nasikia ametumiwa kitu akiwa bafuni na akina Akilimali
...........................................................Mkurugenzi wa Ufundi wa klabu ya Yanga, Patrick Naggi ameacha kazi akidai ni kutokana na ubabaishaji wa viongozi wa klabu hiyo.
Naggi ambaye ni Mkenya amefikia uamuzi huo hivi karibuni baada ya kukaa muda mrefu bila ya kusaini mkataba wowote wa kuitumikia klabu hiyo tangu alipotua hapa nchini Septemba mwaka huu kwa ajili ya kuwa Katibu Mkuu wa klabu hiyo.
Hata hivyo, hakuweza kupewa cheo hicho baada ya kuzuka kwa malumbano kati ya viongozi na baadhi ya wanachama wa klabu hiyo ambao hawakutaka apewe nafasi hiyo ya Katibu Mkuu ambayo inakaimiwa na Lawrence Mwalusako.
Kutokana na hali hiyo uongozi wa Yanga ulimteua kuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa klabu kazi ambayo ameifanya kwa muda wa miezi mitatu bila ya kuwa na mkataba wa aina yoyote ...
analetwa Mganda
Aaah Mkuu, sasa ina maana wa-TZ hatujui kazi au? Au ndiyo mambo ya EAC soko la pamoja?