WomanOfSubstance
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 5,458
- 956
Katika suala zima la kupambana na UKIMWI, kitu ambacho kimeendelea kuleta utata na mtafaruku mkubwa katika familia, ndoa na mahusiano mengi ni suala la kupima na kujua hali ya mhusika kama amepata maambukizi ama lah!
Tatizo linalowapata wanawake wengi ni kuwashawishi wanaume kupima virusi. Wanawake wajawazito hujikuta "wakilazimika" kupima ili kuwakinga watoto walio matumboni mwao na virusi wakati wa kujifungua au wakati wa kunyonyesha. Wapo pia wale wenye kutaka kujua hali zao ili waishi kwa matumaini ikiwa ni pamoja na kujikinga na maambukizi mapya. Tatizo linakuja: mwanamke akipima akagundulika ana virusi, basi kumetokea vurugu na fujo za kila aina na lawama kwamba kwanini kaenda kupima.Ina maana kuishi maisha ya kubabaisha na kuficha kichwa mchangani kama mbuni ndio njia iliyo bora zaidi?
je,
1. Kwanini wanaume wengi hawataki kupima na kujua afya zao ( majority wanajua kabisa kuwa wanaishi maisha hatarishi ( risky life styles)
2.Mbinu gani zitumike kuwashawishi wanaume wasiotaka kujua afya zao kupima kwa hiari?
Tatizo linalowapata wanawake wengi ni kuwashawishi wanaume kupima virusi. Wanawake wajawazito hujikuta "wakilazimika" kupima ili kuwakinga watoto walio matumboni mwao na virusi wakati wa kujifungua au wakati wa kunyonyesha. Wapo pia wale wenye kutaka kujua hali zao ili waishi kwa matumaini ikiwa ni pamoja na kujikinga na maambukizi mapya. Tatizo linakuja: mwanamke akipima akagundulika ana virusi, basi kumetokea vurugu na fujo za kila aina na lawama kwamba kwanini kaenda kupima.Ina maana kuishi maisha ya kubabaisha na kuficha kichwa mchangani kama mbuni ndio njia iliyo bora zaidi?
je,
1. Kwanini wanaume wengi hawataki kupima na kujua afya zao ( majority wanajua kabisa kuwa wanaishi maisha hatarishi ( risky life styles)
2.Mbinu gani zitumike kuwashawishi wanaume wasiotaka kujua afya zao kupima kwa hiari?