miles45
JF-Expert Member
- Jan 4, 2019
- 3,466
- 8,281
Ilikua ni siku tulivu tu Kama siku nyingine, basi shetani nae alikua kazini Kama kawaida yake.
Kifupi mke wangu huyu hana tabia kabisa ya kushika simu yangu hadi majuzi alipo ingiwa na tamaa za kutaka kujua Kama yaliyomo yamo.
Basi ni siku moja nyuma yake nilikua nimefanya muamala wa pesa kwa mwanadada Beatrice kulipia bidhaa alio niuzia. Baada ya kulipia nikamtumia text kumuuliza Kama kapata? Akanijibu ndio nimepata Asante. Nami nikamjibu Asante pia kwa kunivumilia Basi maongezi yakawa yameishia hapo na huyu Beatrice.
Basi hiyo siku nipo zangu bafuni naoga nasikia wife anabamiza bamiza milango mala atoke mala aingie ile kumaliza kuoga natoka namkuta mtu amefura hatari Mara ashike hichi aache, ashike hichi aache akaenda kushukua dekio kalileta ndani akaacha akachukua mswaki akatoka nje , akarudi kumbe kasau kuweka dawa akarudi akaweka dawa akaanza kupangalua mabegi Kama Kuna kitu anakitafuta hivi aah mimi kuoana hivyo nikamuuliza kulikoni mbona hivyo nikajibiwa kamuulize Beatrice. Nikaanza kujiuliza kwani Beatrice kafanya Nini? Mtoto wa watu akaangua kilio hatari huku akisema yaani tunafuta hela kwa shida hivi halafu wewe unahonga kirahisi hivyo. Na kwa unaomba na samahani kabisa kwa kumcheleweshea .
Kufikia hapo nikakosa sababu ya kuendelea kuongea nae na kubaki tu nacheka maana hata sijui pa kuanzia kumuelewesha kwa sababu hata simu yangu nilisha kataza kuushika , anacho nifikiria kufanya sijafanya. Na kiukweli Mimi Bwana kujieleza sipendi hasa kwa kiumbe wa kike. Na Mambo hayapo sawa Hadi leo Moto umewaka mtu Hana amani kabisa, yaani nisifanye chochote naambiwa Beatrice kwa hiyo humu ndani wimbo ni Beatrice. Aman huyu Dada angejua jina lake limeleta balaa kwenye familia yangu sijui angejisikiaje Dada wa watu. Sijui angeacha hii kazi yake ya kuuza bidhaa zake kwa mkopo na kutumiwa hela kwa simu sijui.
Sijui nimfokee huyu wife kwa Nini alishika simu? Sijui nikae chini nianze kumueleza Hali ilivyo hapa naona uvivu na akili inachoka kabisa.Yaani ni lawama tu kuwa aliniamini Sana na hakujua Kama Kuna siku nitamfanyia hayaa. Na hata nikimuelezea ataona Kama nampanga tu cos majibu tayari anayo.
Nimesha amua bana liwalo na liwe. Wacha Moto uwake ukimaliza utazima wenyewe.
NB
......... wanawake achaneni na simu za wanaume wenu .......
Kifupi mke wangu huyu hana tabia kabisa ya kushika simu yangu hadi majuzi alipo ingiwa na tamaa za kutaka kujua Kama yaliyomo yamo.
Basi ni siku moja nyuma yake nilikua nimefanya muamala wa pesa kwa mwanadada Beatrice kulipia bidhaa alio niuzia. Baada ya kulipia nikamtumia text kumuuliza Kama kapata? Akanijibu ndio nimepata Asante. Nami nikamjibu Asante pia kwa kunivumilia Basi maongezi yakawa yameishia hapo na huyu Beatrice.
Basi hiyo siku nipo zangu bafuni naoga nasikia wife anabamiza bamiza milango mala atoke mala aingie ile kumaliza kuoga natoka namkuta mtu amefura hatari Mara ashike hichi aache, ashike hichi aache akaenda kushukua dekio kalileta ndani akaacha akachukua mswaki akatoka nje , akarudi kumbe kasau kuweka dawa akarudi akaweka dawa akaanza kupangalua mabegi Kama Kuna kitu anakitafuta hivi aah mimi kuoana hivyo nikamuuliza kulikoni mbona hivyo nikajibiwa kamuulize Beatrice. Nikaanza kujiuliza kwani Beatrice kafanya Nini? Mtoto wa watu akaangua kilio hatari huku akisema yaani tunafuta hela kwa shida hivi halafu wewe unahonga kirahisi hivyo. Na kwa unaomba na samahani kabisa kwa kumcheleweshea .
Kufikia hapo nikakosa sababu ya kuendelea kuongea nae na kubaki tu nacheka maana hata sijui pa kuanzia kumuelewesha kwa sababu hata simu yangu nilisha kataza kuushika , anacho nifikiria kufanya sijafanya. Na kiukweli Mimi Bwana kujieleza sipendi hasa kwa kiumbe wa kike. Na Mambo hayapo sawa Hadi leo Moto umewaka mtu Hana amani kabisa, yaani nisifanye chochote naambiwa Beatrice kwa hiyo humu ndani wimbo ni Beatrice. Aman huyu Dada angejua jina lake limeleta balaa kwenye familia yangu sijui angejisikiaje Dada wa watu. Sijui angeacha hii kazi yake ya kuuza bidhaa zake kwa mkopo na kutumiwa hela kwa simu sijui.
Sijui nimfokee huyu wife kwa Nini alishika simu? Sijui nikae chini nianze kumueleza Hali ilivyo hapa naona uvivu na akili inachoka kabisa.Yaani ni lawama tu kuwa aliniamini Sana na hakujua Kama Kuna siku nitamfanyia hayaa. Na hata nikimuelezea ataona Kama nampanga tu cos majibu tayari anayo.
Nimesha amua bana liwalo na liwe. Wacha Moto uwake ukimaliza utazima wenyewe.
NB
......... wanawake achaneni na simu za wanaume wenu .......