mtu anailaumu mvua. Siwezi kuwabishia kwakuwa sikuwepo. Nangoja hapa hapa Miono nione yatakayojiri.
Mkimaliza kule Kalenga-Iringa,njooni huku Chalinze-Pwani. Halali mtu hapa kwa siku hizi za kampeni
Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Chalinze)