MkikiMkiki: Uliza swali mdahalo wa vyama vya siasa kuhusu Rushwa na Maadili

Jul 2, 2015
20
23

View attachment 293617

Asilimia 78 ya wananchi wanasema hali ya rushwa imezidi kuwa mbaya kwa miaka kumi, asilimia 30 wakitaka waliochukua pesa kwa mgongo wa rushwa wazirudishe, asilimia 32 wakisema wafukuzwe kazi na wanyimwe pensheni.

Asilimia 92 ya wananchi wanaamini wagombea wanaotoa pesa kipindi cha uchaguzi ni rushwa na asilimia 55 ya wananchi wanasema rushwa ina athari kubwa kwenye maisha yao.

Kwa mara nyingine tena Mdahalo wa Mkikimkiki unawadia na unaweza kuuliza swali lako kwa vyama vya siasa kwenye mdahalo unaohusu Rushwa.

Tarehe: Jumapili October 4, 2015
Muda: 7:00 – 10:00am (Saa saba mchana hadi saa kumi jioni)
Mahali: Ukumbi wa Julius Nyerere International Conference Centre (JNICC) – Posta

Midahalo hii inalenga kuvipa vyama vyote fursa ya kunadi Ilani zao na kwa wananchi kuuliza maswali muhimu yatakayo pelekea maamuzi yao katika uchaguzi. Vyama vinavyoshiriki ni vile vyenye wagombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Zanzibar na wagombea Ubunge angalau majimbo 65.

Midahalo hii itakuwa live hapa jukwaani kwa ushirikiano na JamiiForums na Fikra pevu. Pia Midahalo hii itarushwa moja kwa moja na Star TV na Redio RFA. Vyombo vya habari vinakaribishwa kushiriki lakini lazima wajiandikishe kabla ili kufanya hivyo.

Kupata nafasi ya swali lako kuulizwa kwenye mdahalo, uliza swali lako hapa jukwaani kwenye mada(Thread) hii.

Kama unapenda kuwa mmoja wa watazamaji ukumbini tuma neno KUSHIRIKI acha nafasi tuma jina na kazi yako kwenda 15678.

Utatozwa bei ya kawaida ya ujumbe wa simu (SMS). Hakuna gharama ya ziada.
 
Rushwa ndio chanzo cha kikubwa cha udhaifu unaotokea kwenye serikali, watendaji hawatendi majukumu yao kusikilizia rushwa, maamuzi mazuri yanapinduliwa na rushwa. Vyama vya upinzani wana mkakati gani kuzuia rushwa iliyoshamiri hasa kwenye maamuzi makubwa yanayohujumu maisha na uchumi wetu?
 
Rushwa ndio chanzo cha kikubwa cha udhaifu unaotokea kwenye serikali, watendaji hawatendi majukumu yao kusikilizia rushwa, maamuzi mazuri yanapinduliwa na rushwa. Vyama vya upinzani wana mkakati gani kuzuia rushwa iliyoshamiri hasa kwenye maamuzi makubwa yanayohujumu maisha na uchumi wetu?


Rushwa itaisha kama itaweza kuzuiliwa kwenye ngazi ya UCHAGUZI,ukishaweza kuzuia hapo huku kwingine ni rahisi sana kuzuia.

Tunahitaji IDARA ya kupambana na rushwa kwenye TUME yetu ya UCHAGUZI na mtu anayepokea na kutoa rushwa wote wawili wanatakiwa kuadabishwa.Mpokeaji kutoruhusiwa kupiga KURA na MTOAJI kufutwa kabisa kwenye KUGOMBEA nafasi zozote maisha,yaani asiteuliwe tena na vyama na kama chama kikimteua basi akatwe juu kwa juu na TUME,hii itaondoa RUSHWA kwenye UCHAGUZI.

Sababu kubwa ni kwamba hawa wanaochaguliwa ndiyo wawakilishi wetu ndani ya Bunge na kwenye manispaa,tukipata watu walioingia kwa uadilifu ndani ya Bunge (Wabunge na Madiwani) basi kwa kiasi kikubwa tutakuwa tumepiga hatua kubwa ya kuzuia RUSHWA
 
Maswali yangu ni mawili;

1. Chama Tawala kimekua na tuhuma kubwa ya rushwa kipindi hiki cha uchaguzi, baadhi ya wagombea walionekana wakitoa rushwa ili waweze kuchaguliwa katika uchaguzi huu. Je, Chama tawala watawezaje kumaliza tatizo la rushwa na wakati wao wenyewe wamekua
wakitoa rushwa ?

2. Mgombea anayegombea urais chama pinzani alituhumiwa na kashfa ya kuchukua pesa Richmond, kwa kupitia mchakato mzima wa Richmond rushwa imepita sana mpaka kufanikisha, Je atawezaje kumaliza tatizo la rushwa wakati yeye mwenyewe kama kiongozi wakati ule alishindwa kuzuia rushwa?
 
Ni kwa namna gani wanaotafuta dhamana ya uongozi kwetu wataweza kukomesha rushwa katika kila ngazi? Si rahisi kwasababu kuna vitu vidogo ambavyo vinaweza vikamfanya mtu aamue tu kutoa pesa na kuendelea na mambo yake.

Mfano: Ukikamatwa na polisi barabarani na ukaona kabisa anakulazimishia kosa na una haraka, utaamua tu kumuachia hela ili uondoke, cases kama hizi zipo nyingi sana. Sasa watakabiliana nayo vipi ili kuitokomeza?
 
kwa media hii mnayoitumia nyie ndo walewale wa TWAWEZA hi kampuni ya Sahara Media haina maadili ya kihabari imelalia upande wa chama tawala hivyo nahisi hata maswali ya kuibana ccm hayatoruhusiwa
 
Kama Rushwa iko kwa kiwango hicho kinachoonekana, Polisi, Siasa, TRA, Ardhi, Huduma za Afya, Elimu na Serikali za Mitaa, Swali: CCM ambao ndio chama tawala, wanaweza kutwambia ni wapi wameshindwa au kwanini waliruhusu hiyo hali kuwa hivyo? na leo wanataka tuwachague ni nini watafanya ili kuzuia hiyo hali ile hali wapo madarakani kwa zaidi ya miaka 50 na wameshindwa kukomesha Rushwa?

Wapinzani sii kesi kubwa ila tunataka mtwambie, mtafanya kitu gani kupambana na Rushwa ambacho mmeona CCM wameshindwa kukifanya?
 
Swali kwa wagombea ufisadi umeonekana kua ni kikwanzo kikubwa kwa taifa letu je wamejipanga vipi kuwashugulikia mafisadi walio chukua pesa na kuzibiti isitoke tena ufisadi mwingine
 
Kutokana na jedwali hapo juu, linaonesha rushwa ipo kwa kiasi kikubwa kila idara. SWALI: Je tumefikaje hapo?
 
Ila ninawashangaa wanachi wanaopokea RUSHWA kutoka kwa wagombea halafu wanawapigia KURA baada ya muda hawaishi kulalamika.

Kumaliza RUSHWA ya UCHAGUZI ni kutokupokea HONGO,na kama UKIPOKEA basi KUWA na moyo MGUMU wa kutompa KURA anayetoa RUSHWA.
 
Maswali:

Je ni kweli kwamba Rushwa imeshindikana kuizuia au kuikomesha kabisa kuanzia chini mpaka imefikia mahali hata vyombo vya dola wanashindwa kuidhibiti?

Inawezekana wanasiasa hasa chama tawala ndio wanaoikuza Rushwa, na hivyo kushamiri kwa kiasi kikubwa kwetu?
 
Hakuna Jipya Hapo, Waandaji TWAWEZA Na Wanaorusha Ni STARTVCCM!! Ndorooobai!! WATANZANIA Tunajua WATU Wakaokuja Kupambana Na HAYO Yote!! Hatuhitaji Midahalo Nao!
 
Hakuna Jipya Hapo, Waandaji TWAWEZA Na Wanaorusha Ni STARTVCCM!! Ndorooobai!! WATANZANIA Tunajua WATU Wakaokuja Kupambana Na HAYO Yote!! Hatuhitaji Midahalo Nao!

Wapuuzi kweli kweli. Wanafikiri watanzania ni wale wa miaka ya 1980s
 
Rushwa wahusika wake ni hawa.Mwananchi,Poli ce,Hospitali,Mahakamani,Idara za kazi, wote hawa ni wahusika wakuu wa rushwa sasa nani atamaliza rushwa wakati sisi wenyewe ndo watoaji na wapokeaji?
 
Mfumo Huu Wa Rushwa Nchini Kwetu,umetokana Na Sisi Wenyewe Wananchi Kupenda Kupata Vitu Kwa Njia Ya Mkato Mkato,kirahisi Rahisi Na Wengi Wetu Wabinafsi...Watanzania Wenyewe Tunajirahisisha Kwa Vitu Ambavyo Tukisimama Kwa Umoja Wetu Tunaweza Kuvipata.Watanzania Leo Hii Wengi Hatupendi Kufuata Sheria Weng Tunapenda Kupita Uchochoroni Je,kwa Hali Hii Kweli Rushwa Itakoma?Swala La Rushwa Wa Kwanza Kuliua Na Kulimaliza Ni Sisi Wenye Watz Kubadili Tabia Zetu....
 
Back
Top Bottom