Mke wangu anadai niifukuze familia ya kaka nyumbani

navin-govind

Member
Apr 10, 2015
72
112
Wadau nawasalimu,

Kuna mgogoro wa kifamilia unafukuta nyumbani kwangu,

Ni kwamba kuna kaka yangu ambae alipata matatizo na yupo jela sasa takribani mwaka wa pili akitumikia kifungo cha miaka saba.

Huku nje familia yake ilishindwa kumudu kodi ya nyumba baada ya kodi aliyolipa jamaa kuisha, mkewe alikuja kuniona kwa ajili ya hilo, nami nikaliwasilisha kwa wazee ambapo walishauri niichukue hiyo familia tukae pamoja kwangu kwa kujibanabana hivyo hivyo.

Kwa kuwa kumlipia kodi kwa kweli kwa majukumu niliyonayo nisingeweza, maana ada za shule za watoto wake ni mimi pia ndio nalipa kwa sasa, tuliwatoa shule za gharama na kuwaleta za kawaida.

Wakahamia kwangu yeye na watoto wake, tunaamini kuwa miaka mitano iliyobaki katika kifungo si mingi sana, tukimwacha mwanamke aende njia yake si ajabu jamaa akatoka huku familia imepotea au kuchukuliwa na jitu lingine ukizingatia mwanamke hakua na kazi, ni house wife na wote tunajua jinsi hawa wenzetu walivyo dhaifu, nadhani wengi mmeshasikia simulizi nyingi za watu waliofungwa waliwakuta wake zao wako wapi pindi walipotoka huko.

Nyumbani amani imetoweka sasa, kati ya mke wangu na huyo shemeji yangu, huyu shemeji kiukweli ni mchapa kazi na mwenye heshima ya hali ya juu, nikirudi kutoka kazini huja mlangoni kunifungulia geti, baada ya hapo huja kwenye gari hunipa shikamoo huku amepiga magoti na kupokea kwa unyenyekevu mzigo wowote ninaokua nao.

Nikitoka kwenda bar nikirudi saa tano saa sita usiku huja kunifungulia geti anamzuia housegirl asiamke anakuja yeye, kisha hunipakulia chakula na kunikaribisha, ananisubiria anatoa vyombo na kuni wish good night.

Sasa hii treatment ambayo huyu shemeji ananipa imemkasirisha sana mke wangu ambae kwa kweli nimeshasahau mara ya mwisho ni lini alinikirimu hivi, mimi uhudumiwa na hg na wengi wao huwa viburi sio kama anavyofanya shemeji, Sasa umezuka ugomvi mkubwa ndani kati ya mke wangu na shemeji.

Usiku silali naambiwa nichague nimfukuze shemeji au yeye aondoke eti kama nimeona shemeji ni bora, mke wangu sasa haendi kulala mapema anakaa sitting room na shemeji hadi saa sita hadi nifike ili aone kama kuna kitu kinafanyika, ameshatangazia wanaukoo kuwa mimi na shemeji kuna kitu kinaendelea jambo ambalo sio la kweli.

Pia shemeji anapenda kuniita kwa jina la "" mume"" juzi mke wangu alimsikia akiniita hivyo na kumuuliza mume wako na nani ukazuka ugomvi mkubwa sana, wakati mwingine naporudi usiku mwingi shemeji anakua yupo ukumbini na mavazi ya kulalia akitazama series, mke wangu nae anatoka kuja kunisubiria hapo hapo akidhani kuna kitu labda tutafanya hapo na shemeji, hawazungumzishani kitu hadi mimi napofika, yule shemeji anawahi mezani kunipakulia chakula.

Juzi juzi tulikua tunakunywa bia mimi na shemeji yangu mahala fulani, huwa namtoa out mara moja moja ili walau apoteze mawazo ya matatizo yaliyowapata, nikatumia Muda huo kuongea ili ajishushe kuepusha ugomvi usiokua wa lazima pale home lakini akanijibu kuwa wife ndio anapaswa kujishusha kwa kuwa ni mdogo kwake.

La hasha nikampangie kwake yeye na wanawe niwe namhudumia huko, nikamjibu sina uwezo huo wa kuhudumia familia mbili, ukizingatia kuwa ndugu ni kama wamenitelekezea mimi huu mzigo kila mtu anajifanya yupo busy na wengine wakilia ugumu wa maisha.

Wadau mnanishauri nini kuhusu tatizo hili, maana hali sasa ni tete, mke wangu amenipa ultimatum kwamba nimuondoe shemeji or else aondoke yeye, mimi tatizo langu kubwa ni wale watoto, hatima yao, inafikia hatua sasa mke wangu anawazuia watoto wetu wasicheze pamoja na wale wa kaka kutokana na ugomvi na mama yao.

Msaada wa haraka unahitajika
 
Mwambie pia shemeji ako aache kuvaa night dress siting room, awe anavaa kipindi cha kulala tu. Pia anakiwa ajishushe tu, kwani hapo si kwake na asikuonyeshe mahaba zaidi hizo kazi inabidi azifanye mkeo mwambie mkeo pia ajiongeze pia, mbaya zaidi wanawake huwa hawawezi ishi pamoja hilo nalo ni tatizo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wote inaonekana ni watu wenye nia nzuri, Lakini mwambie shemeji yako aache kufanya hayo mambo. Kwa sababu Mke wako anaona kama anachukua sehemu yake.

Fanya Kikao waite ndugu wote wachangie Halafu jaribu kupangisha nyumba nyingine kwa shemeji na watoto wake.
 
1. Hongera sana kwa kumfadhili kaka yako aliyepo matatizoni, huo ni uanaume.
2. Wanawake wakikaa pamoja ni desturi yao kutoaminiana.
3. Mpangishie shemeji yako mpe na mtaji ili azalishe pato lake.
 
Huyo mke wako ana roho mbaya huo ndio ukweli..... Kwa matatizo aliyopata kaka yako si vema ukawafukuza hapo nyumbani kwako cha msingi ni kuongea na shemeji yako aache tabia ya kukusubiria usiku na kukuandalia chakula..... Na pia awe mpole tu kwa mke wako kwa kuwa yeye ana shida..... Haya ni maisha leo kwake kesho kwenu... Endeleza ubinadamu wako kaka achana na roho mbaya aliyokuwa nao mke wako

Kingine make sure hao watoto wanakuwa na maelewano mazuri kwa kuwa wote ni ndugu..... Jitahidi hata siku moja moja unawatoa hao watoto unawapeleka hata beach unakaa nao na kuwakumbushia kuwa inabidi wapendane wao ni ndugu na wasaidiane pia katika maisha yao...... Wajengee mazoea ya kuwa pamoja

Ila mke wako ana tabia za kichawi
 
Ila nawe kama unamtaka shemejio hiviiii na shemejio anakutaka pia ama mnamahusiano tayari ila huweki wazi.

Anavaa nguo za kulalia

Anakimbikia kukupakulia chakula wakati mkeo yupo, mnatoana ana out bila mkeo...ha ha ha hata mie ningewaka kunusuru ndoa.

La msingi hapo

Mwambie shemejio aache kufanya majukumu ya mke kama mkeo hataki mwache aendeleee kufanya hausgeli kama ulivyozoea zamani

Yaaani kupigiwa magoti na kupokelewa begi ndio kunakufanya utake kuendelea kupokea hayo...?? kwani ukikosa utapungukiwa nini??

La pili mwambie tena huyo shemejio ajishushe yupo hapo kusaidiwa jibu alolitoa i la kijinga sana.."eti ajishishe mkeo kwakuwa ni mdogo" anatakiwa ajue nafasi yake..shenzi zake..anataka kuwa mke huyo.

lingine aache utani wa "mume" wakati mumewake yupo ndani kwa muda mrefu.. utani mwingine sio mzuri na wala hauna afya hasa kwa senario yako.

la mwisho....mtafutieni mtaji afanye biashara ajitegemee maisha sio kazi tu.

mnaweza kukaa kama familia mchangieni mtaji aokote ya kodi ya nyumba hata vyumba 2.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa viumbe hawana rangi halisi mkuu, cha msingi ni kusimamia kile unachoamini.

Mwanamke asiependa ndugu zangu kwangu ni kimeo hata kama nimemfukuzia kwa muda

Psalm 133:1 "Behold, how good and how pleasant it is for brethren to dwell together in unity."
 
1. Shemeji aache kuingilia majukumu ya mwenzie.
2. Acha ku-entertain tabia za shemeji yako kwa kuhisi kuwa ni za kawaida, kwa wanawake hakuna dogo.
3. Kama wazazi wenu wapo, peleka huyo shemeji akawafanyie huo ukarimu wazazi kwa muda ili ugomvi upoe, baki na wanae ili waendelee na masomo.

4. Punguza mazoea yaliyopitiliza kwa shemeji yako, maana mnakoelekea utamla kabla kifungo cha jamaa hakijaisha au utaanza kumwonea wivu siku akipata lijamaa (kumbuka nae ni binadamu mwenye hisia)

NB:
Usitatue hilo varangati kwa vikao, maana asilimia kubwa ya vikao ndivyo huvuruga ndoa/mahusiano. Kila jambo liko mikononi mwako.
 
Yani uko mbioni kumla shemeji. Kwasababu kwanza yeye atakua anakutaka, maana huenda kabla ya mme wake kufungwa alikua hamfanyi haya yote kwa mmewe. Pili kuna udhaifu fulani umeonyesha mbele yake kuhusu mkeo sasa anataka achukue hiyo advantage umtafune. Hawa wote ambao wanasema huyu dada anaroho mbaya aithani alishaona mbele.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom