Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,587
- 215,184
Umekutana na binti mjini Dar, binti huyu wazazi wake ni wanasiasa tangu enzi za chama kushika hatamu. Wana eneo la heka tano na zimezungushiwa uzio.
Mapenzi yenu yameiva mpaka mnaona. Siku ya harusi mbele ya wageni Baba mkwe kwenye hotuba yake anawapa kiwanja ndani ya eneo lake, kwa tambo anasema wajukuu zake wasizaliwe kwenye nyumba ya kupanga.
Baada ya honeymoon mmepewa guest wing muanzie maisha wakati mnajenga. Mmejenga nyumba imekwisha na mmehamia.
Mmekorofishana kidogo na mke, hali halisi ni kuwa wote mna hasira mmoja wenu inabidi aondoke kwa muda. Kati ya wewe na mke wako ataondoka nani?
Mapenzi yenu yameiva mpaka mnaona. Siku ya harusi mbele ya wageni Baba mkwe kwenye hotuba yake anawapa kiwanja ndani ya eneo lake, kwa tambo anasema wajukuu zake wasizaliwe kwenye nyumba ya kupanga.
Baada ya honeymoon mmepewa guest wing muanzie maisha wakati mnajenga. Mmejenga nyumba imekwisha na mmehamia.
Mmekorofishana kidogo na mke, hali halisi ni kuwa wote mna hasira mmoja wenu inabidi aondoke kwa muda. Kati ya wewe na mke wako ataondoka nani?