Ijumaa njema wadau,
Wiki iliyopita yule mwanadada maarufu katika mtandao wa kijamii wa instagram anayeishi nchini marekani, Mange Kimambi aliandika kwenye akaunti yake ya instagram kuwa David Kafulila na mke wake Jesca Kishoa wameonekana wakila bata katika hoteli ya slip in iliyoko Kariakoo ambako Jesca amefikia pamoja na wabunge wenzake wa chadema kwa ajili ya kushiriki mashindano ya michezo ya wabunge wa Afrika Mashariki yanayofanyika jijini Dar es salaam. Chanzo cha taarifa ya Mange ni mbunge mmoja mwanamke wa chadema kwani kwa style ya uandishi wa mwanadada huyo huanza kwa kunukuu maneno ya mtu aliyempa taarifa.
Habari za uhakika zinasema kuwa ni mbunge huyo ambaye ndiye chanzo cha taarifa hiyo na ambaye inasemekana yuko karibu sana mh. Mbowe alimpigia simu Mbowe na kumuelea hali hiyo na jinsi ambavyo wabunge wengine hawakufurahishwa na kitendo cha kishoa kwenda na mumewe hotelini hapo kwa mbwembwe huku akijua kabisa amekisaliti chama. Mbowe aliahidi kulifanyia kazi suala hilo
Ikumbukwe kuwa mara tu baada ya Kafulila kujiondoa chadema, mke wake aliitisha vyombo vya habari na kukanusha sababu alizozitoa mumewe za kujiondoa chadema huku akimuona mtu asiye na msimamo. Ni mange kimambi aliyemtaka Jesca Kishoa kuvunja ndoa yake na Kafulila kama kweli aliyoyasema mbele ya vyombo vya habari alikuwa anayamaanisha kweli, la sivyo ilikuwa ni janja tu ya kutaka kuwapa imani chadema. Ili wasimchukulie hatua ambazo pengine zingekuwa ni pamoja na kumfujuza chama . Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema alishaonesha dalili za Kishoa kufukuzwa uanachama kutokana na andiko lake kwenye mtandao wa twitter.
Kutokana na sakata hilo la Kafulila, Jesca Kishoa na chadema, jana kamati kuu ya chadema imeazimia wabunge wote wa chama hicho wanaoshiriki mashindano ya wabunge wa Afrika Mashariki kujiondoa mara moja katika mashindano hayo kwa kisingizio cha kupinga kile ambacho wenyewe wanakiita ukandamizaji wa demokrasia, sababu ambayo haina mashiko kwa sababu kelele zao za ukandamizwaji wa demokrasia zimeanza tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani mwaka 2015 na wakati wanawaruhusu wabunge wao kushiriki mashindano hayo walikuwa wanalijua hilo.
Wiki iliyopita yule mwanadada maarufu katika mtandao wa kijamii wa instagram anayeishi nchini marekani, Mange Kimambi aliandika kwenye akaunti yake ya instagram kuwa David Kafulila na mke wake Jesca Kishoa wameonekana wakila bata katika hoteli ya slip in iliyoko Kariakoo ambako Jesca amefikia pamoja na wabunge wenzake wa chadema kwa ajili ya kushiriki mashindano ya michezo ya wabunge wa Afrika Mashariki yanayofanyika jijini Dar es salaam. Chanzo cha taarifa ya Mange ni mbunge mmoja mwanamke wa chadema kwani kwa style ya uandishi wa mwanadada huyo huanza kwa kunukuu maneno ya mtu aliyempa taarifa.
Habari za uhakika zinasema kuwa ni mbunge huyo ambaye ndiye chanzo cha taarifa hiyo na ambaye inasemekana yuko karibu sana mh. Mbowe alimpigia simu Mbowe na kumuelea hali hiyo na jinsi ambavyo wabunge wengine hawakufurahishwa na kitendo cha kishoa kwenda na mumewe hotelini hapo kwa mbwembwe huku akijua kabisa amekisaliti chama. Mbowe aliahidi kulifanyia kazi suala hilo
Ikumbukwe kuwa mara tu baada ya Kafulila kujiondoa chadema, mke wake aliitisha vyombo vya habari na kukanusha sababu alizozitoa mumewe za kujiondoa chadema huku akimuona mtu asiye na msimamo. Ni mange kimambi aliyemtaka Jesca Kishoa kuvunja ndoa yake na Kafulila kama kweli aliyoyasema mbele ya vyombo vya habari alikuwa anayamaanisha kweli, la sivyo ilikuwa ni janja tu ya kutaka kuwapa imani chadema. Ili wasimchukulie hatua ambazo pengine zingekuwa ni pamoja na kumfujuza chama . Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema alishaonesha dalili za Kishoa kufukuzwa uanachama kutokana na andiko lake kwenye mtandao wa twitter.
Kutokana na sakata hilo la Kafulila, Jesca Kishoa na chadema, jana kamati kuu ya chadema imeazimia wabunge wote wa chama hicho wanaoshiriki mashindano ya wabunge wa Afrika Mashariki kujiondoa mara moja katika mashindano hayo kwa kisingizio cha kupinga kile ambacho wenyewe wanakiita ukandamizaji wa demokrasia, sababu ambayo haina mashiko kwa sababu kelele zao za ukandamizwaji wa demokrasia zimeanza tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani mwaka 2015 na wakati wanawaruhusu wabunge wao kushiriki mashindano hayo walikuwa wanalijua hilo.