Kindimbajuu
JF-Expert Member
- Jul 8, 2009
- 710
- 243
kijijini amerudi kuwa ndoa imevunjika au likizo??.Kwanza nianze kwa kuwasalimia Great Thinkers na naamini mtanipa ushauri wa Hekima na Busara.
Mimi ni kudume ambaye kwa sasa nina mke na watoto watatu kwa ufupi niko kwenye ndoa huu mwaka wa 6.Kabla ya kuwa na mke niliye naye nilikuwa na uhusiano na mwanamke mwingine kwa muda wa miaka 6 na hatukuendelea na uhusiano si kwa sababu nyingine bali ni haraka yake ya kutaka kuolewa kipindi nikiwa bado masomoni.So aliniuliza kama niko tayari kumuoa na kweli sikuwa tayari so akaamua kuolewa na mwanamume mwingine.
Nilirudi nyumbani kwa ajili ya likizo nikakuta tayari ameshaolewa na ana takribani miezi miwili kwenye ndoa but aliposikia nimerudi alinitafuta na akadai kuwa mwanamume aliyenaye hampi shughuli kama aliyokuwa akipata toka kwangu hivyo nikajikuta tumeduu hivyo hivyo.Hiyo ilikuwa ni mara moja tu na hatukuwahi kurudia tena manake na mimi nilikaa muda mfupi tu nikawa nimeoa.
sasa Ishu ilianza kipindi huyu mpenzi wa zamani akiwa mjamzito coz aliniambia kuwa huo mzigo ni wangu na alinitegeshea kwa makusudi ila nilipuuzia kwa kuamini zilikuwa ni stori za kujifurahisha lakini hali imekuwa mbaya zaidi hivi majuzi baada ya yeye kurudi kijijini kwetu akiwa na mtoto wake huyo mwenye miaka 8 kwa sasa kwani ni carbon copy yangu na hata mama yangu mzazi alipomuona alinipigia simu na kuniambia hilo hilo kwani akisimama na mwanange mwenye miaka 6 kwa sasa ni kama mapacha.
Nifanyeje sasa na kila mara anapigia simu kuniambia kuwa binti yako anakusalimia na mwenyewe nilipomwona nikataka kuzimia coz ananifanana koprait.
sidhani kama ni busara kwenda kutafuta mtoto ndani ya ndoa ya mtu. sikushauri kuhangaika na mtoto aliye kati ya ndoa ya watu.
labda kama unaujasiri, uthibitishe wewe na huyo mwanamke , kwa mume wa huyo mwanamke kuwa wewe ni baba wa mtoto, ili upate huyo mtoto, lakini kumbuka unavunja ndoa ya mwanamume mwenzio