Mke wa mtu anadai mtoto aliyezaa kwenye ndoa ni wangu

Kwanza nianze kwa kuwasalimia Great Thinkers na naamini mtanipa ushauri wa Hekima na Busara.

Mimi ni kudume ambaye kwa sasa nina mke na watoto watatu kwa ufupi niko kwenye ndoa huu mwaka wa 6.Kabla ya kuwa na mke niliye naye nilikuwa na uhusiano na mwanamke mwingine kwa muda wa miaka 6 na hatukuendelea na uhusiano si kwa sababu nyingine bali ni haraka yake ya kutaka kuolewa kipindi nikiwa bado masomoni.So aliniuliza kama niko tayari kumuoa na kweli sikuwa tayari so akaamua kuolewa na mwanamume mwingine.

Nilirudi nyumbani kwa ajili ya likizo nikakuta tayari ameshaolewa na ana takribani miezi miwili kwenye ndoa but aliposikia nimerudi alinitafuta na akadai kuwa mwanamume aliyenaye hampi shughuli kama aliyokuwa akipata toka kwangu hivyo nikajikuta tumeduu hivyo hivyo.Hiyo ilikuwa ni mara moja tu na hatukuwahi kurudia tena manake na mimi nilikaa muda mfupi tu nikawa nimeoa.

sasa Ishu ilianza kipindi huyu mpenzi wa zamani akiwa mjamzito coz aliniambia kuwa huo mzigo ni wangu na alinitegeshea kwa makusudi ila nilipuuzia kwa kuamini zilikuwa ni stori za kujifurahisha lakini hali imekuwa mbaya zaidi hivi majuzi baada ya yeye kurudi kijijini kwetu akiwa na mtoto wake huyo mwenye miaka 8 kwa sasa kwani ni carbon copy yangu na hata mama yangu mzazi alipomuona alinipigia simu na kuniambia hilo hilo kwani akisimama na mwanange mwenye miaka 6 kwa sasa ni kama mapacha.

Nifanyeje sasa na kila mara anapigia simu kuniambia kuwa binti yako anakusalimia na mwenyewe nilipomwona nikataka kuzimia coz ananifanana koprait.
kijijini amerudi kuwa ndoa imevunjika au likizo??.
sidhani kama ni busara kwenda kutafuta mtoto ndani ya ndoa ya mtu. sikushauri kuhangaika na mtoto aliye kati ya ndoa ya watu.

labda kama unaujasiri, uthibitishe wewe na huyo mwanamke , kwa mume wa huyo mwanamke kuwa wewe ni baba wa mtoto, ili upate huyo mtoto, lakini kumbuka unavunja ndoa ya mwanamume mwenzio
 
Kwa dunia ya leo unaweza kukuta hata hao hao watatu unaojifanya ni wako nao sio wako vilevile!!!
Cha msingi chukua hao watatu ulio nao,
Jumlisha na huyo mzamiaji wote kapime DNA,
"Alieuziwa cheni bandia nae kalipa fedha bandia"
 
Hiyo ndio moja ya adhabu za zinaa. Mtoto hana raha maishani mwake (phsychologically), wewe huna raha, mamake hana raha, mama'ko hana raha, na sisi sote umetutowa raha. Halafu unajisifu eti ni "kidume", kuna kidume kikatembea nje ya ndoa? Ungejisifu kwa mema na si kwa huu upuuzi, nendeni mkaungame. Si mkisha ungama mnasamehewa?
 
Hiyo ndio moja ya adhabu za zinaa. Mtoto hana raha maishani mwake (phsychologically), wewe huna raha, mamake hana raha, mama'ko hana raha, na sisi sote umetutowa raha. Halafu unajisifu eti ni "kidume", kuna kidume kikatembea nje ya ndoa? Ungejisifu kwa mema na si kwa huu upuuzi, nendeni mkaungame. Si mkisha ungama mnasamehewa?

FF hujanitendea haki kwa kunishutumu kuwa najivunia nilichotenda bali nilikuwa najaribu kujitofautisha kwa jinsia manake tuna mwanamume humu anait
https://www.jamiiforums.com
 
...eti tukajikuta tumeduu hivyo hivyo... Imoeee.... Halafu unajisifia foto copy na wewe! Kama ukitaka kulinda ndoa na familia yako, Achana na ufotocopy, achana na huyo malaya wako, yeye akuthibitishie kuwa huyo ni mtoto wako. Kwa ujasiri gani wa kutembea na mke wa mtu bila kinga? Hata kama alikuwa gf wako lakini sasa kaolewa muda mrefu. Na kama uliduu hivyo hivyo kwa huyo malaya wako ni mara ngapi umefanya the same kwa mademu wengine? Wangejua ulipo wangeshakuletea nao fotocopy zako. Utawapokea pia? Huko masomoni ulisomea nini mwenzangu? Nakushauri tubu dhambi na uache uzinzi, haukuongezei chochote ila mausumbufu na kukosa maraha. Tulia utunze familia yako, jaribu kuelimika kijana, zinaa mwisho wake mauti.
 
Mkuu, kubali maumivu unless unataka kusambaratisha ndoa ya watu.
Mkuu ulidanganywaje hadi ukaingia peku peku hata kama uliamua kumpa mshedede huyo mama?
 
...eti tukajikuta tumeduu hivyo hivyo... Imoeee.... Halafu unajisifia foto copy na wewe! Kama ukitaka kulinda ndoa na familia yako, Achana na ufotocopy, achana na huyo malaya wako, yeye akuthibitishie kuwa huyo ni mtoto wako. Kwa ujasiri gani wa kutembea na mke wa mtu bila kinga? Hata kama alikuwa gf wako lakini sasa kaolewa muda mrefu. Na kama uliduu hivyo hivyo kwa huyo malaya wako ni mara ngapi umefanya the same kwa mademu wengine? Wangejua ulipo wangeshakuletea nao fotocopy zako. Utawapokea pia? Huko masomoni ulisomea nini mwenzangu? Nakushauri tubu dhambi na uache uzinzi, haukuongezei chochote ila mausumbufu na kukosa maraha. Tulia utunze familia yako, jaribu kuelimika kijana, zinaa mwisho wake mauti.

Pole kijukuu maake uwezo mdogo wa maneno yako uliyotoa hapa yanaonehsa jinsi ambavyo bado akili yako ni changa but usijali ukikua utayaona eeehh
 
Mkuu, kubali maumivu unless unataka kusambaratisha ndoa ya watu.
Mkuu ulidanganywaje hadi ukaingia peku peku hata kama uliamua kumpa mshedede huyo mama?

Osaka hizi mambo zingine zinakunjaga tuy zenyewe yaani nilipomaliza tuu ndo nikajigundua kuwa sikuwa nimevaa kinga but thank God sikunasa miwaya coz nilipima mara kadhaa kabla kabla sijaingia kwenye serious relationship nyingine
 
Kitanda hakizai haramu. Mtoto ni wa baba mwenye ndoa si wako ingawa kafanana nawe. Usikubaliani na huyo mama anaye taka kukupatia mtoto. Duniani wawiliwawili. Potezea.
 
huyo mwanamke anataka wewe ukamchukue huyo mtoto au ufanyeje?na huyo mume wake akijua hili swala unazan atakaa kimya?
achana na huyu x wako,coz ataleta kwake na kwako
 
Kabla sijatoa maoni ningependa kujua ikiwa huyo mtoto wako wa ndoa alizaliwa kabla au baada ya ndoa.
Nitarudi kutoa maoni baada ya jawabu yako.
 
Osaka hizi mambo zingine zinakunjaga tuy zenyewe yaani nilipomaliza tuu ndo nikajigundua kuwa sikuwa nimevaa kinga but thank God sikunasa miwaya coz nilipima mara kadhaa kabla kabla sijaingia kwenye serious relationship nyingine

Mkuu, let bygones be bygones! Stopisha biashara na huyo mama, najua roho yako inauma kwa ajili ya mtoto ambaye ni pure
damu yako, ambaye analelewa na kidume
mwenzio. Achana na biashara ya DNA, c'se ukijua beyond reasonable doubt kuwa mtoto ni wako, mkuu utakosa ile kitu inaitwanga peace of mind joo. Tulia mazee. Achana na ile mambo ya kukumbushia mshedede kwa bibi yako ya zamani.

bibi yako
 
Back
Top Bottom