pwilo
JF-Expert Member
- May 27, 2015
- 10,098
- 12,469
Wakuu habari zenu,
Poleni na majukumu ya mihangaiko ya kila siku bila kupoteza muda niende kwenye mada husika.
Usiku wa kuamkia leo kumetokea tukio la kusikitisha maeneo ya Mbagala Rangi Tatu (Kimbangulile) karibu na mbagala kanisani nyuma kidogo ya kiwanda cha Rasta Cha DARLING ambapo jamaa mmoja, amemuuwa mtu anayedhaniwa kuwa ndo sababu ya kutengana na aliyekuwa mke wake kwa kumchoma na kisu mpaka umauti kumfika na kumjeruhi aliyekuwa mke wake. Baada ya tukio mtuhumiwa alikimbia bila kukamatwa licha ya mwanamke huyo kupiga kelele kuwa "wanauwana huku ndani naombeni msaada" lakini hakuna mwananchi aliyejitokeza na mtuhumiwa kufanikiwa kukimbia eneo la tukio baada ya kumuuwa mwanaume huyo aliyekuwa wamelala na mwanamke huyo huku mwanamke akijeruhiwa na kukimbizwa hospital.
Inasemakana muuwaji alikuwa amemuowa mwanamke mke huyo Ila walitengana baada ya mwanamke kutokuwa mwaminifu kwake na kudai alikuwa anachepuka baada ya ugomvi mwanamke akadai talaka. Sasa aliyekuwa mume wake alipata hasira baada ya kupata taarifa kuwa mwanamke huyo ameolewa na jamaa mwingine ambaye ni wa karibu na wanafahamiana Jambo amabalo mwanaume alihisi walikuwa wanachepuka tangu yupo naye kwenye ndoa na mwanaume huyo alifikia hatua hiyo baada ya uchunguzi wa mda mrefu na hatimae kufanya tukio Hilo lilokusanya watu kutoka maeneo mbali mbali ya mbagala ila maiti ameshaondolewa na mwanamke bado anapatiwa matibabu kwa majeraha aliyo yapata
Wakuu tuweni makini na hawa viumbe kabla ya kuamua kuishi naye kama mke na mume maaana inasemakana mwanamke ndo alidai talaka japo mwanaume alikuwa anampenda sana mwanamke huyo kumbe kuna msela kamdatisha leo hii jamaa hatunaye tena na muuwaji na mwanamke mwisho wao sio mzuri maana vyombo vya Sheria vitalishughulikia Hilo swala na adhabu itatolewa kwa mwenye hatia.
Poleni na majukumu ya mihangaiko ya kila siku bila kupoteza muda niende kwenye mada husika.
Usiku wa kuamkia leo kumetokea tukio la kusikitisha maeneo ya Mbagala Rangi Tatu (Kimbangulile) karibu na mbagala kanisani nyuma kidogo ya kiwanda cha Rasta Cha DARLING ambapo jamaa mmoja, amemuuwa mtu anayedhaniwa kuwa ndo sababu ya kutengana na aliyekuwa mke wake kwa kumchoma na kisu mpaka umauti kumfika na kumjeruhi aliyekuwa mke wake. Baada ya tukio mtuhumiwa alikimbia bila kukamatwa licha ya mwanamke huyo kupiga kelele kuwa "wanauwana huku ndani naombeni msaada" lakini hakuna mwananchi aliyejitokeza na mtuhumiwa kufanikiwa kukimbia eneo la tukio baada ya kumuuwa mwanaume huyo aliyekuwa wamelala na mwanamke huyo huku mwanamke akijeruhiwa na kukimbizwa hospital.
Inasemakana muuwaji alikuwa amemuowa mwanamke mke huyo Ila walitengana baada ya mwanamke kutokuwa mwaminifu kwake na kudai alikuwa anachepuka baada ya ugomvi mwanamke akadai talaka. Sasa aliyekuwa mume wake alipata hasira baada ya kupata taarifa kuwa mwanamke huyo ameolewa na jamaa mwingine ambaye ni wa karibu na wanafahamiana Jambo amabalo mwanaume alihisi walikuwa wanachepuka tangu yupo naye kwenye ndoa na mwanaume huyo alifikia hatua hiyo baada ya uchunguzi wa mda mrefu na hatimae kufanya tukio Hilo lilokusanya watu kutoka maeneo mbali mbali ya mbagala ila maiti ameshaondolewa na mwanamke bado anapatiwa matibabu kwa majeraha aliyo yapata
Wakuu tuweni makini na hawa viumbe kabla ya kuamua kuishi naye kama mke na mume maaana inasemakana mwanamke ndo alidai talaka japo mwanaume alikuwa anampenda sana mwanamke huyo kumbe kuna msela kamdatisha leo hii jamaa hatunaye tena na muuwaji na mwanamke mwisho wao sio mzuri maana vyombo vya Sheria vitalishughulikia Hilo swala na adhabu itatolewa kwa mwenye hatia.