Mke wangu anadai niifukuze familia ya kaka nyumbani

Tafuta pesa afungue biashara yoyote auze vitu ajiendeleze na kusevu pesa kisha aondoke. Hapo ni pagumu haswa kama na yeye anafanya hayo yote huku una housegirl.. kiaina fulani shemeji yako ana uchokozi fulani anautenda.. labda anakupenda ila hawezi kukuambia. Mtafutie mtaji muanzishie biashara uache kuhudumia kila kitu.. yaani ameka kwako bure hata pesa ya chupi utakuwa unamnunulia wewe.. duh!!!
Umevuka mipaka na kwanini unamtoa yeye out bila kwenda na mkeo pia... unatatizo inabidi ujipange.. shemeji yako mgomvi sana anatamani maisha ya mkeo. Ni HATARI fikiria
 
Wadau nawasalimu,

Kuna mgogoro wa kifamilia unafukuta nyumbani kwangu,

Ni kwamba kuna kaka yangu ambae alipata matatizo na yupo jela sasa takribani mwaka wa pili akitumikia kifungo cha miaka saba.

Huku nje familia yake ilishindwa kumudu kodi ya nyumba baada ya kodi aliyolipa jamaa kuisha, mkewe alikuja kuniona kwa ajili ya hilo, nami nikaliwasilisha kwa wazee ambapo walishauri niichukue hiyo familia tukae pamoja kwangu kwa kujibanabana hivyo hivyo.

Kwa kuwa kumlipia kodi kwa kweli kwa majukumu niliyonayo nisingeweza, maana ada za shule za watoto wake ni mimi pia ndio nalipa kwa sasa, tuliwatoa shule za gharama na kuwaleta za kawaida.

Wakahamia kwangu yeye na watoto wake, tunaamini kuwa miaka mitano iliyobaki katika kifungo si mingi sana, tukimwacha mwanamke aende njia yake si ajabu jamaa akatoka huku familia imepotea au kuchukuliwa na jitu lingine ukizingatia mwanamke hakua na kazi, ni house wife na wote tunajua jinsi hawa wenzetu walivyo dhaifu, nadhani wengi mmeshasikia simulizi nyingi za watu waliofungwa waliwakuta wake zao wako wapi pindi walipotoka huko.

Nyumbani amani imetoweka sasa, kati ya mke wangu na huyo shemeji yangu, huyu shemeji kiukweli ni mchapa kazi na mwenye heshima ya hali ya juu, nikirudi kutoka kazini huja mlangoni kunifungulia geti, baada ya hapo huja kwenye gari hunipa shikamoo huku amepiga magoti na kupokea kwa unyenyekevu mzigo wowote ninaokua nao.

Nikitoka kwenda bar nikirudi saa tano saa sita usiku huja kunifungulia geti anamzuia housegirl asiamke anakuja yeye, kisha hunipakulia chakula na kunikaribisha, ananisubiria anatoa vyombo na kuni wish good night.

Sasa hii treatment ambayo huyu shemeji ananipa imemkasirisha sana mke wangu ambae kwa kweli nimeshasahau mara ya mwisho ni lini alinikirimu hivi, mm uhudumiwa na hg na wengi wao huwa viburi sio kama anavyofanya shemeji,
Sasa umezuka ugomvi mkubwa ndani kati ya mke wangu na shemeji.

Usiku silali naambiwa nichague nimfukuze shemeji au yeye aondoke eti kama nimeona shemeji ni bora, mke wangu sasa haendi kulala mapema anakaa sitting room na shemeji hadi saa sita hadi nifike ili aone kama kuna kitu kinafanyika, ameshatangazia wanaukoo kuwa mimi na shemeji kuna kitu kinaendelea jambo ambalo sio la kweli.

Pia shemeji anapenda kuniita kwa jina la "" mume"" juzi mke wangu alimsikia akiniita hivyo na kumuuliza mume wako na nani ukazuka ugomvi mkubwa sana, wakati mwingine naporudi usiku mwingi shemeji anakua yupo ukumbini na mavazi ya kulalia akitazama series, mke wangu nae anatoka kuja kunisubiria hapo hapo akidhani kuna kitu labda tutafanya hapo na shemeji, hawazungumzishani kitu hadi mimi napofika, yule shemeji anawahi mezani kunipakulia chakula.

Juzi juzi tulikua tunakunywa bia mimi na shemeji yangu mahala fulani, huwa namtoa out mara moja moja ili walau apoteze mawazo ya matatizo yaliyowapata, nikatumia Muda huo kuongea ili ajishushe kuepusha ugomvi usiokua wa lazima pale home lakini akanijibu kuwa wife ndio anapaswa kujishusha kwa kuwa ni mdogo kwake.

La hasha nikampangie kwake yeye na wanawe niwe namhudumia huko, nikamjibu sina uwezo huo wa kuhudumia familia mbili, ukizingatia kuwa ndugu ni kama wamenitelekezea mm huu mzigo kila mtu anajifanya yupo busy na wengine wakilia ugumu wa maisha.

Wadau mnanishauri nini kuhusu tatizo hili, maana hali sasa ni tete, mke wangu amenipa ultimatum kwamba nimuondoe shemeji or else aondoke yeye, mimi tatizo langu kubwa ni wale watoto, hatima yao, inafikia hatua sasa mke wangu anawazuia watoto wetu wasicheze pamoja na wale wa kaka kutokana na ugomvi na mama yao.

Msaada wa haraka unahitajika



Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu ugomvi unataka mwenyewe, kwanini usimzuie huyo Shemeji yako kufanya hayo anayofanya na umwambie mkeo ajifunze kwa mwenzake na kuanza kuwajibika kama Mke?una uwezo wa kuhudumia familia mbili zikiwa pamoja unashindwa kumpangishia Shemeji yako walau chumba tu?mbona vipo vya gharama nafuu tu lazima akubaliane na hali halisi na kukubali kwamba maisha kuna kupanda na kushuka aishi chumba utakachomudu kumlipia na ikiwezekana mtafutie hata kijibiashara kidogo hata cha mama ntilie ili aweze kupata baadhi ya mahitaji yake ili hali na wewe ukiongeza nguvu,unajua tatizo huwa tunafikiria vitu vikubwa wakati kila hali ina solution zake kulingana na uwezo.Mke wako anafanya hivyo for the sake ya ndoa yenu anaona mambo yanavyokwenda ipo siku utateleza ukamsingizia shetani. Jiongeze
 
Hujafa hujaumbika, kweli miaka mitano si mingi. Endelea kutunza familia ya kaka yako mkuu maana ndio damu yako na ukoo wako mana mwanamke ni sawa na ganda la mti mwingine kupachika kwenye mti mwingine kitu ambacho hayawezi kushikana ila wewe na kaka yako ni ganda la mti mmoja. Naamini yapo mazuri ambayo kaka yako alishawahi kukufanyia na yeye kuwa gerezani ni kipimo cha fadhila za kaka yako kwako na tambua LEO KWAKE, KESHO KWAKO. Hao watoto wa kaka yako usiwaone wadogo, kesho watapata kazi za maana tu na watawasaidia, (Nakumbuka mzee wangu alipostaafu ba'mkukwa na baadhi ya
ba'wadogo walitudharau sana tukiwa S/Msingi wakijua hatutafika popote lakini tulipambana kwa sasa tumeua University wameanza kujirudi nasi tumesamehe 7x70).

Shem kukuita MUME ni kawaida ila hizo za kufungua geti na kukupakulia chakula afanye mkeo kama hataki jipakulie mwenyewe.

NB:
Wanawake huwa hawapendani.
 
Undugu hauishi je akimbandua mke wa kaka yake vipi hqpo undugu utakuwaje! Yeye amwambie shemeji yake ukweli pale sio kwake hivyo afuate masharti ya pale mbona yeye kashindwa kukaa mwenyewe kwake asimvunjie nyumba mwenzie hata mmewe akisikia mke wa mdogo wake kaondoka kisa mkewe wanakulana na mdogo wake nini kitatokea!

Sent using Jamii Forums mobile app
hata akimla undugu uko pale pale.....hawezi badilisha damu na vimelea vyake......awe mwanaume wa kweli.....kujisogeza kwa shemejio ni tatizo haswaa....
 
Mimi muda wote nasoma hii stori nacheka tu kwa jinsi jamaa anavyotuchuuza

Sent using Jamii Forums mobile app
Umeona eeh....anazunguuuka kumfanya mkewe aonekane mbaya kumbe tatizo lake mwenyewe. Na wa jela ana miaka mingine mitano mizima....akirudi wallah atakuta kabadilishwa jina yeye ndiyo kawa shemeji badala ya mume....
 
Ila nawe kama unamtaka shemejio hiviiii na shemejio anakutaka pia ama mnamahusiano tayari ila huweki wazi.

anavaa nguo za kulalia

anakimbikia kukupakulia chakula wakati mkeo yupo, mnatoana ana out bila mkeo...ha ha ha hata mie ningewaka kunusuru ndoa.


La msingi hapo

mwambie shemejio aache kufanya majukumu ya mke kama mkeo hataki mwache aendeleee kufanya hausgeli kama ulivyozoea zamani

yaaani kupigiwa magoti na kupokelewa begi ndio kunakufanya utake kuendelea kupokea hayo...?? kwani ukikosa utapungukiwa nini??

la pili mwambie tena huyo shemejio ajishushe yupo hapo kusaidiwa jibu alolitoa i la kijinga sana.."eti ajishishe mkeo kwakuwa ni mdogo" anatakiwa ajue nafasi yake..shenzi zake..anataka kuwa mke huyo.

lingine aache utani wa "mume" wakati mumewake yupo ndani kwa muda mrefu.. utani mwingine sio mzuri na wala hauna afya hasa kwa senario yako.

la mwisho....mtafutieni mtaji afanye biashara ajitegemee maisha sio kazi tu.

mnaweza kukaa kama familia mchangieni mtaji aokote ya kodi ya nyumba hata vyumba 2.

Sent using Jamii Forums mobile app
Yani umechukua mawazo yangu kabisa, me mwenyewe nimeshangaa, alafu cha ajabu kuna watu humu wanamlaumu huyo mke wa mleta mada eti ana roho mbaya sijui nini, tena ukute akija hapa kuhadithia mambo ambayo huyo bi dada anayafanya tutachoka. Mimi mwenyewe huwezi kuja kuishi kwangu alafu ujifanya wewe ndo mwenye nyumba hadi kwa mume wangu weee thubutuu mbona ningewapisha mtu na shem wake waliwazane vzr pumbavuuu
 
Wanawake wengi huwa hawapendi kabisa ndugu wa Mume, wanajitahidi sana kuwapenda watu wa pembeni ili waonekane wazuri.
 
Ila nawe kama unamtaka shemejio hiviiii na shemejio anakutaka pia ama mnamahusiano tayari ila huweki wazi.

anavaa nguo za kulalia

anakimbikia kukupakulia chakula wakati mkeo yupo, mnatoana ana out bila mkeo...ha ha ha hata mie ningewaka kunusuru ndoa.


La msingi hapo

mwambie shemejio aache kufanya majukumu ya mke kama mkeo hataki mwache aendeleee kufanya hausgeli kama ulivyozoea zamani

yaaani kupigiwa magoti na kupokelewa begi ndio kunakufanya utake kuendelea kupokea hayo...?? kwani ukikosa utapungukiwa nini??

la pili mwambie tena huyo shemejio ajishushe yupo hapo kusaidiwa jibu alolitoa i la kijinga sana.."eti ajishishe mkeo kwakuwa ni mdogo" anatakiwa ajue nafasi yake..shenzi zake..anataka kuwa mke huyo.

lingine aache utani wa "mume" wakati mumewake yupo ndani kwa muda mrefu.. utani mwingine sio mzuri na wala hauna afya hasa kwa senario yako.

la mwisho....mtafutieni mtaji afanye biashara ajitegemee maisha sio kazi tu.

mnaweza kukaa kama familia mchangieni mtaji aokote ya kodi ya nyumba hata vyumba 2.

Sent using Jamii Forums mobile app
This is right.
Huyo mwanamke afunguliwe biashara aishi kivyake.
Usikute ameshaanza kumgonga huyo mwanamke.
 
Ila nawe kama unamtaka shemejio hiviiii na shemejio anakutaka pia ama mnamahusiano tayari ila huweki wazi.

anavaa nguo za kulalia

anakimbikia kukupakulia chakula wakati mkeo yupo, mnatoana ana out bila mkeo...ha ha ha hata mie ningewaka kunusuru ndoa.


La msingi hapo

mwambie shemejio aache kufanya majukumu ya mke kama mkeo hataki mwache aendeleee kufanya hausgeli kama ulivyozoea zamani

yaaani kupigiwa magoti na kupokelewa begi ndio kunakufanya utake kuendelea kupokea hayo...?? kwani ukikosa utapungukiwa nini??

la pili mwambie tena huyo shemejio ajishushe yupo hapo kusaidiwa jibu alolitoa i la kijinga sana.."eti ajishishe mkeo kwakuwa ni mdogo" anatakiwa ajue nafasi yake..shenzi zake..anataka kuwa mke huyo.

lingine aache utani wa "mume" wakati mumewake yupo ndani kwa muda mrefu.. utani mwingine sio mzuri na wala hauna afya hasa kwa senario yako.

la mwisho....mtafutieni mtaji afanye biashara ajitegemee maisha sio kazi tu.

mnaweza kukaa kama familia mchangieni mtaji aokote ya kodi ya nyumba hata vyumba 2.

Sent using Jamii Forums mobile app
This is right.
Huyo mwanamke afunguliwe biashara aishi kivyake.
Usikute ameshaanza kumgonga huyo mwanamke.
 
Umeona eeh....anazunguuuka kumfanya mkewe aonekane mbaya kumbe tatizo lake mwenyewe. Na wa jela ana miaka mingine mitano mizima....akirudi wallah atakuta kabadilishwa jina yeye ndiyo kawa shemeji badala ya mume....
Hahahahah katafuta njia ya kumfukuza imeshindikana anaamua kumtafutia visa mkewe.
 
Utuambie tu ukweli kuhusu huyo shemeji yako haiwezekani akwambie hawez kujishusha kwa mkeo na we unaridhika pia unaendelea kufurahia tuu huduma zake mkataze asikuhudumie hayo matatzo unaleta mwnyewe,..na umesema una wazee kwa mini asiende kwa wazazi wenu upeleke matumizi huko?
 
Hii Ngumu kumeza,but here are some things to go thro

1. Mke wa kaka yako aende kwa ndugu zake,hapo kwako wabaki watoto tu.
Kwa maana yeye ndie chanzo cha kupoteza amani,anakufungulia geti hiyo vepe wakati mdada wa Kazi yupo? Anavaaje Nguo za kulalia halafu akupakulie chakula!!!! Mbona anaonyesha direct mambo ya kishetani??? Si ana mama wakubwa na Dada au ndugu zake?? Aende huko abakize watoto.

2. Ongea na mke wako,ugomvi wa watu lazima asiwaingize watoto,ujue watoto wanakua na wanaona kinachoendelea?? Watajenga chuki mioyoni mwao,watashindwa kusaidiana kama ambavyo wewe unamsaidia kaka yako kwa sasa.

3. Nenda kalifikishe kwa kaka yako huko gerezani kusaidie mawazo mke wake aende wapi au umeamua aende wapi kutokana na yanayoendelea.

Nb: kabishangaza sana unataka kushindana na mwenye nyumba inahusu.

Au

Make mgomo baridi,Ili akikufungulia gate mwambie usisumbuke mwache Dada wa Kazi afanye hiyo Ndio Kazi yake ukiingilia nitakuwa namlipa mshahara bure. Akikupakulia chakula kalie chumbani kwako na upotelee huko mpaka kesho yake avitoe mke wako. Akili kichwani kwako but mke wako huko right about the thoughts Ku kuhusu wewe na huyo mke wa kaka ako,mwache abiria achunge mzigo wake.
 
Wadau nawasalimu,

Kuna mgogoro wa kifamilia unafukuta nyumbani kwangu,

Ni kwamba kuna kaka yangu ambae alipata matatizo na yupo jela sasa takribani mwaka wa pili akitumikia kifungo cha miaka saba.

Huku nje familia yake ilishindwa kumudu kodi ya nyumba baada ya kodi aliyolipa jamaa kuisha, mkewe alikuja kuniona kwa ajili ya hilo, nami nikaliwasilisha kwa wazee ambapo walishauri niichukue hiyo familia tukae pamoja kwangu kwa kujibanabana hivyo hivyo.

Kwa kuwa kumlipia kodi kwa kweli kwa majukumu niliyonayo nisingeweza, maana ada za shule za watoto wake ni mimi pia ndio nalipa kwa sasa, tuliwatoa shule za gharama na kuwaleta za kawaida.

Wakahamia kwangu yeye na watoto wake, tunaamini kuwa miaka mitano iliyobaki katika kifungo si mingi sana, tukimwacha mwanamke aende njia yake si ajabu jamaa akatoka huku familia imepotea au kuchukuliwa na jitu lingine ukizingatia mwanamke hakua na kazi, ni house wife na wote tunajua jinsi hawa wenzetu walivyo dhaifu, nadhani wengi mmeshasikia simulizi nyingi za watu waliofungwa waliwakuta wake zao wako wapi pindi walipotoka huko.

Nyumbani amani imetoweka sasa, kati ya mke wangu na huyo shemeji yangu, huyu shemeji kiukweli ni mchapa kazi na mwenye heshima ya hali ya juu, nikirudi kutoka kazini huja mlangoni kunifungulia geti, baada ya hapo huja kwenye gari hunipa shikamoo huku amepiga magoti na kupokea kwa unyenyekevu mzigo wowote ninaokua nao.

Nikitoka kwenda bar nikirudi saa tano saa sita usiku huja kunifungulia geti anamzuia housegirl asiamke anakuja yeye, kisha hunipakulia chakula na kunikaribisha, ananisubiria anatoa vyombo na kuni wish good night.

Sasa hii treatment ambayo huyu shemeji ananipa imemkasirisha sana mke wangu ambae kwa kweli nimeshasahau mara ya mwisho ni lini alinikirimu hivi, mm uhudumiwa na hg na wengi wao huwa viburi sio kama anavyofanya shemeji,
Sasa umezuka ugomvi mkubwa ndani kati ya mke wangu na shemeji.

Usiku silali naambiwa nichague nimfukuze shemeji au yeye aondoke eti kama nimeona shemeji ni bora, mke wangu sasa haendi kulala mapema anakaa sitting room na shemeji hadi saa sita hadi nifike ili aone kama kuna kitu kinafanyika, ameshatangazia wanaukoo kuwa mimi na shemeji kuna kitu kinaendelea jambo ambalo sio la kweli.

Pia shemeji anapenda kuniita kwa jina la "" mume"" juzi mke wangu alimsikia akiniita hivyo na kumuuliza mume wako na nani ukazuka ugomvi mkubwa sana, wakati mwingine naporudi usiku mwingi shemeji anakua yupo ukumbini na mavazi ya kulalia akitazama series, mke wangu nae anatoka kuja kunisubiria hapo hapo akidhani kuna kitu labda tutafanya hapo na shemeji, hawazungumzishani kitu hadi mimi napofika, yule shemeji anawahi mezani kunipakulia chakula.

Juzi juzi tulikua tunakunywa bia mimi na shemeji yangu mahala fulani, huwa namtoa out mara moja moja ili walau apoteze mawazo ya matatizo yaliyowapata, nikatumia Muda huo kuongea ili ajishushe kuepusha ugomvi usiokua wa lazima pale home lakini akanijibu kuwa wife ndio anapaswa kujishusha kwa kuwa ni mdogo kwake.

La hasha nikampangie kwake yeye na wanawe niwe namhudumia huko, nikamjibu sina uwezo huo wa kuhudumia familia mbili, ukizingatia kuwa ndugu ni kama wamenitelekezea mm huu mzigo kila mtu anajifanya yupo busy na wengine wakilia ugumu wa maisha.

Wadau mnanishauri nini kuhusu tatizo hili, maana hali sasa ni tete, mke wangu amenipa ultimatum kwamba nimuondoe shemeji or else aondoke yeye, mimi tatizo langu kubwa ni wale watoto, hatima yao, inafikia hatua sasa mke wangu anawazuia watoto wetu wasicheze pamoja na wale wa kaka kutokana na ugomvi na mama yao.

Msaada wa haraka unahitajika



Sent using Jamii Forums mobile app


UNATEMBEA NAYE NA KUMPA KICHWA WEWE, USITUFANYE SISI WAJINGA KIASI HIKI ....
 
Jamani...hata kama kuishi nyumba za watu mtihani...ndio ukeshe usiku kusubiria kufungua mageti ili hali kuna mke na dada wa kazi juu....Mbona kazi za kuamsha amsha ni nyingi tu za kuonyesha uwepo wako....usafi ndani na nje, kama kuna eneo tifua bustani ali mradi heka heka tu....
Hapo ndo alipokosea
 
Jamaa kasema hata zaman mke wake alikuwa hampi hizo huduma
Zaidi ya dada wa kazi tu
Sasa watu sijui hawaoni huo msitari!
Watu wamekazana tu anaingilia majukum sio yake akat jamaa
Amekiri dada wa kaz ndo alikuwa
Akilfanyia hayo
Ya kumfungulia geti
Mimi mpaka nimeamua kuacha na sitaki kubishana na watu humu......kuishi nyumba za watu ni kazi sana hasa ukiangalia na situation ya huyo dada
 
15 Reactions
Reply
Back
Top Bottom