Mke wa jirani amenieleza mapungufu ya mumewe

Yofav

JF-Expert Member
Mar 12, 2021
3,951
6,853
Ni katika hali ya story za kuhusu masuala yanayohusu mazingira tunayoishi, Hapa namaanisha kuhusu usafi na mengineyo na Mimi ni single boy hivyo sina wa kusimamia masuala hayo zaidi ya mimi mwenyewe ndipo tukajikuta tunazungumzia masuala ya mahusiano na ndipo mwanadada huyu akaenda direct kwenye topic ya wivu.

Kuhusu wivu akaanza kumkandia mumewe kwamba ana wivu wa Kimbatu (wivu wa kijinga) kwani hajiamini hata kidogo na wala hamuamini yeye mwenyewe... Picha linaanza jamaa anamkagulia simu kila wakati, Imefika hatua jamaa ame-divert simu yake kwamba kabla simu au message yoyote haijafika kwa mwanadada huyu basi inapita kwanza kwa jamaa, Mwanadada anaongea kwa uchungu sana kuonesha hali hiyo kwamba inamkwaza sana na kumfanya ahisi kama anaishi gerezani, Anasema kila simu itakayopigwa au message kuingia akiwa na jamaa yake ndani basi ni lazima aulizwe "Nani huyo..." kwa sauti yenye tempa😁, Muda wote huo nilimsikiliza kisha kumuuluza "Lakini Happy kama wewe ni muaminifu kwake basi kwanini ukwazike yeye kujihakikishia?" Mwanadada yule hakuridhia majibu yangu bali aliendelea kuelezea tu jinsi gani anavyokereka na mwenendo wa jamaa

Mwanadada amefunguka mengi sana ila wakati anataka kuelekea kwenye kuongea madhaifu ya jamaa kitandani mimi nikamkatisha kwa kujipokelesha simu ya uwongo na kweli na kumuacha kwenye mataa mwanadada yule huku nisichangie neno lolote wala kumpondea jamaa. Ama kweli mimi na wana ni dam dam.

Mwisho: Wakuu acheni kukagua simu za wanawake zenu kiasi wakajua mnawafuatilia, Hiyo ni ishara kwamba hujiamini na hilo ni jambo ambalo linakushusha thamani kwa mwanamke ndani ya dk 0, Kingine jinsi unavyoonesha udhaifu wa kumpenda mwanamke na kuwa na wivu wa hali ya juu ndipo unapompa hamasa ya yeye kutaka ku-teste the new test.
 
Unapiga lini ?

20230516_184957.jpg
 
Tulipoambiwa tuishi nao kwa akili ni kwa sababu ni akili pekee ndio zitakazo muweka salama mwanaume mbele ya uso wa mwanamke.........

Katika akili ya kawaida na jinsi ulivyotanabaisha ni kuwa matumizi yako ya akili mbele ya mwanamke yapo chini sana na hilo linaweza kukuletea matatizo au kuyaangamiza maisha yako.....kitendo Cha wewe kukaa faragha na mke wa mtu na kukuelezea mambo yote hayo na wewe kuyaamini na kuyabeba kama yalivyo ni uthibitisho kuwa matumizi yako ya akili yako chini sana mbele ya kiumbe mwanamke.........

Moja ya matumizi sahihi ya akili kwa mwanamume ni kujua na kuheshimu mipaka yake dhidi ya mwanamke ambaye si halali yake na kwa kufanya hivyo utakuwa umeyaepusha maisha na majanga makubwa na hata kifo........

Muendelezo wa hizo faragha kutazaliwa jambo ambalo litakuletea matatizo makubwa.... kumbuka sio wote wanaohukumiwa juu ya mambo hayo kwa wamelala nao bali hata mazingira tatanishi yanaweza kuwafanya watu waamini hivyo........


Word is enough for the wise
 
Mwisho: Wakuu acheni kukagua simu za wanawake zenu kiasi wakajua mnawafuatilia, Hiyo ni ishara kwamba hujiamini na hilo ni jambo ambalo linakushusha thamani kwa mwanamke ndani ya dk 0, Kingine jinsi unavyoonesha udhaifu wa kumpenda
Na wewe tafuta KAZI za kufanya acha kukaa na Wake za watu na kuongea umbea, wanaume wenzako wameoa na wanaenda kutafuta pesa, wewe unakaa home na kufanya usafi kwenye vyoo vya wapangaji wenzio. Stop 🛑 🚏
 
Ndoa lazima ziwe na miundo miwili.
1. Urafiki na utani
2.Ufalme.
Lazima muwe marafiki na watani, kila mmoja kuwa huru na kufurahi.
Tukienda hatua ya pili ufalme. Hapa mke lazima ajue kuwa mume ni mfalme muda wowote anaweza kuamuru lete simu na kuanza kuipekua na kumrejeshea.
Sasa wewe ishi na mwanamke kwa kanuni nambari 1 tu utaona kilio chake.
Acheni mapenzi ya kizungu, hamtatoboa, akili na hulka ya mwanamke wa kiafrika ina utofauti na wazungu.
 
Ni katika hali ya story za kuhusu masuala yanayohusu mazingira tunayoishi, Hapa namaanisha kuhusu usafi na mengineyo na Mimi ni single boy hivyo sina wa kusimamia masuala hayo zaidi ya mimi mwenyewe ndipo tukajikuta tunazungumzia masuala ya mahusiano na ndipo mwanadada huyu akaenda direct kwenye topic ya wivu.

Kuhusu wivu akaanza kumkandia mumewe kwamba ana wivu wa Kimbatu (wivu wa kijinga) kwani hajiamini hata kidogo na wala hamuamini yeye mwenyewe... Picha linaanza jamaa anamkagulia simu kila wakati, Imefika hatua jamaa ame-divert simu yake kwamba kabla simu au message yoyote haijafika kwa mwanadada huyu basi inapita kwanza kwa jamaa, Mwanadada anaongea kwa uchungu sana kuonesha hali hiyo kwamba inamkwaza sana na kumfanya ahisi kama anaishi gerezani, Anasema kila simu itakayopigwa au message kuingia akiwa na jamaa yake ndani basi ni lazima aulizwe "Nani huyo..." kwa sauti yenye tempa😁, Muda wote huo nilimsikiliza kisha kumuuluza "Lakini Happy kama wewe ni muaminifu kwake basi kwanini ukwazike yeye kujihakikishia?" Mwanadada yule hakuridhia majibu yangu bali aliendelea kuelezea tu jinsi gani anavyokereka na mwenendo wa jamaa

Mwanadada amefunguka mengi sana ila wakati anataka kuelekea kwenye kuongea madhaifu ya jamaa kitandani mimi nikamkatisha kwa kujipokelesha simu ya uwongo na kweli na kumuacha kwenye mataa mwanadada yule huku nisichangie neno lolote wala kumpondea jamaa. Ama kweli mimi na wana ni dam dam.

Mwisho: Wakuu acheni kukagua simu za wanawake zenu kiasi wakajua mnawafuatilia, Hiyo ni ishara kwamba hujiamini na hilo ni jambo ambalo linakushusha thamani kwa mwanamke ndani ya dk 0, Kingine jinsi unavyoonesha udhaifu wa kumpenda mwanamke na kuwa na wivu wa hali ya juu ndipo unapompa hamasa ya yeye kutaka ku-teste the new test.
niwe dhaifu kwa kukagua simu?
 
Huyo sio mke, usishangae kesho akamwambia jamaa yake umemtongoza, kaa naye mbali, mambo ya simu inategemea, mimi sikagui simu lakini password lazima niijue na nikitaka kuiangalia sitegemei akatae, it goes both ways, anaweza kuangalia yangu pia sina shida
 
Back
Top Bottom