yello masai
JF-Expert Member
- Jan 8, 2016
- 3,542
- 3,502
Heshima kwenu ndugu zangu.
Jambo likikukuta mshirikishe mwingine mwenye uzoefu, na mficha maradhi kifo humuumbua.
Naamini humu wapo wengi wenye ndoa na wazoefu wa changamoto mbali mbali,
Nimekaa nikatafakari sana nikaona bora nilete huku jambo langu hili ili nipate mawazo mapya.
Nimekuwa na changamoto kadhaa kwenye ndoa yangu, japo nimekuwa nikizichukulia poa lakin sasa naona ni wakati wa kuwa serious kidogo,
Ninaomba niorodheshe mambo kadhaa ambayo kwa upande wangu nayaona kama ni madhaifu ya mke wangu na niseme tu kuna baadhi nilishaongea nae lakin sijaona mabadiliko yoyote.
Mke wangu ana umri wa miaka 28 na mimi nina 33 na tumejaliwa watoto wawili mpaka sasa. Na mke wangu ni mama wa nyumbani (sio mfanyakazi).
Namshukuru Mungu mengi natimiza na hatujawahi kulala njaa.
Mke wangu ananishangaza kwa tabia ya uvivu aliyonayo,
Ni mvivu kufua nguo, tenga la nguo chafu linaweza kujaa na zaidi lakin nguo hazifuliwi mpaka umkumbushe. Na ukimkumbusha atafua lakin utakuta nusu zimebaki.
Mimi ninafanya shughuli zangu karibu sana na tunaposhi, lakin nikimwambia apike mchana aniletee chakula inakuwa adhabu kubwa sana kwake. Kwahiyo mara nyingi naamua kula kwa mama ntilie tu.
Mwili wake ni mzito sana, hajui kujiongeza katika mambo mengi madogo madogo, kitu kinaweza kuwa kipo sehem sio yake lakini hawezi kunyanyuka akakiondoa mpaka umwambie, hawezi kuona meza ina vumbi au TV akachukua kitambaa akafuta.
Huyu mke wangu suala la kuamka kitandani saa mbili au tatu asubuh kwake ni la kawaida.
Mbaya zaidi, huyu mwanamke hajui kuonesha mapenzi. Navyojua mwanaume ukirud kutoka kwenye mihangaiko unatarajia upokelewe vizuri na mkeo, lakini yeye unakuta kakaa tu kwenye kiti, hakupi ile hali ya kujisikia kama umerudi nyumbani umemkuta mke.
Mbaya zaidi huyu mwanamke ni mvivu hata kwenye kufanya tendo la ndoa. Usipomkumbusha mwenyewe mnaweza kukaa hata wiki mbili na wakati mwingine nikihitaji anagoma mpaka nitumie ushawishi wa hali ya juu au nguvu. Lakini kwa hili siku hizi nimeamua kumpotezea, siombi kabisa, nkishashiba nalala zangu. Mpaka akili inaniambia nitafute mchepuko niwe najipoza kidogo.
Kama upo kwenye ndoa naomba mtazamo wako, maoni na ushauri kuhusu haya yanayonikuta kama mwanachama mwenzako kwenye chama hiki.
Jambo likikukuta mshirikishe mwingine mwenye uzoefu, na mficha maradhi kifo humuumbua.
Naamini humu wapo wengi wenye ndoa na wazoefu wa changamoto mbali mbali,
Nimekaa nikatafakari sana nikaona bora nilete huku jambo langu hili ili nipate mawazo mapya.
Nimekuwa na changamoto kadhaa kwenye ndoa yangu, japo nimekuwa nikizichukulia poa lakin sasa naona ni wakati wa kuwa serious kidogo,
Ninaomba niorodheshe mambo kadhaa ambayo kwa upande wangu nayaona kama ni madhaifu ya mke wangu na niseme tu kuna baadhi nilishaongea nae lakin sijaona mabadiliko yoyote.
Mke wangu ana umri wa miaka 28 na mimi nina 33 na tumejaliwa watoto wawili mpaka sasa. Na mke wangu ni mama wa nyumbani (sio mfanyakazi).
Namshukuru Mungu mengi natimiza na hatujawahi kulala njaa.
Mke wangu ananishangaza kwa tabia ya uvivu aliyonayo,
Ni mvivu kufua nguo, tenga la nguo chafu linaweza kujaa na zaidi lakin nguo hazifuliwi mpaka umkumbushe. Na ukimkumbusha atafua lakin utakuta nusu zimebaki.
Mimi ninafanya shughuli zangu karibu sana na tunaposhi, lakin nikimwambia apike mchana aniletee chakula inakuwa adhabu kubwa sana kwake. Kwahiyo mara nyingi naamua kula kwa mama ntilie tu.
Mwili wake ni mzito sana, hajui kujiongeza katika mambo mengi madogo madogo, kitu kinaweza kuwa kipo sehem sio yake lakini hawezi kunyanyuka akakiondoa mpaka umwambie, hawezi kuona meza ina vumbi au TV akachukua kitambaa akafuta.
Huyu mke wangu suala la kuamka kitandani saa mbili au tatu asubuh kwake ni la kawaida.
Mbaya zaidi, huyu mwanamke hajui kuonesha mapenzi. Navyojua mwanaume ukirud kutoka kwenye mihangaiko unatarajia upokelewe vizuri na mkeo, lakini yeye unakuta kakaa tu kwenye kiti, hakupi ile hali ya kujisikia kama umerudi nyumbani umemkuta mke.
Mbaya zaidi huyu mwanamke ni mvivu hata kwenye kufanya tendo la ndoa. Usipomkumbusha mwenyewe mnaweza kukaa hata wiki mbili na wakati mwingine nikihitaji anagoma mpaka nitumie ushawishi wa hali ya juu au nguvu. Lakini kwa hili siku hizi nimeamua kumpotezea, siombi kabisa, nkishashiba nalala zangu. Mpaka akili inaniambia nitafute mchepuko niwe najipoza kidogo.
Kama upo kwenye ndoa naomba mtazamo wako, maoni na ushauri kuhusu haya yanayonikuta kama mwanachama mwenzako kwenye chama hiki.